Posts

Showing posts from July, 2016

ZIJUE SIRI ZA UFALME WA GIZA!.

ZIJUE SIRI ZA UFALME WA GIZA!. Na Nickoso Mabena Bwana Yesu asifiwe Mtu wa Mungu Popote pale Ulipo, ninayo furaha leo hii kukuletea Ujumbe wa Neno la Mungu, Ujumbe huu ni Muhimu sana kwa Kila Mwanadamu aweze kuupata. Ninamshukuru Mungu pia kwa ajili ya watu wake aliowatumia kuniuliza Maswali, na wengine kunishauri niandae Somo kama hili, na hiyo yote ilikuja Baada ya Siku Moja kuandika Ujumbe Uliohusu UPASUAJI NA MATATIZO YA MATUMBO KWA WANAWAKE, na Niliandika kwenye ujumbe ule ya Kwamba hizo ni roho kutoka Kuzimu!. Watu wengi walinitaka nielezee maana ya roho kutoka kuzimu.. Somo hili nimeliita Zijue Siri za Ufalme wa Giza, na leo hii nataka nianze na Utangulizi tu wa Somo hili, ili upate Picha japo kwa kidogo, vitu nitakavyofundisha! NAMUOMBA MUNGU KWA AJILI YAKO ILI UPATE UFAHAMU WA KIROHO 👉Tunapaswa kujua ya Kwamba kuna Falme kuu Mbili katika Ulimwengu wa roho, 1.Ufalme wa Nuru 2.Ufalme wa Giza Falme hizi zinatenda Kazi na kuratibu Mambo mengi sana tunayoyaona na...

martha mwaipaja nifundishe kinyamaza click hapa

Image
wimbo wa mwimbaji martha mwaipaja nifundishe kunyamaza

PICHA NA TAARIFA KAMILI ZA AJALI ALIYOPATA BAHATI BUKUKU

Image
PICHA NA TAARIFA KAMILI ZA AJALI ALIYOPATA BAHATI BUKUKU Gari waliyokuwemo Bukuku na wenzake. Bahati Bukuku akiwa kwenye hospitali ya Wilaya ya Kongwa. Usiku wa kuamkia leo, muimbaji nyota wa nyimbo za injili, Bahati Bukuku pamoja na wasaidizi wake, walipata ajali akiwa njiani kuelea Kahama kwenye huduma. GK ilikuripotia taarifa za awali , na hapa tunakuletea pcha kamili na taarifa rasmi ya jeshi la polisi mkoani Dodoma. Juhudi za kumhamishia Bahati Bukuku kuelekea Muhimbili kama ilivyopangwa awali zimeshindikana, kutokana na kushindwa kugeuka wala kuinuka - akiwa amelazwa. Tayari ndugu na marafiki walishafika kutoka Dar es Salaam, na watu kadhaa wa Dodoma na viunga vyake walipita kuwajulia hali na kuwafariji. Taarifa ya Jeshi la Polisi, Dodoma. Gari lenye namba IT 7945 Toyota Nadia likiendeshwa na EDSON MWAKABUNGU (31) mkazi wa Tabata Dar es Salaam liliacha njia na kugonga gema na kusababisha majeraha kwa watu watatu baada ya kugongwa na gari jingine...

WAIMBAJI WAJITOKEZA KUMFARIJI BAHATI BUKUKU MSIBA WA BABA YAKE

Image
WAIMBAJI WAJITOKEZA KUMFARIJI BAHATI BUKUKU MSIBA WA BABA YAKE Hizi ni baadhi ya picha za msiba wa baba mzazi wa mwimbaji gospel nchini Bahati Bukuku aitwaye mzee Lwaga Bukuku ambaye alifariki dunia hivi majuzi jijini Dar es salaam. ambapo msiba ulikuwa nyumbani kwa mwimbaji huyo maeneo ya Tabata, watu mbalimbali wakiwemo waimbaji wenzake Bahati kama David Robert, Jennifer Mgendi, Christina Shusho,Jane Misso, Christina Matai, Neema Gasper na wengine walifika nyumbani hapo kumpa pole,  mwili umesafirishwa kuelekea mkoani Mbeya kwa mazishi. Nyumbani kwa Bahati Christina Matai. Watu wakiwa msibani. Jane Misso akimsifu Mungu. Watu wakitoa heshima za mwisho. Msiba nyumbani kwa Bahati. Bahati akiwa na wafiwa wengine. Wafiwa wakipata chakula kabla ya ibada ya mazishi kuanza. Baadhi ya waimbaji wakiongozwa na Christina Shusho wakiwa msibani hapo. Neema Gasper akimsifu Mungu huku akipewa nguvu ...

SOMO: JINSI YA KULIELEWA NENO LA MUNGU - ASKOFU KAKOBE

Image
SOMO: JINSI YA KULIELEWA NENO LA MUNGU - ASKOFU KAKOBE Askofu Zachary Kakobe Tunaendelea tena leo, kujifunza Kitabu cha YOHANA katika Biblia zetu. Leo tunatafakari YOHANA 7:17-52. Ingawa kichwa cha somo letu la leo ni, “JINSI YA KULIELEWA NENO LA MUNGU“, kuna mengi zaidi ya kujifunza katika mistari hii. Tutayagawa mafundisho yote tunayoyapata katika mistari hii, katika vipengele kumi:- (1) JINSI YA KULIELEWA NENO LA MUNGU (MST. 17); (2) JINSI YA KUMTAMBUA NABII WA KWELI (MST. 18); (3) KUSHINDWA KWA WANADAMU WOTE KUISHIKA TORATI (MST. 19); (4) SABABU KUU YA KUMWITA MTUMISHI WA MUNGU KWAMBA ANA PEPO (MST. 19-20); (5) WAJIBU NA JINSI YA KUHUKUMU (MST. 21-24); (6) SABABU KUU YA WATU WENGI KUSHINDWA KUMPENDA MUNGU (MST. 25-29); (7) SAA YA KUKAMATWA (MST. 30); (8) NAMI NILIPO NINYI HAMWEZI KUJA (MST. 33-36); (9) MITO YA MAJI YALIYO HAI (MST. 37-44); (10) KOSA LA KUMHUKUMU MTU KABLA YA KUMSIKIA (MST. 31-32...

Mnatumwa kutangaza na kushuhudia Habari Njema!

Utume wa Kanisa unafupishwa kwa maneno ya Kristo katika Injili ya Marko anaposema “Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa” (Mk 16:15 – 16). Utume huu si jambo jingine bali ni uendelezaji wa habari njema ya wokovu ambayo Bwana wetu Yesu Kristo kwa hiyo aliutwaa ubinadamu wetu na kukaa katikati yetu. Habari hiyo ni “kuwahubiria maskini habari njema ... kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao na vipofu kuona tena, kuwaacha huru waliosetwa na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa (Lk 4:18 – 19). Hii inamaanisha kwamba utume wa Kanisa unapaswa kujikita katika kumwangalia mwanadamu aliyejeruhiwa, kumganga na kumfanya apate nafuu na kuiona tena huruma ya Mungu. Wajibu huu kama tunavyosisitiziwa sana katika mwaka huu wa Jubilei ya huruma ya Mungu huonekana vizuri zaidi kwa kuwaangalia wale waliosukumiziwa pembezoni na ambao sauti zao haziwezi kusikika. Mfano wa hawa ni yatima, wajane na wanyonge weng...

Pst Abiud Misholi Siku Moja

Image
Pst Abiud Misholi Siku Moja   MCH   ABIUDI  MCH   ABIUDI  

ABIUDI MISHOLI - NIWEWE JAWABU song

Image
ABIUDI MISHOLI - NIWEWE JAWABU