Mafundisho yao juu ya Vita vya Kiroho.



Mafundisho yao juu ya Vita vya Kiroho.

Wanaigawa vita ya kiroho katika ngazi tatu. Kwanza, kuna kile wakiitacho mapambano ya “ngazi ya chini”, ambayo wanamaanisha kutumia mamlaka ambayo Mungu amelipatia kanisa lake kuwatoa mapepo toka kwa mtu mmoja mmoja. Hii imetolewa mfano wake vizuri katika Injili na Matendo ya Mitume na hivyo siyo jambo lenye kuleta hoja kwetu. Aina ya pili inaitwa mapambano ya “ngazi ya kishirikina” ambavyo wanamaanisha kuwa ni kukabiliana na kuzifunga roho za uchawi, dini ya kishetani, ibada za sanamu, na kadhalika, mambo ambayo kwa kawaida yanaleta athari zake ovu kupitia kwa mtu fulani binafsi. Ngazi ya “juu” ya mapambano ya kiroho inaitwa mapambano ya “kimkakati” au ya “kwenye anga za juu” ambapo maombezi yanahitajika ili kuzitambua na kuzifunga roho mbaya za ngazi za juu, au mamlaka na nguvu, ambazo zinatawala katika maeneo makubwa ya kijografia.
Hizi ngazi mbili za mwisho ni mambo ya kukisia na ubunifu wa hawa waandishi wa kisasa, kama tutakavyoweza kuona. Ile ngazi ya pili haina umaarufu mkubwa na inaingiliana kwa kiasi fulani na ile ya tatu. Kwa hiyo nitazungumza kidogo juu ya ngazi hii ya pili, tutakapoangalia vifungu vinavyohusiana nayo. Lakini ni ngazi ile ya tatu ambayo mafundisho yao yanakazia, kwa hiyo kwa upana zaidi tutakuwa tunatazama ngazi ya mwisho, kwa vile ndiyo hasa inayowakilisha udanganyifu na hatari kubwa.
Ni namna gani roho hizi mbaya zinatambulikana na watu kukabiliana nazo? Sawa, kwa wale ambao wanaamini kuwa wameitwa ili kuhusika na aina hii ya vita, wanatumia muda wao mwingi katika maombi kutafuta kutambua kwa njia za karama za kiroho na “upambanuzi”, jina au aina ya roho (moja au zaidi ya moja) iliyoshikilia eneo fulani – inaweza ikawa ni roho ya kiburi, uchoyo, tamaa mbaya au uchafu, ndipo tena wanakabiliana nayo katika vita vya maombi na kuzifunga nguvu zake – hii inaweza ikachukua siku kadhaa au wiki kadhaa. Ili kutambua ni roho gani inatawala juu ya mji, wanafundisha pia haja ya kile wanachokiita kuwa ni “kutengeneza ramani za kiroho”, kazi ambayo inahusisha uchunguzi wa historia ya mji – hali ya mji huo kidini, kijamii na kikabila, na historia ya nyuma, hali kadhalika kuhusu matendo maovu yaliyofanywa katika mji huo, au kufanywa na mji huo, au yaliyofanywa dhidi ya mji huo – kurudi nyuma miaka zaidi ya mia au kama si elfu na zaidi! Inafundishwa kwamba tendo hili litatusaidia sana kuzitambua ni roho chafu za jinsi gani zinazoshikilia mji kwa nguvu sana ili kwamba tuweze kuomba kwa ufanisi dhidi yake na kisha kuzifunga nguvu zake! Nilishughulikia juu ya hoja hii ya kiushirikina katika ile makala yangu ya kwanza.
Baadhi ya hawa wahubiri wa kisasa wanasema kwamba hawataweza kuhubiri Injili katika eneo lolote lile hadi kwanza wawe wametambua roho mbaya zinazotawala na wakazifunga nguvu zake. Lakini sasa Yesu hakutumia mtindo huu katika mji wowote aliouendea. Hatusomi chochote kuhusiana na mtume Petro au Paulo akishiriki katika aina hii ya “vita vya kiroho” kabla hajautembelea mji wowote ule; au kuhubiri Injili hapo. Hatusomi chochote kile kuhusiana na mtume Paulo kuzifunga roho za uzinzi, uchoyo au tamaa mbaya kule kwenye miji ya Efeso au Korintho kabla hajaanza kazi yenye nguvu hapo. Wala hatusomi popote kwamba katika nyaraka zao kuwa mitume hao waliwasihi watakatifu kuomba dhidi ya roho za kimaeneo, kama hawa waandishi na wahubiri wa kisasa wanavyotutaka sisi tufanye!
Makosa Mawili ya Kimsingi
Fundisho hilo siyo tu kwamba ni nyongeza kwa Maandiko, bali kwa kweli linaielezea vibaya na kuidhoofisha kazi yote ya Kristo pale Kalvari na jinsi Injili ilivyo. Na tutaanza kwa kuyatazama makosa mawili ya kimsingi ambayo mafundisho hayo yanawatumbukiza watu ndani yake.
Kwanza, fundisho hili linakanusha au kupunguza ushindi mkamilifu ambao Yesu aliutimiza pale msalabani. Mafundisho yenyewe hauyakiri kikweli ushindi halisi ambao Kristo ameupata dhidi ya nguvu zote katika ulimwengu wa roho, kwa niaba ya kanisa lake, kadhalika na kwa ajili ya wanadamu, wala hawa walimu hawaheshimu kikweli na kujali mamlaka zote na haki ambazo Mungu anazo za kuwaelekezea watu wake na kujenga kanisa lake.
Kabla ya pale Kalvari, Yesu mwenyewe alikuwa akitembea huko na huko akihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu. Hali kadhalika aliwatuma mitume pamoja na wanafunzi kuhubiri Injili ya ufalme wa Mungu na kuwatoa watu mapepo na kuwaponya wagonjwa. Akiwa amepokea msamaha na ushindi juu ya majeshi ya uovu pale msalabani, Kristo aliita, akatuma na akawatumia mitume vile vile na watu wengine katika kulijenga kanisa lake. Tunajua kuwa watu wengi waliokolewa kupitia mahubiri ya mtume Petro. Filipo alitumwa na Mungu kuwageuza wengi watokane na dhambi na uchawi. Matendo 8. Na katika ile Matendo 11:19-21, tunasoma kuwa, “… mkono wa Bwana ukawa pamoja nao, wao … waliohubiri Yesu ni Bwana kwa mataifa na watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana”. Mtume Paulo aliitwa na Mungu, Matendo 26:13-18; katika ile Matendo 13:2 mtume Paulo alitumwa na Mungu. Watu hawa wote walihubiri neno la Mungu kwa watu wengine, wakikiri kile ambacho Kristo amekifanya pale Kalvari na watu wengi walimgeukia Bwana. Mitume waliwakomboa waume kwa wake pia kutokana na roho za uovu na waliyakemea mapepo yaliyokuwa yakitenda kazi ndani ya mtu mmoja mmoja. Matendo 13:8-11; 16:18; 19:12. Hayo yote yalitokea pasipo hata kupata mafundisho yahusuyo na pasipo matumizi ya mtindo huu wa kisasa ambao unaitwa “mapambano ya kimkakati”
Hebu niseme hapa kwamba inapaswa iwe wazi kwetu, kwamba sio mahubiri yoyote na kila mahubiri huwa na ufanisi. Mtume Paulo alikuwa makini katika kumhubiri Kristo, lakini yeye alijikabidhi mwenyewe kwa ndugu zake pamoja na kwa kanisa, naye alikuwa tayari kurejea nyumbani kwake katika mji wa Tarso, Matendo 9:26-31. Baadaye tunamkuta kama mmoja wa manabii na walimu huko Antiokia, Matendo 13:1. Paulo hakuhubiri tu mahali popote pale kulingana na mipango yake na ubunifu wake, bali akiwa na ushirika na Mungu na akimtii Roho na kanisa, Paulo aliitwa na Mungu kuihubiri Injili, Matendo 13:1, na alielekezwa na Roho maeneo ya kwenda na maeneo ya kutokwenda, Matendo 16:6 – 10. Hivyo mtume Paulo anasema katika Warumi 10:14 – 15. “…basi wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikiaje pasipo mhubiri? Tena wahubirije wasipopelekwa?” Mtume Paulo pamoja na wenzake walikuwa makini sana kuhusiana na wito huu wa kimungu – 1 Kor. 9:16,17 na alikuwa makini zaidi pia kuwa angeweza kufanya kazi vizuri tu kulingana na wito wake, 2 Kor. 10:13-18.
Ikiwa tutaenda mbali na wito wa Kimungu na karama; ikiwa tutaenda mbali na muda wa Kimungu katika maisha yetu; ikiwa tutaenda mbali na Neno la Mungu – basi tusitegemee kupata matunda ambayo Mungu anayategemea kutoka kwetu. Tunapaswa kuwa watumishi wa Mungu, hii ina maana kwamba tunatakiwa kufanya yale tu anayoyasema na kujikabidhi kwenye maelekezo yake na muda wake katika maisha yetu. Hatutakiwi pia kwenda mbali zaidi ya karama na wito wetu. Hii inaweza kuwa pengine ndiyo sababu wengine wanaenda pasipo kupelekwa? Inaweza kuwa ndiyo sababu kwamba wanapata mafanikio kidogo au hawaoni mafanikio kabisa kutokana na mahubiri yao. Juhudi ya jinsi hii ya wahubiri wasio na subira wanatafuta sasa kutunga au kubuni mtindo fulani au mbinu ambazo zitaifanya kazi yao iweze kufanya kazi vizuri na kuleta “mafanikio”! Inaweza ikawa ndiyo sababu wanaenda mbali zaidi ya yale ambayo yanafundishwa na Maandiko ili kwamba wapate haya? Ninafikiri kuwa mambo hayo pia yanachangia katika jambo hili lote la UInjilisti wenye mafanikio pamoja na kushughulikia “mbinu mpya”. Hii yote haimaanishi kuwa ikiwa tumetumwa na Mungu, basi siku zote tutaona ‘matokeo makubwa’, bali ikiwa tuna shauku ya kumtumikia Mungu na kumzalia matunda na kiukweli kupeleka Neno lake kwa watu, basi tutaenenda kwa kufuata Neno lake na Roho wake.
Kama tusomavyo Injili na Matendo ya Mitume, tunaona kwamba watu wa Mungu walihubiri na kushuhudia juu ya kifo chake na ufufuo katika utii wa amri zake na maongozi yake au kwa kadiri fursa zilipojitokeza. Ijapokuwa walifahamu kuwa Kristo ameangamiza mamlaka na uwezo, haina maana yoyote, kama tusomavyo katika habari zao, kwa watu wa Mungu kuchukua UInjilisti “katika mikono yao wenyewe” na kujaribu kuifanya kazi ya Mungu kwa ajili yake. Mitume hawakufanya mambo kwa kukisia pale walipokuwa wakilitumia neno la Bwana au walipotumia uwezo na mamlaka ambazo aliwapatia. Walimtii Mungu na Mungu aliwarejesha wengi kwake na akadhihirisha nguvu zake kuu. Na Mungu aliupata utukufu! Hayo yote yalitendeka pasipo hata kuzitambua au kuzifunga roho za kimaeneo! Hawakujaribu kuongezea chochote kile juu ya yale ambayo Mungu alisema na kuyafanya ili kuufanya uInjilisti uwe wenye mafanikio zaidi! Lakini hawa walimu wa kisasa pamoja na wahubiri wanathubutu kuonyesha kwa mafundisho yao, kwamba yale ambayo Kristo aliyafanya pale msalabani hayakutosha. Ndiyo, wanatangaza kwamba Kristo alipata ushindi pale msalabani, lakini inaonekana kana kwamba hakuzivunja mamlaka na enzi vya kutosha kwa ajili yao, kwa sababu wahubiri hawa wanaamini kuwa roho chafu bado zina haki kisheria kuwashikilia watu katika giza na kifungo na kuwa Injili haiwezi kupenya katika eneo linalotawaliwa na roho hizo. Wanafundisha kuwa mtu anahitajika kwanza kufanya “vita vya kiroho” ana kwa ana na mamlaka hizo pamoja na nguvu hizo kwa maombi, hadi kuzishinda nguvu zake kupitia maombi kwanza, kabla Mungu hajazirejesha roho za watu kwake! Mawazo ya aina hii kwa hakika ni ya jamii ya kiushirika tu na yenye milki ya ulozi zaidi kuliko kuwa na mawazo ya kimaandiko. Mtazamo huu juu ya aina hii ya roho ya kimaeneo pamoja na uwezo wao pamoja na aina hii ya kuzingatia katika maombi dhidi ya roho ya uovu, hayapatikani katika maandiko ya neno la Mungu. Mtazamo huu unaweza kumtukuza ibilisi kwa namna itakayowanyima watu wa Mungu ufahamu wa kweli na nguvu ya Kristo ndani ya watakatifu wake na kupitia kanisa lake. Inawafanya watu wamfikirie shetani zaidi badala ya kuweka mawazo yao kwa Kristo, na kwa jinsi hiyo wanampatia shetani uwezo zaidi na utukufu na kuwanyang’anya watakatifu ile imani yao ya kweli katika Mungu. Maandiko yanasema kwamba, “Ijapokuwa hatujayaona mambo yote yakitiishwa chini ya nyayo zake, lakini tunamwona Kristo.” Amina! Lakini sasa, badala yake walimu hawa wa kisasa wanatutaka sisi tuyaone mapepo! Ni mafundisho madhaifu na manyonge kama vile yenyewe yalivyo si ya kibiblia. Na hao walioyahamasisha mafundisho hayo ndio huwa wa kwanza kukubali katika vitabu vyao kwamba watu wameharibiwa walipokuwa wanajaribu kutumia mbinu hizo. Mafundisho hayo ni kashfa dhidi ya mamlaka ya Mungu na shambulizi dhidi ya ushindi kamili wa Kristo alioupata pale Kalvari, ambao ndio unaomruhusu kulijenga kanisa lake kulingana uradhi wa mapenzi yake mwenyewe. Katika uweza ambao Mungu aliutumia katika kumfufua Kristo kutoka katika wafu. (Efe 1: 19-23)!
Ndiyo tunatambua kile kinachofundishwa na maandiko, kwamba mfalme wa uweza wa anga ni ile roho itendayo kazi sasa katika wana wa uasi; Efe 2:2. Shetani huzungukazunguka kama simba angurumaye akiwafunga wengi kuyatenda mapenzi yake na hafanyi lolote isipokuwa ni kuua, kunyang’anya na kuharibu. Yeye hudanganya na kuwafunga wengi katika vifungo. Mambo hayo pamoja na mengineyo yanafundishwa ndani ya maandiko, na wala hiyo sio hoja yetu tena hapa. Nami sisemi hapa kwamba hatuwezi kuomba kwa Mungu, kuhusiana na mambo ya aina hii; wakati ambapo tunajua hali na watu ambao wanahitaji neema ya Mungu, rehema pamoja na wokovu wake. Lakini linapokuja jambo la uenezi wa Injili na jinsi inavyoenezwa na kubadilisha maisha ya watu, ndipo tunaweza kusema kuwa mafundisho hayo ya kisasa yameenda nje ya maandiko, na yametumbukia katika kasoro na udanganyifu – yanawafanya watu wawe shabaha ya roho za udanganyifu. Wanakubali kuwa Kristo amepata ushindi pale kalvari dhidi ya shetani, lakini bado wanaamini kwamba wanatakiwa pia wapate ushindi zaidi juu ya roho zinazotawala ju ya maeneo yote yanayokaliwa na watu.
Ni nini kinaipatia roho hizo za kimaeneo haki ya kisheria kukamata mamlaka za aina hii juu ya watu, kiasi kwamba hata iifanye Injili isiwe yenye mafanikio katikati yao? Haya ati wanasema ni zile dhambi zilizopita za jumuia hiyo au mkoa na ile laana iliyowekwa juu yake kwa sababu ya dhambi hizo! Napenda niwaambie ukweli, wanachokifanya hawa walimu wa kisasa ni kuzijaza akili za watu wa Mungu mambo yasiyo ya kiInjili yenye ushirikina mtupu na yenye kasoro nyingi. Kristo amezichukua dhambi za ulimwengu mzima na amelipia gharama kubwa isiyohesabika ili kufanya hayo. Kristo ni mwenye mamlaka zote za juu – ni Mkuu. Shetani anaweza tu akaenda pale ambapo Mungu amemruhusu kwenda. Sawa, maandiko yanakiri kuwa ipo haja ya maombi, kuhubiri, uInjilisti, kazi pamoja na ukombozi wa mtu mmoja mmoja kutokana na mapepo; lakini kadiri ya haja ya kuihubiri Injili inavyohusika, bado maandiko hayakiri kwamba kuna haja ya toleo lingine zaidi ya lile alilolinunua tayari Kristo pale msalabani kwa ajili ya ulimwengu wala maandiko hayakiri kwamba “dhambi zile za kihistoria” zilizopita za maeneo ndizo zinaipatia roho za kimaeneo haki ya kisheria kuzuia Injili; wala pia maandiko hayakiri kuwa ipo haja ya watakatifu kujiingiza moja kwa moja katika makubaliano ya kiroho na hizo roho za kimaeneo kana kwamba roho hizo zinahitajika kufungwa kabla ya Injili kufanyika na kuenezwa kwa mafanikio yanayopaswa ( tafadhali angalia makala yangu ya kwanza ambamo jambo hili limeelezwa kwa undani zaidi ).
Wakati mtume Paulo alipokuwa Athene, hawakupatikana watu wengi waliomgeukia Mungu lakini pamoja na hali hiyo, si Paulo mwenyewe wala si maandiko ya Neno la Mungu yanapohesabu hali hiyo ya watu kutoipokea Injili kuwa ilisababishwa na nguvu kuu na mamlaka au haki ya roho za uovu kupinga Injili au kazi ya Mungu. Mtume Paulo hakuianza kuzishughulikia roho za kimaeneo katika maombi kwa sababu ya kuonyesha “upungufu wa mafanikio” katika huduma yake. Mtume Paulo alikuwa na ufahamu mkubwa zaidi na mafunuo kuliko hawa walimu wa kisasa, lakini yeye hakukimbilia kwenye “mbinu za kiwango cha kimkakati” ili kuzishinda “roho ya kuabudu sanamu” ambazo zilidhaniwa “kutawala” katika mji wa Athene, katika jitihada yake ya kuushinda upungufu huu wa mwitikio katikati ya watu. Unaona, hawa walimu wa kisasa wao wanasema kwamba, watu kwa kweli hawapo huru kuitikia Injili hadi hapo tutakapokuwa tumezifunga roho za kimaeneo! Mmoja wa waandishi, kwa kweli anapendekeza kuwa roho za kimaeneo zinazotawala kule Athene, zilikuwa zenye uwezo mkubwa kiasi kwamba zilimfanya mtume Paulo kuzishindwa na eti hiyo ndiyo sababu alipata mafanikio kidogo sana huko! Lakini sio Paulo wala maandiko ya neno la Mungu yanayohitimisha jambo hilo kuhusu aina hii ya “upungufu wa mafanikio”. Badala yake, mtume Paulo yeye anaendelea mbele na safari yake kwa mapenzi yake Mungu na mpaka anapoingia katika mji wa Korintho, hatuoni popote pale panapomuonyesha akijishughulisha na kazi ya kuzifunga roho za kimaeneo, na bado watu wengi sana walimgeukia Bwana. Maandiko hayaelezei sababu hasa inayofanya watu wengi zaidi wamgeukie Bwana katika eneo moja kuliko jingine, lakini yanatupa vidokezo na kutuelekeza kwenye kanuni fulani fulani, ambazo tutaziangalia hivi punde.
Lakini jambo moja lenye uwazi ni kwamba maandiko hawayahesabii “mafaniko” au “kupungua kwa mafanikio” kwamba imetokana na mtu mmoja ambaye ameweza kuzishinda roho za kimaeneo zinazotawala au la.
Ninadhani kuwa kama hawa walimu wa kisasa wangekuwepo kule nyakati zile za Paulo alipotembelea Athene, wangeweza kushauri kuwa Paulo aweze kuhudhuria masomo katika moja ya seminari ya Kithiolojia ili aweze kujifunza kwanza “kanuni za kukua kwa kanisa”. Pengine wangeweza kumwelezea pia kuwa mtindo wake anaoutumia katika UInjilisti bila shaka “haufanyi kazi” vizuri na hivyo anapaswa kuzisomea “mbinu mpya za mafanikio” ya uenezaji wa Injili, ambazo ndizo zimethibitishwa kuleta mafanikio! Wangeweza kumwambia kuwa yote aliyoyafanya amekosea kwa sababu tatizo halikuwa ni Wathene binafsi isipokuwa ni ile roho ya kieneo ya kuabudu sanamu ndiyo iliyokuwa inawazuia watu kule wasiweze kuiitikia Injili. Mtume Paulo angelazimika kufundishwa vita vya kiroho iwapo angependa kuona mafanikio katika kuieneza Injili! Angepaswa kujifunza kuhusu kutambua majina ya roho chafu za kimaeneo na namna ya kuzikabili katika kuzifunga kwa maombi! Asingetazamia kupata mafanikio hadi kwanza afahamu jinsi ya kuyafanya mambo haya! Lakini sasa hebu fikiria jinsi Paulo alivyoweza kuwashughulikia walimu wa uongo walionyemelea makanisa ya Galatia; sifikirii kwamba angeweza kuvutiwa kwa vyovyote vile, badala yake angeweza kuwakemea kwa nguvu kwa ajili ya kuichafua Injili ya Kristo.
Hii ndiyo sababu inayonifanya niseme kwamba, mafundisho hayo wanayotuletea ni kashfa dhidi ya mamlaka na busara za Mungu, ambaye huwaita na kuwatuma watu kwenda kuhubiri Injili kulingana na amri na mafundisho ambayo ameyaweka kwa ajili yetu. Hawa waandishi wa kisasa wanaweka busara yake Mungu na mamlaka za utawala wake katika maswali. Wangeweza kuiita huduma ya Paulo kwa ajili ya watu wa Athene ni jambo “lililoshindwa”. Wako makini kutafuta mafanikio kiasi kwamba wanadiriki kuisukumilia mbali amri ya Kristo – ya kwenda ulimwenguni kote kuihubiri Injili – sasa kinyume chake wao wanazunguka huku na huko wakianzisha amri zao wenyewe, na hivyo wanajiweka kinyume na busara za mamlaka ya Mungu na utawala wake juu ya mambo haya.
Hata kama Mungu alibariki au kama aliwaruhusu waweze kujaribiwa, hata kama kulikuwa na mwitikio mkubwa wa watu au kidogo – bado mitume wa mwanzoni kabisa, wao pamoja na kanisa waliendelea kumwangalia Mungu; wakijikabidhi kwake, wakimwamini yeye na kumtukuza yeye! Hivyo ndivyo walivyofanya! Na kama hapakuwepo na mwitikio sana, hawakumtilia shaka Mungu na kuanza kukimbia huko na kuko kujifunza na kubuni “kanuni mpya za ukuaji wa kanisa”! Wao walikuwa wakiomba na wakihubiri na walikuwa imara katika imani na upendo; kama vile tusomavyo katika kitabu cha Matendo ya Mitume, lakini wao pia hawakujishughulisha katika aina ya maombi yanayohusika na kuzishambulia roho za kimaeneo kama ambavyo inavyohamasishwa na waandishi hawa wapya.
Ijapokuwa wanakiri juu ya ushindi wa Kristo pale Kalvari, lakini mafundisho yao hayo yanaufanya wokovu wa roho za watu uonekane kuwa unategemea matokeo ya aina fulani ya mapambano ya ana kwa ana kati ya majeshi ya kiroho ikiwepo roho chafu kwa upande mmoja, ikipambana na karama za Roho na maombezi ya Wakristo kwa upande mwingine; vita hiyo inayoelezwa humo ni ubunifu wa akili zao wenyewe tu ( ambayo wanaiazima kutoka kwenye milki za ulozi. Vitabu vya ubunifu – kama vile kitabu cha Frank Perret ) na vinajaribu kuongezea kitu kingine juu ya ushindi ambao Kristo aliupata pale Kalvari (msalabani). Katika maandishi yao, wakati mwingine inatolewa mfano wa nguvu za upinzani zilizo sawa sawa zikipigana dhidi ya roho. Wanaonyesha kuwa iwapo hutazishinda roho za kimaeneo zilizo za kienyeji na za kimaeneo zinazomiliki eneo fulani, basi kazi ya Injili na wokovu wa nafsi haiwezi kufanikiwa ipasavyo. Katika kutimiza hamu yao ya kupata “mitindo ya mafanikio”, wahubiri hawa pamoja na waandishi wao hawajikabidhi katika Neno la Mungu na maelekezo yake ambayo Yesu ameyakamilisha pale msalabani – wanafanya hayo yote kwa ajili tu ya kutafuta matokeo. Nasema tena kwamba mawazo hayo ni ya kuanzishwa toka duniani, hayamtukuzi Mungu, badala yake yanatukuza mafundisho yasiyothibitishwa ambayo husababisha machafuko na kukata tamaa, na zaidi ya yote yanamtukuza shetani.
Mafundisho yasiyothibitishwa ambayo husababisha kuchanganyikiwa na kukata tamaa.
Lakini hebu niseme hapa kuwa shauri lao halijathibitishwa! Bila shaka haionyeshi kwamba wanaweza kwa kweli kuonyesha kuwa jamii imebadilishwa kutokana na mafundisho hayo yao. Zaidi ya hayo yote, wengi wa mashabiki wa mafundisho hayo wanaishi Marekani (USA). Je huko kwao yameleta mabadiliko gani? Mchungaji mmoja wa kanisa moja kubwa kule New York aliwahi kuandika kitabu kuhusu kazi za kanisa lake na jinsi Mungu alivyopambana na mafundisho haya ya kisasa – na jinsi hata yeye alivyoumizwa katika moyo wake kuona jinsi ambavyo dhana hii isiyo ya kibiblia inavyoweza kushikilia akili za watu wa Mungu na inaendelezwa kufundishwa nchi nzima. Lakini analiweka swali lile lile na linalofanana – kuelezea ni kwa nini basi, iwapo mafundisho hayo ni ya ukweli, mbona hayabadilishi miji ya Amerika – tunaambiwa na watu wengine kuwa California ya kusini ni mji unaowakilisha kituo cha vivutio vya matamanio katika ulimwengu. Yako wapi basi mabadiliko hayo makubwa katika miji ya Marekani iwapo mafundisho hayo ni ya ukweli? Lakini mtu mwingine anaweza kuuliza hivyo hivyo kuhusu miji mingine mingi pamoja na nchi. Mafundisho hayo hayo yamekuwa yakiendeshwa Uingereza karibu miaka 15 sasa kwa kadiri ninavyofahamu, lakini sasa, yako wapi – basi mabadiliko hayo makubwa yaliyoahidiwa na mafundisho hayo? Ninafikiri kuwa watu wengi wangekubali kwamba, sio jamii tu yenye hali mbaya, isipokuwa kanisa leo limo katika hali mbaya zaidi; kwa kusema kwa ujumla, liko katika hali mbaya kuliko ilivyokuwa miaka 20 iliyopita. Tendo mojawapo lililosababisha machafuko, matengano, maumivu ya mioyo, kuchanika kwa makanisa, kadhalika na kugawanyika kwa makanisa, je huko ndiko kuzaa kwa wingi kwa imani hiyo mpya!
Mashabiki wa mafundisho hayo wametengeneza mkanda wa video, ili kuwashawishi watu waone namna ambavyo vita hivyo vya kiroho vinavyoleta mafanikio. Baadhi ya watu wengine ambao wamechunguza yale yanayodaiwa na mikanda hiyo ya video, kwa kuzuru hadi kwenye maeneo hayo waliyo chukulia mkanda huo pamoja na kupata habari sahihi za maeneo hayo, wanatuambia kuwa mambo mengi, yaliyodaiwa ndani ya mikanda hiyo yametiwa chumvi – na mara nyingi ni habari za uongo. Wale wanaoamini katika imani au mafundisho hayo, kwa uasili wa kutosha wanaamini kwamba “inafanya kazi” na wanajaribu kuonyesha watu kuwa ni kutokana na mtindo wao mpya wa kuomba dhidi ya roho za kimaeneo, ndiyo iliyoleta mafanikio makuu pale Injili ilipobanwa katika jumuiya fulani fulani. Lakini hatuoni kuungwa mkono na maandiko ya Neno la Mungu katika maeneo hayo; na wala haiwezi ikaonyeshwa kuwa hilo limekuwa ndiyo “ufunguo” au “jawabu” la ufanisi wa uInjilisti kwa namna ya kimatendo, mbali ya malalamiko ya hadithi zao.
Kwa kweli kitabu kimeandikwa ambacho nimekitaja hapo punde tu, kwa usahihi kabisa ni kwa sababu kumekuwepo na machafuko pamoja na maumivu ya moyo yaliyosababishwa na mafundisho hayo. Mwandishi wa kitabu hicho yeye mwenyewe pia anaamini katika vita vya kiroho dhidi ya roho, lakini anatueleza kuhusiana na kukata tamaa pamoja na hofu iliyowanyemelea wakristo waliokuwa na matazamio ya hali ya juu ya mafanikio kutokana na mafundisho hayo. Lakini hatimaye waligundua kuwa haikufanya kazi yoyote; ile kama walivyotarajia na hata ikawasababishia majanga! Hali hiyo imewasababishia kujisikia ni watu wawezao kunaswa na shida, hofu na machafuko! Ingawaje anajaribu kuonyesha kuwa mambo yaliwaharibikia kwa sababu ya ongezeko na ujinga wa watu wenyewe wa kutokujua kanuni za aina hii ya mapambano; mbali ya hayo yote kitabu hicho pia kinakazia ukweli kwamba, upepo huu mpya wa imani sio huo ambao mashabiki wake wamelalamikia kuwa ndio, na wala hautoi matokeo kwa namna ambayo hawa waandishi wapya wangetupelekea sisi tuamini hivyo.
Katika kitabu chake cha “Roho za Kimaeneo”, (kurasa za 17, 18), Wagner anakiri kuwa katika hali nyingi mtindo huu hautoi matokeo yanayokusudiwa. Anatoa sababu gani hapo? Haya, anatueleza kuwa shetani “anapinga mwenendo wa mambo”. Je, hii ina maana kwamba huyo shetani ana uwezo mkubwa kiasi kwamba watu hawawezi kuokolewa? Hapo haelezei kwa ufasaha. Lakini anatuelezea kuhusu uwezo, na werevu alionao na kwamba shetani anawapinga watakatifu, kupitia roho zenye kiwango cha ngazi tofauti; ili watu wasitambue mapenzi ya Mungu ipasavyo! Na kwamba kwa kadiri kiwango cha roho za kimaeneo kinavyozidi kuwa juu zaidi ndivyo nguvu zaidi zinahitajika ili kuzishinda! Hali kadhalika anatuambia kuwa Wakristo wengi hawajajiimarisha ili kukabiliana na aina hii ya roho za viwango vya juu. Kwa hivyo basi inaonyesha shetani anaweza kuzuia watu kuyatambua mapenzi ya Mungu katika mapambano haya; na hata kama watatambua aina ya roho zinazopaswa kushughulikiwa bado watu wengi hawana msimamo wa kiroho ili kuyashinda. Jambo hili humpatia mtu utukufu na humpatia pia uwezo mwingi shetani. Kwa hiyo hitimisho tunalolipata hapo ni kwamba wokovu wa roho za watu unategemea aina fulani ya watu walio jaliwa kuwa na uwezo wa kutambua mambo katika “ulimwengu wa kiroho”. Pasipo uwezo wa “kutambua” jina na tabia ya roho za kimaeneo na pasipo uwezo wa kiroho wa mtu binafsi pamoja na msimamo wa mtu binafsi kuyashinda hayo katika maombi – hakutakuwepo na ufanisi wa UInjilisti! Hakika, kama utasadiki porojo hizo zisizo na msimamo wa Kibiblia, basi wewe unaweza kuamini lolote lile! Ili kuonyesha jinsi mafundisho haya yanavyokaribia kuingia kwenye ulozi, hebu uniruhusu ninukuu yale anayoyasema mwishoni mwa ushauri wake hapo juu; anasema kuwa, “…. tunapogundua kuwa sisi ni muhimu katika kuzifunga (roho za kimaeneo) ….. tutafanya vema kutafiti uwezekano wa chanzo chake katika ulimwengu wa kiroho”. Kutafuta chanzo, na sio katika maandiko, isipokuwa katika ulimwengu wa kiroho! Je wanatutaka sisi tuwe waaguzi, wachawi au waangaliao mambo ya roho? Pasipo kuelewa, hivyo ndivyo inavyotendeka katikati yao. Wao hawaenendi kiroho, haupo utambuzi wa kiroho na kweli, hii sio maombi ya kiroho. Hivi sio vita vya kiroho – huu ni udanganyifu. Wanafanya mawasiliano ya kiuharamu na yenye hatari na ulimwengu wa maroho na hivyo hudanganyika (ninaposema ulimwengu wa kiroho ninamaanisha kuwa wanafanya mawasiliano na maroho maovu, au kujiweka katika hali inayoweza kuwashawishi na kudanganywa na maroho maovu). Tutaangalia zaidi kidogo hilo hapo baadaye kidogo. Lakini sasa hapa tunaona kwamba ili kuweza kusimulia kushindwa kwa mafundisho yao pamoja na maumivu ya moyo yaliyosababisha – wanatafuta kiurahisi tu kubuni makosa zaidi.
Niruhusu nitaje hapa yale ambayo nimewahi kuyasema mahala penginepo yaani, tunajua kwamba Bwana analijenga kanisa lake na anayaheshimu mahubiri ya neno lake na hakika hujali anapoona watu wake hujinyenyekeza wenyewe katika maombi na kuutafuta uso wake kwa mioyo yao yote. Inawezekana kuwa Mungu anafanya kazi katikati ya watu ambao baadhi yao viongozi wao huamini katika mafundisho haya na kuyashikilia, lakini kazi yake ya neema haiwezi kuhalalisha mafundisho hayo yote ambayo yameshikiliwa na watu ambao wanaweza wakawa ndio wanaoongoza kazi mahala fulani. Tunajua hivyo kutokana na historia, pia tunaweza kuziona kanuni hizo sisi wenyewe ndani ya maandiko pia. Lakini napenda niseme tena kuwa kule kuona Mungu akitembea katikati ya watu katika uweza wa kuokoa, haihalalishi kila mafundisho yaliyoshikiliwa na hao wanaokuwa katika uongozi wa sehemu fulani, na wapo mbali sana katika kuonyesha kuwa mtindo wao huo mpya kwa kweli unafanya “kazi” au kwamba mtindo huo ndio unaohusika katika kuwaleta watu wengi katika ufalme wa Mungu.
Katika mambo ya matukio ya kiroho ya nyuma na katika kujua kwa nini mambo hutokea au kutotokea, mara nyingi maandiko hayatoi jibu la maswali yetu au kufunua kila kitu. Na kutokana na hoja hiyo, Mungu anatuonya katika Kumbukumbu la Torati 29:29 kwamba “mambo ya siri ni ya Bwana Mungu wetu, lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele”. Hatutakiwi kupenyeza tu katika mambo ambayo Mungu hajatufunulia kwa neno lake. Ni busara zake Mungu, kwamba ameyaweka mambo fulani mbali na ufahamu wetu. Lakini tunatakiwa kuyazingatia kikamilifu mambo ambayo ametufunulia tayari. Hayo yatakuwa ni yenye kutuletea faida kwetu – katika kukuza ufahamu wa Mungu na kuimarisha imani yetu. Lakini katika jitihada zao za kupata matokeo wakati wote na katika sehemu zote, hawa wahubiri na walimu wa kisasa wanapenyeza kwenye mambo yasiyoonekana – ambamo wanajigamba juu ya maono yao, mafunzo yao, na uzoefu wao wa mambo ya juu – ambayo ni mazao ya akili zao za kimwili tu na wala hayailetei jamii mabadiliko katika maisha yao. Kama tunavyoambiwa katika Kolosai 2:18 na wala hawashikilii kichwa cha kanisa, Yesu Kristo. Ijapokuwa Mtume Paulo anaongelea maalum kuhusu wale wanaotafuta kuwarejesha watakatifu kwenye mila za kiyahudi, ile sura nzima Kolosai 2:6-19 inashauri sana juu yetu, kuhusiana na mambo haya ya mafundisho mapya.
Ulinganifu wa kimaandiko – kanisa katika kuomba.
Nyakati za matendo ya mitume kanisa lilijiheshimu na kuomba kwa jinsi ya tofauti kabisa ukilinganisha na hawa walimu wa kisasa wanavyoamuru. Kulipotokea mateso kule Yerusalemu, kanisa halikukabiliana na roho chafu katika maombi yao.
Kanisa halikukiri juu ya roho za kimaeneo kwamba ndizo zinazowashikilia wanaume na wanawake hata wasiupokee ufalme wa Mungu. Wao waliomba kwa Mungu na kukiri juu ya mamlaka zake na uungu wake. Kulikuwepo na upinzani mkali wakati huo ( kuliko hata ilivyo sasa naweza kusema ) juu ya kuihubiri Injili; naye ni nani anayeweza kupinga kwamba shetani anachochea ugumu wa mioyo ya hao wasiotaka kuamini ili wapinge kazi ya Mungu? Lakini sasa hebu sikiliza jinsi kanisa lilivyoomba katika Matendo 4: 24-30, kwanza walitangaza busara kuu na uweza, wa Mungu juu ya yote mengine, wakipokea maelekezo na hamasa kutoka katika maandiko ya neno la Mungu! Ndipo wakatangaza:
“. . . Basi sasa ee Bwana, yaangalie matisho yao, ukawajaalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, ukinyoosha mkono wako kuponya, ishara na maajabu zikafanyike kwa jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu”.
Hebu tazama hapo watumishi hao wametishwa, lakini maombi yao yameelekezwa kwa Mungu, wala hawayaelekezi dhidi ya aina yoyote ile ya roho za kimaeneo zinazotawala Yerusalemu, wanayohisia juu ya mamlaka za Mungu na za ushindi wake juu ya mambo yanayowapata, na wanaomba sio kwa ajili ya kukabililiana na roho za kimaeneo ili kwamba ziweze kufungwa, lakini wao wanaomba ili kwamba waweze kulisema neno lake kwa ujasiri na kwamba Bwana aweze kutenda kazi kwa nguvu katikati yao. Lakini hata hivyo wanakiri juu ya mamlaka za utawala wa Mungu na ushindi wake kupitia Kristo. Hayo hayawaelekezi kufuata mambo ya kuhisihisi – wao hawachukui kutoka kwa Mungu ule uweza wake mkuu na kutafuta kumtumikia kwa ajili ya kutimiza matakwa yao na mipango yao kwa ajili ya ukuaji wa kanisa. Isipokuwa wanabakia wakiwa wamejikabidhi kwa Mungu na katika busara zake wakikiri kuwa wao ni watumishi wake tu. Hilo ndilo kanisa ambalo linamwinua Yesu juu zaidi kuliko chochote kile. Na ijapokuwa wanadamu na mapepo wanaweza kupanga, wao wanaendelea kubakia wakiwa wamekaza macho yao kumwelekea Kristo- na kile alichokikamilisha kupitia kifo chake na ufufuo wake – yote mawili katika fikara zao na maombi yao. Hawatafuti kuongezea chochote kile juu ya ushindi kamili pale Kalvari, au kunyang’anya uwezo wake na maana yake kwa kuhesabia uwezo huo juu ya “roho za kimaeneo” ambao hawanao! Maombi yao yanakazia macho kwa Kristo na mamlaka zake na wanamtukuza yeye, sio shetani au roho za kimaeneo.
( Kuhusiana na maombi na kanisa, vile vile na kuhubiri Injili kama njia ya Mungu ya kuokoa hao waaminio, tafadhali soma sehemu ya pili ya makala ya kwanza ya “Kutubu kwa ajili ya Dhambi za Taifa”)
Na ni kweli tunaona kwamba wanayo sababu nzuri inayowafanya wafikiri na kuomba namna hiyo. Katika Wakolosai 2:15, tunasoma kuhusu kifo cha Kristo pale Kalvari kwamba; “… akisha kuzivua enzi na mamlaka na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri akazishangilia katika msalaba huo”. Na kwa hiyo Mungu alikuwa na uwezo wa “kutukomboa kutokana na nguvu za giza na kutuingiza katika ufalme wa mwana wake mpendwa”.
Na katika Waebrania 2:14 tunaambiwa kuwa, “Yesu Kristo alishiriki damu na mwili vivyo hivyo;.ili kwamba kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti yaani Ibilisi”.
Na mtume Yohana anakubaliana na hilo pale anaposema katika Yoh 3:8 “… kwa kusudi hili mwana wa Mungu alidhihirishwa ili aziharibu kazi za shetani”
Ukuu wa kimungu alilonao Kristo na mamlaka zake juu ya mambo yote umetangazwa katika Wakolosai 1:16. ” kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana, ikiwa ni vitu vya enzi au usultani au enzi au mamlaka, vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.”
Haupo wito wowote kwa kanisa tena ili kuzidi kuharibu “mamlaka na uweza” kwa kuzifunga na kukemea roho za kimaeneo kana kwamba zenyewe zinayo haki ya kisheria juu ya nafsi. Yesu Kristo alizichukua dhambi za ulimwengu mzima na kwa hiyo yeye ni mwokozi wa wanadamu wote (1Tim 4:10) hata kama wanaamini na kupokea wakovu huo au hapana. Yeye amenunua msamaha na wokovu kwa ajili ya wanadamu kwa damu yake mwenyewe na kwa hiyo imeandikwa kwamba, “Mungu alikuwa ndani ya Kristo ……. asiwahesabie makosa yao…”. Kwa wale ambao wangeweza kuamini Injili na wakapatanishwa na Mungu, Mungu asingeweza tena kuyashikilia dhidi yao mambo yao maovu ya dhambi zilizopita (2 Kor 5:19) isipokuwa yeye huwaachia na kuwasamehe bure – pasipo malipo yoyote. Wale ambao wanaukataa na kuupinga wokovu wa bure wa Mungu na ambao wanaendelea kuzishikilia dhambi zao, watahesabiwa kuwa wanapaswa kuhukumu.
Lakini sasa haya mafundisho yao ya kisasa kwa kweli yanaifanya damu na dhabihu ya Bwana wetu Yesu Kristo pale msalabani ionekane kuwa haina maana. Mafundisho hayo yanamkataa yeye aliye wa kweli na mwenye mamlaka alizozinunua na kuzipata kama mwokozi wa wanadamu wote kupitia kumwagwa kwa damu yake. Kristo amekwishachukua msamaha wa wale wote watakaoamini. Lakini mafundisho haya ya kisasa yanatangua kazi ya msalaba kwa kuzihesabia roho za kimaeneo haki ya kisheria katika kuwaweka watu nje ya ufalme wa Mungu, kwa sababu ya kile wanachokiita wao kuwa ni “dhambi zisizoungamwa na kusamehewa za eneo la kijografia katika mkoa au jumuia.” Wao wanafundisha kuwa roho za uovu bado zina uwezo juu ya eneo lolote lile, ambalo mambo yaliyopita ya kijamii au mengineyo ya uovu uliotendeka. Imani za aina hii zinashikiliwa na kizazi kipya cha roho za wanadamu wa leo; na hapo ndipo imani ya aina hii inakotokea, kuliko kutokea katika Biblia. Wanasema kuwa maovu yaliyopita yanahitajika yapate “ondoleo” (toleo) lake, kwa wakristo kuungama na kuzitubia dhambi hizo, na kutumia damu ya Yesu, kabla roho za kimaeneo hazijaweza kufungwa! Kwa hiyo wanalundika kosa moja juu ya kosa jingine. Jambo hili limetazamwa ipasavyo ndani ya makala yangu ya kwanza.
Ikiwa tutafuata mafundisho hayo yao, tutagundua kwamba kila mtu katika ulimwengu huu sasa hawezi kusamehewa mara moja, wala kuokolewa na kukombolewa kutokana na nguvu za shetani kwa sababu ya msalaba. Hapana; ni kweli kwamba haiwi mara moja kwa haraka. Lakini Kristo akiwa amenunua wokovu huu wa bure na mkamilifu kutokana na dhambi, kuhukumiwa na uwezo wa shetani. Biblia inatangaza kwa nguvu sasa kuwa, “Injili ya Kristo ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye.” Rumi 1:16. Hivyo ndivyo maandiko yanavyofundisha; na kwa sababu ya wokovu hutujia pasipo haja ya kuzitambua na kuzifunga hizo zinazoitwa roho za kimaeneo – isipokuwa kama unataka kubatilisha matokeo ya damu ya Yesu pamoja na ushindi wake dhidi ya mamlaka na uwezo.
Hata hivyo ili kuonyesha kuwa sitii chumvi ule umaana wa jambo hili pale ninaposema kuwa mafundisho haya yanawakilisha mashambulizi juu ya Injili ya Yesu, hebu tutazame kwa makini yale ambayo kiongozi maarufu wa thiolojia hii mpya (George Ottis jr) anavyotangaza. Katika kutoa mhadhara wake kwa kusanyiko la YWAM huko Tacoma, Washingtone mnamo mwaka 1981, yeye pamoja na mambo mengine alisema kwamba:
“…Kristo hajatukomboa kwa kutupatia uzima wake kama fidia kwa ajili ya dhambi zetu, ili kwamba apate kutuachilia. Ikiwa tutazikubali asili au (chanzo) ambacho Kristo kikweli amenunua……wokovu wetu kwa damu yake …….. naye alimlipa Baba. Hivyo mtindo huu kabla ya yote unamwonyesha Mungu ambaye ni Baba kana kwamba yeye ni mwenye kulipiza mambo na ni mwenye kiu ya damu na kwa ujumla asiye patana na msamaha utolewao na Biblia.”
“Msamaha……. ni kiburudisho cha madai ya haki…….itakuwa ni vigumu kwa Mungu kuwa nayo kama mtunzi wa nyimbo anavyoiweka, “alilipa deni langu na akanisamehe dhambi zangu zote”
“Manukato ya toleo la Kristo yaliendelea katika utii wake kwa sheria za kimwili kwa niaba ya mwenye dhambi. Kristo katika maisha yake alitii sheria za mwili kwa ajili yetu na hayo ndiyo kwa uhalisi ni manukato ya toleo.”
Ijapo kuwa mwandishi huyo haelezei kwa uwazi sana kutokana na mpangilio huu, lakini bado hajayakana mawazo kama hayo, na wengine wanaamini kwamba yale aliyo yaandika tangu hapo pia yamejaa mawazo yenye kukaririwa. ( Kuyatambua mambo ya hapo juu, pamoja na taarifa nyinginezo juu ya mwandishi huyo aitwaye Ottis na mafundisho yake, hali kadhalika na mkanda wa video nilioutaja hapa kwenye makala hii angalia http://www.Bibleguide.com. Makala inayoitwa “George Ottis na mafundisho yake ya udanganyifu yaliyotayarishwa na Profesa J.S Malan – yote katika lugha ya Kiingereza.) Shirika lile ambalo linaongozwa na Ottis ndilo lililo husika na utayarishaji wa mkanda huo wa uongo wa video. Kwa sasa wameutayarisha mkanda wa pili wa video – ambao niliutaja mwanzoni – ambao unakusudia kuonyesha kwamba jumuia fulani fulani zimebadilishwa kupitia mafundisho haya ya roho za kimaeneo. Ottis pia anaheshimika kama mwanzilishi wa mawazo ya “ramani ya kiroho” ambayo nayo tutalitazama tutakapokuwa tukifikiria Ezekiel sura ya 4. Kama nilivyokwisha kusema, msingi wa kweli kuhusiana na maisha ya dhambi ya mwanadamu na hitaji lake la toba, pamoja na tabia na kusudi la kifo cha Yesu pale msalabani – inaonekana ilikuwa ni jambo lenye kutia giza (lisilo eleweka) kama si kupingwa kwa moja kwa moja na mafundisho haya ya kisasa! Ninatumaini kwamba unaweza ukajionea mwenyewe kutokana na maelezo ya hapo juu, kuwa hayawakilishi mambo mawili yote kwa pamoja, yaani ni mashambulizi juu yake na kuukana wokovu ambao Kristo amenunua kwa mapenzi ya damu yake. Ni kuyakana maisha ya dhambi ya mwanadamu ambayo ndiyo yanayomtenganisha na Mungu na pia ni kukana hitaji na tabia juu ya wokovu wetu wa ajabu kutokana na dhambi pamoja na milki yake.
Ni Injili Nyingine!
Hili sasa linatupeleka kwenye msingi wa pili wa makosa ya mafundisho haya, ambayo pengine ni ya hatari zaidi kuliko jambo lingine lolote lile kwa namna inavyodhalilisha na kushambulia moyo halisi wa Injili. Mafundisho hayo yanaonyesha kiini cha matatizo kisiwe ni dhambi, ugumu na kutokuamini kwa moyo wangu, bali uonekane kwamba ni majeshi ya uovu ya kiroho ndiyo yanayonizuia mimi kushindwa kumkubali Mungu. Wanasema kwa ujumla sio mimi mwenyewe wala sio hali ya moyo wangu ambayo ndiyo tatizo, isipokuwa ni roho chafu ndizo zinazonizuia nisimjue Mungu na kufungika katika giza. Chini ya mafundisho hayo, wenye dhambi sasa wamekuwa ni (wajinga) nao wamewekwa kuwa ni shabaha ya roho za uovu na kwamba inaelezwa kuwa, sio hali ya mioyo yao ambayo ndiyo tatizo, isipokuwa ni hizo roho za kimaeneo ambazo ndizo zinazowazuia wenye dhambi kushindwa kuitikia! Wazidi kudai kuwa kwa sasa haiwi tena ni dhambi za mtu binafsi kuwa ndiyo tatizo, isipokuwa sasa tatizo ni dhambi za jumuia, au miji, ambazo ndizo zinazohusika na roho hizi za kitaifa! Kwa sababu wao huyaamini mambo hayo, pia kuyafundisha kuwa njia kuu ya kuleta wokovu kwa watu sio kuihubiri Injili, isipokuwa ni kwanza kuzifunga roho za kimaeneo! Mahubiri ya Injili yanachukua nafasi ya pili na bado yanaweza tu kufanya kazi kwa ufanisi zaidi pale tu ambapo roho za uovu zitakuwa zimefungwa kwanza! Kwa hakika mafundisho ya jinsi hii yanawakilisha Injili nyingine – ni mashambulio kwenye ile sababu ya kimsingi na halisi juu ya kwa nini Yesu alikufa msalabani! Ni kukana mafundisho ya Yesu mwenyewe kuhusiana na mtu, kuhusiana na dhambi, kuhusiana na shetani, na kuhusiana na hukumu.
Mwandishi mmoja anatuambia kuhusu kiongozi mmoja maarufu wa kanisa huko Amerika ya kusini ambaye kwa kawaida huomba yeye mwenyewe kwa muda wa wiki moja kabla hajaanza kampeni zake. Anafanya hivyo ili aweze kuzitambua na kuzifunga mamlaka ya nguvu za giza juu ya mji huo ambao amekuja kuuhudumu. Mpaka “anapojisikia” kuwa amelipata lengo lake, ndipo anapoanza kuhutubia katika mikutano ya hadhara akiwaelezea watu kuwa “sasa” wako huru kumjia Kristo! Watu hawa wanajiinua wenyewe pamoja na mafundisho yao, wanajiinua juu zaidi ya Kristo pamoja na mitume ambao hawakuwahi kufanya madai ya jinsi hiyo kwa watu waliowajia. Kristo pamoja na mitume walikuja wakihubiri habari njema na wakiwasihi waume kwa wanawake watubu! Kwa maneno mengine, watu hao wanafundisha kuwa tatizo halisi sio ugumu wa moyo wangu mwenyewe wala sio dhambi, isipokuwa ni hizi roho za kimaeneo ambazo zinatakiwa kutambuliwa na kufungwa! Sio kupinga kwa moyo wangu kuwa ndilo tatizo, isipokuwa kupinga kuwa roho za kimaeneo ndicho kinachoniweka nje ya ufalme wa Mungu. Wanataka tuelewe kuwa ni roho za kimaeneo sasa ndizo zenye kuhusika na kiburi, tamaa mbaya na ugumu wa moyo wangu – kadhalika na kutokuamini kwangu?- na sio mimi mwenyewe. Mara tu mtu akizifunga roho za kimaeneo katika jamii basi, wenye dhambi wanakuwa wamewekwa “huru” kumjua Kristo! Mwinjilisti mwingine hawezi kuhubiri katika mji mpaka pale watakapojisikia kuwa wamezishinda katika maombi hizi roho za kimaeneo ambazo zinaushikilia mji huo kwa nguvu zao, na mmoja wa viongozi maarufu wa kanisa ambaye amehamasisha makosa hayo anatangaza kuwa: “ninafahamu vizuri pasipo shaka yoyote ndani yake, kuwa mahubiri makubwa hayawezi kuzisababisha roho za watu kuokoka na kanisa kukua … Hapana, isipokuwa ni pale utakapozishusha chini ( kuziangusha ) nguvu za giza zililzokuwa zinawazuia watu kumwishia Mungu katika maisha yao; hiyo ndiyo itakayosababisha kanisa kukua“. (Makala ya Larry Lea katika kitabu cha “Roho za Kimaeneo.” – Territorial Spirits” – Kilichoandikwa na Wagner, ukurasa wa 91 kilichokubaliwa na “Karisma na Maisha ya Kikristo” ã 1989, Strang Communication Company.)
Je watu hawa hawadhihaki kwa kumpinga Kristo mwenyewe? Mwandishi wa hapo juu anasema kuwa ana uhakika mkamilifu kwamba – hata mahubiri makubwa, hayawezi kuokoa roho za watu au kulijenga kanisa! Lakini tazama mwana wa Mungu aliwaambia wanafunzi wake, “Nendeni katika ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Yeye aaminiye na kubatizwa ataokoka”. Mk 16: 15,16. Mtume Paulo naye anaurudia usemi huo huo, “siionei haya Injili ya Kristo kwa sababu ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye.” Rumi 1:16. Pia katika 1Kor.1:17,18,21 kwa kuwa Kristo hakunituma ili kubatiza isipokuwa kuihubiri Injili … kwa sababu neno la msalaba …. ni nguvu ya Mungu iletayo wokovu …. Mungu alipenda kuwaokoa waaminio kwa upuzi wa lile neno linalohubiriwa”. Maandiko mengineyo mengi yangeweza kunukuliwa ili kuthibitisha tangazo lake Mungu litolewalo kwa ajili ya wokovu wa hao waliopotea na kulijenga kanisa lake, lakini sasa hawa waandishi wa kisasa wanapinga moja kwa moja ukweli huu kwa hiyo imani yao. Kristo hakuwaagiza wanafunzi wake, “kwenda kuzitambua na kuzifunga roho za kimaeneo ambazo zinawazuia watu washindwe kuokoka!”
Ijapokuwa waandishi hawa wanaamini kuwa kuhubiri Injili ni njia ya kuokoa roho za watu, bado wao huanza kwa kuzifunga roho za kimaeneo kana kwamba hilo ndiyo tendo la mwanzo na lenye msingi katika kanisa. Na kule kuihubiri Injili sasa hushika nafasi ya pili katika mipango yao – na bado Injili hiyo inategemea kikamilifu mtindo huo wao wa kuomba dhidi ya roho za kimaeneo. Hili ni tatizo kubwa la kasoro na ni sawa na kusema kuwa, “Sawa, ni kupitia Yesu kristo mtu anaweza kuokolewa, lakini unahitaji kutahiriwa kwanza”. Ukumbuke kuwa katika makanisa ya Galatia waliamini mambo mengi yaliyo mazuri na yenye haki kuhusu Kristo, na msamaha pamoja na wokovu ambao tunapata kwa yeye. Lakini wao waliongezea mafundisho yasiyo ya kiinjili, ambayo yalidhalilisha na kutishia uwepo wa imani yote! Mtume Paulo amesema “wamelogwa” kwa mafundisho ya aina hiyo. Na ijapokuwa wahubiri hawa wa kisasa ambao wanafundisha mapambano dhidi ya roho za kimaeneo, wanaweza pia wakaamini mambo mema na yenye haki vile vile, bila kujali kiasi gani wamejiingiza katika kujishughulisha na kazi “halisi” ya Mungu, hawajali kuwa mafundisho hayo yahusuyo roho za kimaeneo ni uchawi wenye hila ndani yake! Inayodhalilisha imani ya Injili.
Mafundisho haya hayaji kutoka kwa Yesu wala kutoka kwa mitume, au tusemeje sasa? Je Yesu alishindwa kuzitambua na kuzifunga roho zilizokuwa zinatawala Kapenaumu? Korazin na Bethsaida? Huko kulikuwa na mwitikio mdogo sana kufuatia mafundisho yake ijapokuwa amefanya kazi kwa nguvu kwao. Mat 11:20-24. Je tunaweza kulaumu upungufu wa mwitikio wa watu hawa katika miji hiyo kuwa unatokana na roho za kimaeneo, au kutokana na kushindwa kuyatambua majina ya roho hizo za kimaeneo? Au je, roho hizo za kimaeneo zilikuwa na mamlaka ya “kuzuia” huduma ya Yesu kwa sababu alikuwa bado hajafa pale msalabani (Kalvari)? Hapana! Hakuna lolote kati ya mawazo hayo ambalo lina ukweli wowote. Yesu alisema kwamba, ikiwa kazi alizozifanya katika miji hiyo zingefanyika huko Tarso na Sidon, wangekwisha kutubu siku nyingi iliyopita na hata Sodoma ingesalia hadi leo. Yesu anawakaripia watu wa miji hiyo ya Israel kwa sababu ya kukataa kwao kutubu. Anawakaripia kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kulingana na yote aliyoyasema na kuyafanya bado hawakuweza kuzioacha dhambi zao. Walikataa kumwamini na kumruhusu Yesu ayabadili maisha yao. Hiyo ilikuwa ni ugumu wa mioyo yao wenyewe na kutokuamini ndiyo iliyosababisha upungufu wa mwitikio, na ilikuwa ni kutokana na hilo ndio maana Yesu alitangaza hukumu kali juu yao. Walipaswa kujilaumu wao wenyewe na sio shetani wala sio roho za kimaeneo! Ikiwa tutafuata maelezo basi haya ndiyo mafundisho halisi ya maandiko ya neno la Mungu. Katika matendo ya mitume hatumsomi mtume Paulo akijifungia ndani mwenyewe kwa siku nyingi ili kujishughulisha na mapambano ya moja kwa moja na roho chafu, kabla hajahubiri katika mji – kana kwamba hiyo ilikuwa mbinu ya lazima! Hapana. Tunajua kuwa yeye alikuwa ni mtu wa maombi, lakini alipowasili katika miji na jiji, kwa kawaida anasema habari zake kwamba alikuwa akienda moja kwa moja kwenye masinagogi, au sehemu za masoko kumhubiri Yesu Kristo kwa watu. Na pale wayahudi walipoupinga ukweli wa Injili, Mtume Paulo analaumu juu ya mioyo yao. Mtd 13: 45,46.
Mtume Paulo alipokuwa huko Athene na alipoona mji mzima umekabidhiwa kwa masanamu kwa mara nyingine yeye hakujiingiza katika “ulimwengu wa kiroho” ili kuzifunga roho za ibada za masanamu. Hapana, bali yeye alienda katika masinagogi na sehemu za sokoni kumhubiri Kristo na ufufuo! Mtd 17:16-19. Sio wengi waliookolewa kule Athene. Na baada ya kuondoka hapo alielekea kwenye mji wa Korintho. Baadaye alipokuwa akiwaandikia Wakorintho, aliwaambia kuwa, alifika kwao baada ya kuondoka kule Athene akidhamiria asikijue kitu kingine chochote isipokuwa “Yesu Kristo aliyerubiwa”, 1Kor.2:2. Pengine kudhamiria huku kwake kuliweza kuimarishwa ndani yake alipoona uhafifu wa busara ya kibinadamu ambayo iliwashika watu wengi wa Athene, ambayo ndiyo iliyowafanya washindwe kuupokea ukweli wa Mungu. Hata kama hiyo ni kweli au hapana, Paulo mwenyewe analifafanua kwa ajili yetu, kwa nini iko hivyo kwamba watu hawapokei kweli ya injili.
“Kwa kuwa Wayahudi wanahitaji kuona ishara, Wayunani wanatafuta hekima, lakini tunamhubiri Kristo aliye sulubiwa, ambaye kwa wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuuzi.”
Anaendelea kueleza kuwa sio watu wengi wenye hekima na wenye nguvu walioitwa; 1Kor.1:22-29. Anafafanua hivyo kwa makini kuwa ni hekima za kibinadamu au tungeweza kusema ni kiburi ndicho kinachowazuia watu kuupokea ukweli wa Mungu – na sio roho za kimaeneo! Inashangaza kuona Biblia yenyewe inavyofafanua vizuri mambo yake. Wayahudi wanatafuta kuona aina fulani za ishara au miujiza na Wayunani wanatukuza hekima zao wenyewe – watu wenye vitabia vya jinsi hiyo hawako tayari kulipokea neno la Mungu kwa moyo wa unyenyekevu bali hujiinua wao wenyewe kinyume na kweli ya Mungu.
Katika mwangaza wa ukweli huu, sasa tunaweza kuona ni kwa nini watu wengi hawakuweza kuitikia kule Athene. Katika ule mstari wa 18 mtume Paulo anatangaza, “kwa kuwa mahubiri ya msalaba kwa wao waangamiao ni upumbavu bali kwetu sisi tuokolewao ni uweza wa Mungu.” Katika ile 2Kor 4:3,4 anapanua wazo hili kidogo; anasema Injili imefichwa kwao waliopotea, na anaendelea kuelezea “ambamo ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikra zao wasioamini isiwazukie nuru ya Injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.”
Katika sura hiyo anasimulia kwamba shetani anao uwanja wa matendo yake maovu kwa sababu ya kutokuamini au ugumu wa mioyo ya watu; ni ule ugumu wa mioyo ya watu wenyewe ambayo humpatia shetani fursa ya kuwadanganya na kuwafanya wawe mateka wa dhambi. Hapa mtume Paulo anaelezea hali ya kiroho ya hao wanaoipinga Injili; sura hii haiwakilishi mbinu kwa ajili ya “vita za kiroho”. Mtume Paulo hatuambii hapa kwamba tunapaswa kumfunga mungu wa ulimwengu huu kupitia maombi ya maombezi ili kwamba hao watu (wajinga?) waweze “kuwekwa huru” ili waweze kuamini Injili. Ijapo kuwa katika kukubaliana na hilo, maneno ya Yesu mwenyewe alipokuwa akiongelea kuhusu “saa yake” ambayo inamaanisha kifo chake pale msalabani. Katika Yoh 12:31 anasema: “Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”
Ukweli huu unarudiwa tena pale Yesu anapoongea kuhusu kuja kwa Roho Mtakatifu. Yesu anasema kwamba, Roho Mtakatifu atawahukumu wanadamu kwa hukumu kwa sababu “…yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa”, Yoh16:11. Bwana Yesu anaungana moja kwa moja na hukumu ya mfalme wa ulimwengu huu ambayo alikuwa anaenda kuitimiza pale Kalvari, pamoja na hukumu ya ulimwengu, ambayo ni hukumu ya ulimwengu huu ina maana kwamba ni ya watu waishio ndani yake. Akizichukua dhambi za ulimwengu pale msalabani Yesu angekinyang’anya kifo ule uwezo wake uliokuwa nao, (“uchungu wa mauti ni dhambi” 1Kor.15:56; Tim.1:10). Na atambatilisha yeye aliyekuwa na uwezo wa mauti, yaani huyo shetani, Heb. 2:14. Kila amwaminiye Yesu Kristo – kwake huyo mauti pamoja na shetani wamekwishapoteza haki yao na mamlaka juu yao. Kwa sababu mwanakondoo wa Mungu amezichukua dhambi zao – dhambi zao zote – na hivyo akanyang’anya toka kwa mauti na shetani ile haki yote waliyokuwa nayo juu yao. Zaidi ya hayo, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya wanadamu wote, anayo haki juu ya wote na kwa hiyo anawaagiza watu wote mahala pote kutubu (Mtd 17:30, tupo kule Athene Tena!). Tanga mwanzo mwa huduma yake na katika kuhubiri Injili, Kristo alikuwa akiwasihi watu kutubu, na mitume waliendeleza ujumbe huo huo Mk 1: 14-15; Mtd 2:38. Je, hawa waandishi wa kisasa wanasema kwamba wanaume na wanawake hawawezi kutubu mpaka kwanza roho zile za kienyeji katika taifa ziwe zimefungwa? Je hiyo ndiyo sababu iliyowafanya watu wa Kapenaum washindwe kutubu kwa sababu Kristo ameshindwa kuzifunga roho hizo juu ya Kapenaumu? Mafundisho haya hayaleti maana yoyote ile katika Agano Jipya! Yesu Kristo alizivunja mamlaka na uwezo pale msalabani kwa sababu alibakia pasipo dhambi, na bado akazibeba dhambi za ulimwengu wote na ufufuo wake ni muhuri kamili wa wokovu wetu, 1Kor.15:12–22. Akiwa amemnyang’anya shetani ule uwezo wake, Kristo sasa anaweza kupanua kwa neema ya Mungu ule uwezo wa uzima wake yeye mwenyewe akawapa hao wamwaminio. Akiwa amewasafisha kutokana na dhambi. Yesu pia anavunja ile milki ya dhambi katika maisha yetu kwa uwezo wa ufufuo wa uzima wake ndani yetu.
“Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo” kwa sababu shetani pamoja na uwezo wake wamehukumiwa na amezitangua pale msalabani. Kwa maneno mengine, huwezi kumlaumu shetani – hakuna popote inapohesabu hivyo! Sawa ni hakika kuwa shetani anawaweka watu katika giza, dhambi na vifungo – hiyo ina maana wale watu ambao hawaamini. Na yeye huja kunyang’anya, kuiba na kuharibu maisha ya watu. Lakini sasa, kwa sababu ya Kalvari huwezi tena kusema kuwa, njia ya kumwendea Yesu imefungwa kwa watu mpaka kwanza zile roho za kimaeneo zizuiazo ziwe zimefungwa! Jambo kama hili linabatilisha tu yale yote ambayo Kristo alilkuja kuyafilia. Hapana, wajibu unaangukia juu yako wewe na mimi kuiamini injili. Kama hatuamini Injili, basi kwa vyovyote vile tutakuwa tunampatia shetani pamoja na dhambi ile fursa na uwanja wa kufanya kazi ndani ya maisha yetu. Na katika hali yoyote ile bado shetani ni jeshi la uovu lenye nguvu katika ulimwengu, sawa sawa kama vile maandiko yanavyotangaza. Lakini maandiko yanatangaza kwa sauti na kwa ufasaha kwamba Yesu Kristo amezishinda dhambi, shetani pamoja na mauti, na akiwataka waume kwa wanawake watoroke wakawe huru kutokana na toleo la wokovu katika yeye ambalo linawakilishwa kupitia Injili.
Kwa sababu ya mambo haya pia, Yesu alisema kuwa na hii ndiyo kazi ya Mungu, “…. kwamba umwamini yeye aliyetumwa”, Yoh 6:29. Na kwa sababu gani roho mtakatifu atawahukumu wanadamu kwa dhambi? Yesu anasema kuwa ni kwa sababu, hawamwamini yeye. Yoh 6:9.
Na hii ndiyo dhambi ambayo wanaume na wanawake watahukumiwa kwayo. Dhambi zinginezo Yesu anaweza kutuweka huru kwa sababu kutokana na kile alicho kikamilisha pale Kalvari. Lakini njia pekee ya kuupokea wokovu huu ni kwa kumwamini yeye; na kama hatutamwamini yeye, basi tutakuwa tumepotea. Mtume Paulo anahitimisha kwa jinsi ya ajabu kwa ajili yetu pale katika Efeso 2:8. “kwa kuwa mliokolewa kwa neema katika imani na hii sio kwa uwezo wenu, bali ni kwa karama ya Mungu“. Na hawa Waefeso walikuwa ni watu wa aina gani? Haya, Mtume Paulo anatujulisha katika ule mstari wa 1-3 wa sura hii – kuwa walikuwa wafu kwa sababu ya makosa ya dhambi zao; waliishi kwa kuzifuata kawaida ya ulimwengu huu na mfalme wa uweza wa aga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi! Na wakawa kama wengine walivyo, watoto wa hasira. Kwa hiyo hapa tunawaona watu ambao wanatenda dhambi kisha wanajiridhia wenyewe, chini ya usimamizi wa shetani na vishawishi vyake kwa sababu ya kutokutii kwao; na kwa hiyo wapo chini ya hukumu ya Mungu. Na tunaambiwa wazi kwamba hiyo ndiyo hali ya wale wote ambao hawataki kuamini. Lakini mambo yalibadilikaje kwa hawa Waefeso? Haya mtu yule aitwaye Paulo, alitumiwa pia huko kwa Wamataifa ili apate “kuwafungua macho yao” na kuwarejesha kutoka katika nguvu za giza na kuwaingiza katika nuru; na kutoka katika nguvu za shetani waingie katika nguvu za Mungu, ili kwamba wapate kupokea msamaha wa dhambi, Mtd 26:18. Hii ilikuwa ni sehemu ya huduma ambayo Mungu ambaye aliyashinda mamlaka na uwezo kupitia Kristo pale Kalvari – alimpatia Paul. Mtume Paulo hakuhitaji kujitahidi au kupigana katika kupata huduma na mamlaka kwa kuzifunga roho za kimaeneo! Hapana, Paulo alikuwa kati ya Wayahudi kwa muda mrefu wa miezi mitatu kwanza kule Athene halafu akawa kwa wamataifa kwa muda wa miaka miwili, akiwa anazungumza, anajadiliana, akichunguza na kuhubiri – na watu wengi walimgeukia Bwana! Na hawa waefeso walipataje kuokolewa? Haya mtume Paulo anatuelezea katika ile sura ya kwanza mstari wa 13. Walimtegemea Kristo baada ya kusikia lile neno la kweli, injili ya wokovu wao! Ilikuwa ni kupitia Mtume Paulo aliyeihubiri Injili ya Kristo kwao na wao wakaiamini Injili, hilo ndilo lilliowasababishia kumgeukia Mungu wakiondokana na nguvu za shetani! Mungu asifiwe!
Kristo alipoenda kwenye nchi yake mwenyewe, Mk 6:1-6, hakuweza kufanya kazi zenye nguvu kwenye eneo hilo mbali ya uponyaji alioufanya kwa watu wachache. Je hii ni kwa sababu roho ya kieneo hiyo ilikuwa ni nguvu sana? Hapana! Biblia inatupatia sababu – inasema Yesu alishangazwa na kutokuamini kwao. Hakushangazwa na nguvu za baadhi ya roho za kimaeneo, isipokuwa yeye alishangazwa na ugumu wa mioyo yao na kutokuamini kwa watu hapo. Mty 13:58 anatuambia kwamba, ” … wala hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao“. Ni ile imani katika Kristo ndiyo iletayo wokovu na sio kule kuzifunga roho ya kitaifa; na imani inakuja kwa kusikia neno la Mungu – Rumi 10:17! Hivyo Yesu Kristo anatueleza katika Yohana 3:18,19:
“Amwaminiye yeye hahukumiwi, bali yeye asiyemwamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Bwana pekee ya Mungu. Na hii ndiyo hukumu, ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni na watu wakapenda giza kuliko nuru, kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.”
Sawasawa na mafundisho ya Yesu, watu wale ambao wanakataa wasimjie na kumwamini, wanafanya hivyo si kwa sababu wanazuiwa na roho za kimaeneo, bali kwa sababu walipenda matendo maovu yao. Mafundisho haya ya kisasa kwa ujumla yanasababisha kuchanganyikiwa na inaleta dhihaka kwa mafundisho ya biblia. Yanafanya maroho ya kimaeneo yaonekana ndiyo yanayohusika na uovu wa watu pamoja na kutokuamini. Wanataka tuelewe kuwa, iwapo tutafanikiwa kuzifunga hizi roho za kimaeneo ndipo watu watakuwa huru kuitikia Injili. Na hivyo makanisa yetu yataongezeka kwa kiwango kikubwa ambacho hujawahi kukiona kabla. Hii kimsingi inachafua mafundisho ya Kristo na ya Mitume. Hawa walimu wa kisasa wanasema kuwa ikiwa mji umeshikiliwa na matabia ya uchoyo, kiburi, ulevi na au tamaa mbaya basi hiyo ni roho ya kieneo ya uchoyo, kiburi, ulevi au tamaa mbaya ambayo inatawala juu ya mji huo na hiyo inahitajika kufungwa katika maombezi ya maombi. Hakuna lolote kama hilo ndani ya biblia. Eti nini? Kukemea roho za kimaeneo au tamaa mbaya na kisha watu wa mji huo wataachiliwa huru kutokana na dhambi hizo? Eti nini? Kwamba tatizo halisi sio mioyo ya watu bali ni uwezo wa roho za kimaeneo? Haya si mafundisho ya kibiblia. Biblia inatambua tatizo halisi kuwa ni moyo wa mwanadamu mwenyewe – au ndani ya moyo wa mwanadamu mwenyewe ndiko liliko tatizo. Tatizo sio kuwa tunatawaliwa na roho za kimaeneo za nje yetu – hapana – bali tatizo halisi ni dhambi iliyomo ndani ya moyo wangu mwenyewe na kule kujipenda. Tatizo halisi ni ugumu wa moyo wangu mimi mwenyewe. Hawa walimu wa kisasa wanafikiri kuwa iwapo utafunga “roho ya ulevi” katika eneo au jumuia ndipo nguvu ya kupendelea ulevi itavunjwa katika jumuia na kuwawezesha watu wote kuwa huru kutokana na ulevi. Huwezi kuifukuzilia mbali roho ya “ulevi” kutoka kwenye eneo kana kwamba hiyo ndiyo inayowashikilia watu katika dhambi hiyo! Watu hawa wanafikiri nini? Wanajaribu kulihamisha lengo la Injili lisieleweke kwa jamii; na lengo la Mungu kwa ulimwengu mzima pale wanapopotosha ukweli wa Injili. Wanajaribu kung’oa mwelekeo wa Mungu kwa wanadamu, kwa kuichepusha ile kweli. Lakini sasa unaweza ukaihubiri Injili kwa watu wote na ikiwa kwa neema ya Mungu watu binafsi wataitikia na kuokoka. Ndipo bila shaka utaweza kuona kupungua kukubwa kama sio kutoweka kabisa kwa ubaya wa aina fulani kama matokeo ya watu wakigeuka kutoka katika dhambi wakimgeukia Mungu! Mtd 19:19, 23-27. Huko Efeso watu wengi walichoma moto vitabu vyao vya uchawi na kuabudu sanamu ya Diana yalitoweka kimchezo tu – lakini hiyo ilitokea kama matokeo ya watu wengi kugeuka kutoka katika dhambi zao kupitia mahubiri ya mtume Paulo (mstari wa 26)! Katika Biblia nzima neno la Mungu huja moja kwa moja kwenye mioyo ya watu wa kuliona tatizo halisi pamoja na kupinga limelala hapo, yaani ndani ya mioyo ya watu. Tunaweza kutaja Yeremia 4:1-4 na Lk.13:34,35, pamoja ni mifano miwili kati ya mingi iliyomo katika Biblia.
Ijapokukwa watu wa Mungu walipaswa kumuombea, lakini hakuna chochote kile cha kuzifunga roho za kijiografia kana kwamba hizo zinawakilisha jeshi linalowaweka watu katika vifungo na kuwakataza wasimpokee Mungu.
Hii tena ni msingi mwingine wa kasoro za mafundisho haya ya kisasa – ni hatari izidiyo. Tatizo la wema na ubaya linaonekana kama ni jitihada kati ya mambo mawili ya ulimwengu mzima au nguvu za roho zinazopingana; na hazionekani kama zinahusika na chaguo ambalo mtu anaweza kulifanya kama yale yaliyoumbwa kwa mfano wa Mungu! Inaonekana kana kwamba wenye dhambi wenyewe sio tatizo halisi na hawafikiriwi kuwa wao wanabeba sehemu muhimu katika kuokoka kwao. Hapo inaonesha kwamba mapambano hayamo ndani yao au kwa ajili ya mioyo yao, bali ni sehemu fulani huko “angani”. Haionyeshi pia kuwa ni dhambi zangu binafsi na kule kutokuamini kwangu, hilo ndilo tatizo, bali inaonekana kama ninashikwa juu kwenye mashindano ya majeshi ya kiroho. Na mimi nipo pale katikati, karibu sawa na mlengwa mjinga. Ninahitaji tu nguvu za roho zilizo kubwa zaidi ili kuzidisha nguvu za roho ndogo ndogo kunifanya niwe huru! Ni huzuni ya jinsi gani hiyo; kuchanganya mafundisho kwa udanganyifu kwa jinsi gani huko? Injili ya Kristo ni uweza wa Mungu kwa kila aaminiye. Wokovu wa roho za watu hautegemei kule kuzishinda roho za kimaeneo! Lakini hawa walimu wa kisasa, sasa wamebuni Injili mpya ya ukombozi kupitia vita vya kiroho!
Kama nilivyokwisha kusema katika zile makala zangu mbili, na bado nazidi kukazia tena kuwa mafundisho hayo ni ya kimwili yanakazania kwenye mambo ya nje na siyo mambo ya kweli ya ndani. Wanamfananisha shetani kama anayetaka kuichukua nchi anayofikiri kuwa kama yake. Na wao wamesema kuwa hiyo ndiyo nchi ya kijiografia! Shetani ni mungu wa dunia hii maadam hii ndiyo mazingira ya kazi yake. Lakini kwa vyovyote vile viwavyo, iwe ni roho za kimalaika, mamlaka za uweza uwao wowote, bado maandiko yanaiweka wazi kwamba uwanja ambao ibilisi anapenda kuumiliki ni mioyo yetu, akili na nafsi zetu! Mapepo hawahamii kwenye “vumbi” kavu, bali wao wanapenda kupata makazi ndani ya binadamu Mty 12:43-45. Hawapati pumziko kwenye maeneo makavu, isipokuwa wanapenda kuishi ndani ya watu. Na hii ndiyo “nchi” ambayo Yesu aliifilia na akamwaga damu yake ili kutafuta nafasi ya kukaa yeye pamoja na Baba! Yoh 14:18-23. Tunatakiwa tuwe makazi ya Mungu kwa Roho, Efe 2: 22. Kwa kupitia kuiamini Injili ya Kristo sisi tumesamehewa na tumeingizwa ndani ya Ufalme wa Mungu kwa uzao mpya! Bali Shetani anataka kutufanya sisi tuwe ni makazi ya roho zake, sio kupitia nguvu za ziada za roho ya kitaifa, isipokuwa kwa kututaka sisi tuamini uongo wake ambao anaupendekeza kwetu kwa kutujaribu ili tusimwamini Mungu na kisha tujipendeze wenyewe. Huo ndio uwanja wa mapambano. Na katika huo uwanja wa mapambano mioyo yetu pamoja na dhamira zetu, Mungu alionyesha pendo lake mwenyewe kwetu sisi kwa kumtuma mwanae pekee afe kwa ajili yetu na kututaka tugeuke mbali na matendo maovu na tuupokee wokovu wake wa bure. Hiki ni kipawa cha Mungu!
Lakini madanganyo ya mafundisho hayo yanazidi kutumbukia ndani zaidi. Baada ya kuwa wameamini kuwa wamekwisha kuzifunga roho za kimaeneo zitawalazo juu ya mji, wengine wao wanawachagua “walinzi wa milangoni.” Eti hao ni watu ambao wanapaswa kuomba ili kuzuia roho za uovu zisiweze kuingia katika miji – hatimaye, watu hao watasimama pia kwa mbinu fulani ndani na karibu na mji – kwenye barabara kuu ndani na nje ya mji na kuendelea! Kwa kufanya hivyo, wanazihesabia roho za mikoa yaani wanazipatia uwezo wa kutawala jumuia yote kana kwamba watu hawana chaguo lao katika mambo – na kwa kiasi kwamba Injili ya Kristo haiwezi kuwafikia kwa ufasaha na kuwaokoa! Hivyo siyo Injili ya Kristo – wanacheza michezo ya ulozi pasipo kutambua! Kwa hivyo, wao kwa vyovyote wanaamini kwamba ikiwa utaweza kuzifunga roho hizo, basi roho ya Mungu itatawala juu ya mkoa, basi hapo sasa watu wapo huru kuitikia Injili na kisha Wakristo wanaweza kuanzisha utawala wa Mungu katika taratibu za jamii ya kienyeji – kwenye mifumo mbali mbali ya serikali na jamii katika mji! Hii inaonekana kama uanzishaji wa ufalme wa Mungu hapa dunianli na “kurejesha” nchi kutoka katika mikono ya shetani. Hawa waombezi wapya wanachokifanya hapo wanapigana ili kupata ardhi, vumbi na dunia ambayo ndiyo wanayoisemea kuwa inapaswa kurejeshwa kutoka katika mikono ya shetani. Baadhi ya hao waandishi wanayo mafundisho mengine yanaweka kwa urahisi yanaeleza kwamba, kwa sababu ya dhambi zake katika bustani ya Adeni – Adamu alipoteza milki ya mipaka ya nchi kwa shetani kwa kufanya hivyo, wanazipatia haki roho za mikoa yaani wanazipatia uwezo kutawala sio tu nchi bali pamoja na watu wanaoishi katika nchi hiyo. Wanasema kuwa Yesu alikufa pale msalabani ili kurejesha milki juu ya vumbi hili na dunia – pamoja na mipaka ya kijiografia. Lakini tunaelezwa zaidi na hawa waandishi wa kisasa kwamba, pale msalabani hapakuharibu mamlaka zote pamoja na uweza wake. Hapana, tunatakiwa kutumia uwezo ambao Bwana ametupatia sasa, ili kuzifunga roho hizi chafu zitawalazo juu ya mkoa na kisha watu wa mkoa ule watakuwa huru kuupokea utawala wa Mungu! Hiyo ni injili yao ya kimwili. Kulingana na mafundisho hayo, pambano la msingi sio kwa ajili ya nafsi za watu (wauume kwa wake) isipokuwa ni mavumbi – yaani, sehemu ya kiografia! Na mara tu tunapokuwa tumezifunga roho hizo zinazotawala juu ya kipande hicho cha vumbi na ardhi, kwa watu wanaotembea au kuishi juu ya kipande hicho cha vumbi au ardhi, watakuwa huru kuipokea Injili na kuingia katika ufalme wa Mungu. Mafundisho haya ya kimwili yote yanawafunika macho watu wasiijue kweli ya maandiko, ihusuyo asili ya dhambi, wokovu na ufalme wa Mungu.
Hebu niseme hapa, kwamba, ninafikiri sote tunajua kwamba eneo fulani fulani au jumuia inaweza ikaingiwa na tabia fulani ya dhambi maalumu inayoonekana kumiliki eneo hilo. Na kwa vyovyote vile, mtu yeyote anayezaliwa katika mazingira ya aina hii, anaweza akashawishika. Na desturi hii ya dhambi katika jumuia, na desturi hii ya dhambi bila mashaka yoyote yale, inakuzwa na Ibilisi na anaweza kuwatumia kuchanganya upinzani wa Injili ndani ya wale wasioamini, Mtd.19:23-28. Lakini hali hii ndivyo haswa iliovyokuwa katika jumuia nyingi na miji ambayo mtume Paulo alitembmelea. Kulikuwepo na zinaa inayoendelea katika miji mingi. Dini za Ulozi na Uchawi zilishikilia jumuia fulani fulani. Kulikuwepo na uchoyo, kiburi, na uchafu. Koritho ilikuwa ni sehemu iliyozoelea mambo ya aina hiyo. Lakini sasa kupambana na roho za kimaeneo ili kuwaweka huru watu kutokana na tabia zao za uzinzi, mambo ya kimwili au uchawi, jambo hili hamna msingi wowote ule wa Kibiblia.
Kwa hakika, mtume Paulo anachagua maneno kwa makini pale anapoyaulizia makanisa ya kule Galatia – “Ni nani aliyewaloga? Mafundisho hayo yanafanana kama ulozi na kadiri mtu anavyoendelea kujifunza mafundisho haya ya kisasa ndivyo mtu anavyoona kwa urahisi kuwa yanafanana na kile ambacho mtu anaweza akafikiria kuwa ni mafundisho na mtindo wa ulozi au wa Uaguzi. Kadiri mafundisho haya yanavyozidi kuenea ulimwenguni kote, bila shaka yanaweza kutengeneza vijitabia vyake kutoka nchi fulani hadi nyingine kadiri watu walivyo na shauku ya mambo mapya; na katika njia tofauti. Kwa mfano; yapo magazeti ambayo yanawahamasisha na kuwasihi wakristo wote kuomba dhidi ya roho za kimaeneo juu ya baadhi ya miji na jiji fulani; magazeti hayo yanajishughulisha sana katika kutafutia aina fulani ya dhambi nyingi hasa Uchawi, ambao umefanywa katika nchi. Na kisha huyatangaza matokeo waliyoyapata ili kwamba wakristo waweze kuomba maalumu dhidi ya roho hizi za kimaeneo, ambazo zinafikiriwa kuhusika na matatizo ya dhambi hizi zote. Hata pia wanawasihi wakristo watembelee maeneo fulani fulani ya kijiografia katika jiji huku wakikemea roho chafu. Lakini vitabu vinavyoongoza ambavyo vimeandikwa kuhusu somo hili kwa ujumla haviwahamasishi wakristo kuingia katika “vita vya kiroho” dhidi ya roho za kimaeneo. Kinyume chake, wanaonya juu ya hayo na watuambia kuwa ni wakristo wale waliokomaa, “na wenye karama rasmi” na wale walioitwa ndio wanaopaswa kuingia katika mapambano hayo. Ijapokuwa bado wanasema kwamba vita hivyo ni vya lazima kwa ajili ya kuleta mafanikio ya uenezaji wa Injili. Zaidi ya hayo bado wanakubali kuwa jambo hili ni kujitumbukiza katika matatizo ya bure na yenye kuogofya na ni mapambano ya hatari yenye kuwapatia wengi misiba. Hayo yote ni sawa na kubatizwa katika mambo ya ushirikina na udanganyifu.
Vita vya Kiroho – ni Matendo yenye Hatari?
Lakini sasa kwa nini “vita hivyo” viwe ni mambo “yenye hatari”, kuogofya na kukuletea matatizo? Haya, wanasema kwamba wakristo “wa kawaida” huwa hawana mamlaka na nguvu zilizo katika kiwango cha “madaraka ya juu” ya roho za kimaeneo. Na wanazidi kutuambia kuwa kumewahi kutokea na itaendelea kuleta msiba katika “vita” hivyo! Waandishi hawa wanatuambia juu ya wachungaji ambao wameanguka katika dhambi “kwa sababu” ya kujiingiza kaika “mbinu ya kiwango cha mapambano ya kiroho” (strategic – level spiritual walfare)! Waandishi hawa wanatuelezea kuhusiana na kuvunjika kwa ndoa, magonjwa, mambo ya kimwili, watu wanajifanyia uvunjifu juu ya Imani zao na hata juu ya kifo – kwa sababu ya kujihusisha kwao katika aina hii ya vita! (Ikiwa ni kweli kuwa matatizo hayo yamewazukia kwa sababu ya watu wenyewe kujihusisha katika aina hii ya mapambano, basi litakuwa ni swali lingine lenye kuhojiana). Kumekuwepo na michanganyiko mingi pamoja na maumivu ya moyo kutokana na mafundisho haya kiasi kwamba kiongozi wa aina fulani ya huduma huko Amerika ameandika kitabu kuhusiana na jambo hili kiitwacho (Needless Casualties of War”; “Misiba isiyo ya Lazima katika Vita”, kilichoandikwa na John Paulo Jackson, Kingsway Publications. Copyright John Paul Jackson 1999). Yeye pia anapendelea mapambano dhidi ya maroho, lakini katika kitabu chake anaeleza jambo fulani zuri na anaonya kuhusu kutokuwa na kiasi, ambako analaumu kuwa ndiko kunako husika na majanga ya kutisha katika maisha ya wakristo. Lakini sasa kule kuamini kwao juu ya imani ya kufunga roho za kimaeneo, kinawafanya waandishi hawa wote wawe vipofu juu ya ukweli uliofunuliwa katika maandiko, nao huuacha ukweli huo kirahisi tu na hawaonyeshi kuhusika kihalisi kwa yale yanayofundishwa na Biblia ili wahalalishe makosa yao. Wanaeneza mafundisho yenye kasoro, na watu wengi wanayafuata mafundisho hayo na mara zote hutumbukia katika matatizo ya kutisha. Kwa hiyo waandishi hawa wanabuni kasoro ili waweze kuzielezea ni kwa nini misiba hiyo! Kwa hiyo, hata mwandishi niliyemtaja hapo juu, anaelezea kwamba “kwa kawaida” wakristo huwa ndani ya Kristo Yesu, Kolosai 3: 3, lakini kama tutajihusisha katika aina yoyote ile ya mapambano ya kiroho, basi hapo tutakuwa tumejiweka wazi kama shabaha kwa nguvu za mapepo na tunaweza kudhuriwa na kuharibiwa na mapepo yale!
Anasema kwamba hata kule kuomba tu kwa Mungu kuhusiana na nguvu za mapepo ni mtindo wa mapambano ya kiroho! Inafanana kama mbwa mwitu kuweka kichwa chake nje ya tundu lake la usalama, hiyo inamfanya aonekane ni chambo cha mnyang’anyi anayezurura! Hii ni aina fulani ya udanganyifu ambao unaenezwa na hawa waandishi. Hayo ni mashambulizi juu ya mafunuo ya mandiko kuhusiana usalama wetu na wokovu katika Kristo! Eti mimi? “Kwa kawaida” tupo ndani ya Kristo, isipokuwa tunapojishughulisha na mapambano ya kiroho “hatuwi tena ndani ya Kristo” au “hatuwi kabisa ndani ya Kristo”, isipokuwa tunakuwa tu “sehemu ndani yake?” Eti mimi? Na kwamba eti tunaweza tukawa ni “shabaha” ya roho chafu anayeweza kusababisha uvunjifu wa ndoa, maradhi na kifo ikiwa tutakuwa si waangalifu?! Hii si kitu kingine isipokuwa ni ubatizo katika mambo ya ushirikina na mafundisho ya ulozi. Agano jipya linafundisha kinyume cha hayo yote; yaani inafundisha kuwa ni kwa njia ya kuenenda katika silaha zote za Mungu tu na kupigana vita vizuri vya imani, hapo tunakaa kwa Usalama kutokana na michezo yenye maumivu ya shetani – hivi ni vita vya kweli vya kiroho na vinapaswa kuhusika na mwenendo wetu kiroho – na wala sio katika kupambana dhidi ya roho za uovu katika maombi kama tutakavyoona baadaye katika Efs.6:10 –18.
Maandiko hayafundishi wala kuhamasisha udanganyifu huu; wala hawawezi kuingiza aina hii ya woga ndani ya moyo yetu. Tunaambiwa kuwa “yeye aliye ndani yetu ni mkuu kuliko yeye aliye ulimwenguni” na kwamba “hakuna kitu kinachoweza kututenga na upendo wa Mungu uliomo katika Kristo Yesu.” Na hii Inajumlisha mamlaka zote na uwezo! Tumeketi pamoja katika Kristo Yesu mbinguni na Uhai wetu umefichwa katika Kristo ndani yake Mungu” – mambo mengi ni yenye kutia moyo na ahadi zake Mungu akituthibitishia Usalama na baraka zaidi ya kingine chochote kile pale tunapotunza neno lake na kumwamini yeye. Hatusomi chochote kihusucho kushambuliwa na maroho machafu au maisha yetu kuharibiwa kwa sababu tu, tunaomba kama maandiko yanavyo tushauri kuomba. Biblia haikiri aina yoyote ile ya misiba kati ya wale wanaoomba. Au je! Unaweza kupata mausia yoyote ya maombi katika Biblia yanatuonya juu ya uwezekano wowote ule wa misiba. Au Biblia inaelezaea kukumbukia wapi ili kuonyesha kikundi maalum na teule cha Kikristo, ambacho wao pekee waliitwa kwenye vita maalum kwa sababu tu kwamba mapambano hayo ni yenye hatari sana kwa wakristo wa kawaida kuyashiriki?! Hivyo ndivyo wao wanavyofundisha, lakini hii pasipo ugumu wowote ni kuwatumbukiza watu ndani ya nyumba ya matope ya ushirikina na makosa.
Mausia yote ya kuomba katika Agano jipya, ni kwa waamini wote na hakuna hata mausia yanayohusu maonyo kwamba inawezekana ikawa ni “hatari” kuomba, na kwamba aina fulani ya maombi inapaswa kushirikisha aina fulani tu ya waamini wenye wito maalum!
Lakini hii karama maalum ni kitu gani ambacho hawa waombezi wanamaanisha kuwa nazo kulingana na mafundisho hayo? Tunaelezwa kuwa wanapaswa kuwa ni wakristo walio komaa na haswa wawe na karama ya kutambua majina na tabia ya roho za kimaeneo na uwezo wa kusikia toka kwa Mungu, ambaye huwasiliana nao ili kujua ni aina gani ya roho inaweza na inahitajika kufungwa. Karama hizi zinafikiriwa kuwa ni za lazima katika vita vya kiroho. Kwa hiyo waombezi hao wanaweza kutumia masiku na mawiki katika maombi wakiwa na shabaha ya kutambua jina au aina ya roho za kimaeneo zinazotawala juu ya jiji na wanasubiri toka kwa Mungu ili kuwaonyesha ni aina gani ya roho inayostahili kukabiliwa katika maombi yao. Wengine wao wanashuhudia kuwa wanajisikia kuwa wanaingia katika milki nyingine ambako wanakabiliana na roho chafu. Wakati mwingine eti wanaweza kuziona hizi roho chafu labda kama katika maono, au dhahiri. Yanaweza kujitokeza kama kiumbe cha kutisha, nasi tunaambiwa kuwa “mivutano” inaweza wakati mwingine ikawa kwa nguvu. Mchungaji mmoja alivutana ili kutia changamoto roho ya kieneo kuhusu mitaa mingapi katika mji inapaswa kuachiliwa. (Inaonekana kuwa mitaa hiyo ambayo huyo roho mchafu aliiachilia kwa washujaa wa maombi, basi watu katika eneo hilo wangeweza kuitikia Injili, lakini kwa bahati mbaya mitaa ambayo roho mchafu hakuiachilia kwa washujaa wa maombi, watu waliopo pale hawakuweza kuokoka! Au tufikirije?!). Baada ya kufungwa kwa roho za kimaeneo (kama wanavyofikiri), mhubiri huyo anaita mikutano ya Injili akiwaambia watu, eti sasa wamewekwa huru waitikie Injili!

Post a Comment

0 Comments