MFALME ALIYEKUWA NA MBWA WAKALI KUMI
MFALME ALIYEKUWA NA MBWA WAKALI KUMI Kulikuwa na mfalme mmoja aliyekuwa na mbwa kumi wakali sana. Alipenda kuwatumia mbwa hawa pindi akitaka kumuadhibu mtumwa aliyekosea. Mbwa hawa waliwatesa watumwa kwa kuwararua na meno yao makali! Wakati mwingine watumwa waliokutana na adhabu hii walipoteza uhai. Siku mtumwa aliyemtumikia mfalme kwa miaka kumi alitoa wazo baya ambalo halikumpendeza mfalme, ikaamriwa akamatwe na kutupwa katika banda la mbwa. Mtumwa alinung'unika na kusema :"nimekutumikia kwa miaka 10, na leo wanitenda hivi? Naomba unipe walau siku 10 kabla hujanitupa baniani! " Mfalme akakubali. Katika siku izo 10, mtumwa alimfuata mlinzi wa banda la mbwa na kumuomba ampe nafasi kuwahudumia mbwa wale. Mlinzi alistaajabu ila akakubali. Mara moja mtumwa akaanza kazi ya kuwapa mbwa chakula, kuwaogesha na kila aina ya faraja ambazo wanyama huhitaji. Siku 10 zikaisha, mfalme akaamuru mtumwa atupwe bandani kutumikia adhabu yake. Hilo likafanyika kwa hara...