Mafundisho yao juu ya Vita vya Kiroho.
Mafundisho yao juu ya Vita vya Kiroho. Wanaigawa vita ya kiroho katika ngazi tatu. Kwanza, kuna kile wakiitacho mapambano ya “ngazi ya chini”, ambayo wanamaanisha kutumia mamlaka ambayo Mungu amelipatia kanisa lake kuwatoa mapepo toka kwa mtu mmoja mmoja. Hii imetolewa mfano wake vizuri katika Injili na Matendo ya Mitume na hivyo siyo jambo lenye kuleta hoja kwetu. Aina ya pili inaitwa mapambano ya “ngazi ya kishirikina” ambavyo wanamaanisha kuwa ni kukabiliana na kuzifunga roho za uchawi, dini ya kishetani, ibada za sanamu, na kadhalika, mambo ambayo kwa kawaida yanaleta athari zake ovu kupitia kwa mtu fulani binafsi. Ngazi ya “juu” ya mapambano ya kiroho inaitwa mapambano ya “kimkakati” au ya “kwenye anga za juu” ambapo maombezi yanahitajika ili kuzitambua na kuzifunga roho mbaya za ngazi za juu, au mamlaka na nguvu, ambazo zinatawala katika maeneo makubwa ya kijografia. Hizi ngazi mbili za mwisho ni mambo ya kukisia na ubunifu wa hawa waandishi wa kisasa, kama tutakavyow...