Posts

Showing posts from March, 2017

MAOMBI MAKALI YAKUOMBA NA KUFUNGULIWA.

*MUNGU akukumbuke. BWANA akutendee muujiza mkuu. MUNGU ayakumbuke machozi yako. Kwa jina la YESU KRISTO umeshinda. BWANA YESU alisema kwamba kila tutakalolifunga duniani na mbinguni limefungwa Mathayo 18:18. Hivyo tunawafunga wachawi wanaokusumbua na watakimbia wenyewe. Kwa jina la YESU KRISTO. umeshindaaaaaaaaa kwa jina la YESU KRISTO. *Nakuombea Masikio yako yafunguke, kifungo cha ulimi wako kilegee uisemee haki yako. Mwili, nafsi na roho yako vifunguliwe na kila aina ya vifungo vya mawazo, maneno na matendo kwa jina na damu ya YESU KRISTO na kwa neno la MUNGU kama lilivyoandikwa katika Marko 7:34-35 '' YESU akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka.Mara masikio yake yakafunguka, kifungo cha ulimi wake kikalegea, akasema vizuri.''Mungu akubariki. * Jiwe lililokuwa kizuizi cha kumzuia BWANA kutoka kaburini, liliondolewa na malaika. Na leo wapo watu wengi leo mawe yamewakalia katika maisha yao, kuna mawe yamekalia bi...

mafundisho yenye makosa, yanayowaongoza watu katika uzoefu udanganyao.

Hatari za Mafundisho ya Kisasa – mafundisho yenye makosa, yanayowaongoza watu katika uzoefu udanganyao. Wanasema kuwa aina hii ya “mapambano ya kiroho” ni muhimu kwa ajili ya mafanikio ya Injili. Pasipo shaka yoyote huo ni udanganyifu. Lakini tena wanatuambia kuwa kutakuwa na “majeruhi” miongoni mwa Wakristo, kwa sababu Wakristo wengi “hawana silaha zifaazo” kwa ajili ya aina hii ya mapambano au hawajafahamu “jinsi ya kupigana” aina hii ya vita! Lakini wazo la kuwa mtu anajishughulisha na vita vya kweli vya kiroho inaweza kumletea matokeo ya roho chafu kukushambulia na kuharibu maisha ya familia yake ni mafundisho yasiyo na maana na yasiyo ya Kibiblia. Hii ni zaidi ya aina fulani ya mafundisho ya ulozi ambayo yanaweza tu kuwaletea watu hofu katika mioyo yao. Hata kama chanzo cha majanga ambayo tunaelewa yanawaangukia wakristo, yanaweza kuwa ni kutokana na kujihusisha kwao na aina hii ya vita vya kiroho ambavyo sio vya Kibiblia, hii ni hoja ya kuijadili kama nilivyokwisha sema...

SIRI YA MAFANIKIO

‘Siri ya Mafanikio’ Maana ya ‘motivational speaker’ ni msemaji ambaye anawatia moyo watu na kuwahamasisha wafikie malengo au makusudi yao kupitia kubadilisha mtazamo wao. Wanawachochea watu watengeneze malengo (goli) kwa ajili ya maisha yao ya baadaye. Wanafundisha sana juu ya ‘mafanikio’ na wanadai kuwasaidia watu kuboresha na kufanikiwa katika maisha yao. Usemi au fikra ‘motivational speaker’ inatoka wapi? Inatokana na nia na roho ya kizazi hiki ambao hawamjui Mungu. Nyendo au mafundisho haya yalianza miongoni kwa wasioamini hasa kama miaka 60 iliyopita. Msingi wa mafundisho haya ni ifuatayo: huhitaji mtu mwingine; huhitaji Mungu au dini; wewe mwenyewe kama binadamu tayari unao uwezo ndani yako kubadilisha maisha yako na kutimiza ndoto zako zote na kutekeleza malengo yako yote! Wasemaji hao wanaahidi watu watafanikiwa katika kila eneo la maisha yao – INATEGEMEA NA MTAZAMO NA FIKRA ZAO TU! Ni lazima kubadilisha mtazamo wako tu! Kama ukibadilisha mtazamo wako na fikra zako, ...