Hatari za
Mafundisho ya Kisasa – mafundisho yenye makosa, yanayowaongoza watu katika
uzoefu udanganyao.
Wanasema kuwa
aina hii ya “mapambano ya kiroho” ni muhimu kwa ajili ya mafanikio ya Injili. Pasipo shaka yoyote huo ni
udanganyifu. Lakini tena wanatuambia kuwa kutakuwa na “majeruhi” miongoni mwa
Wakristo, kwa sababu Wakristo wengi “hawana silaha zifaazo” kwa ajili ya aina
hii ya mapambano au hawajafahamu “jinsi ya kupigana” aina hii ya vita! Lakini
wazo la kuwa mtu anajishughulisha na vita vya kweli vya kiroho inaweza kumletea
matokeo ya roho chafu kukushambulia na kuharibu maisha ya familia yake ni
mafundisho yasiyo na maana na yasiyo ya Kibiblia. Hii ni zaidi ya aina fulani
ya mafundisho ya ulozi ambayo yanaweza tu kuwaletea watu hofu katika mioyo yao.
Hata kama chanzo cha majanga ambayo tunaelewa yanawaangukia wakristo, yanaweza
kuwa ni kutokana na kujihusisha kwao na aina hii ya vita vya kiroho ambavyo sio
vya Kibiblia, hii ni hoja ya kuijadili kama nilivyokwisha sema. Na sasa
ningependa kufanya mambo mawili ya muhimu.
Kwanza, kwa
vyovyote vile aina zote za matatizo hutokea katika maisha yetu ikiwa tutakuwa
hatuishi kulingana na neno la Mungu. Katika Efeso 4:11-14, Mtume Paulo anaongea
kuhusu huduma zitolewazo na Mungu kwa kanisa ili kwamba wote tupate kupokea
kukua katika Kristo. Tunapaswa kukua na kuwa wenye nguvu katika ufahamu wa
Kristo na tusibaki kama watoto wadogo au kama watu wa mwilini ambao huchukuliwa
na kila aina ya upepo wa imani wakitazamia “jambo jipya” linalofuata – ili
kutushitusha sisi na hivyo kutufanya shabaha ya hila na udanganyifu wa
wanadamu.
Kumewahi kutokea
uzao mwingi wenye hatari ya “upepo wa imani” au makosa yenye hatari kwa kadiri
ya miaka mingi sasa. Makosa haya yawezekana yanaanzia au yanapata msaada wenye
nguvu kutoka kwa waamini wa Amerika. Mafundisho hayo hayana msingi wowote wa
neno la Mungu isipokuwa ni matokeo ya kufikiri kwa watu wenyewe na mafunuo ya
pekee. Hali kadhalika na uzoefu wao binafsi ambao hauna ulinganifu wa kweli wa
kimaandiko. Imani hizo zinahamasishwa na baadhi ya majina yanayo julikana vema,
wengi wao ni viongozi wa mashirika yenye nafasi nzuri ya fedha nyingi ambazo
ndizo zinazo wasaidia sana kusambaza ujumbe wao. Mengine hupeperushwa na upepo
huu wa imani, pasipo hata kufikiria yale ambayo Biblia inasema au kufundisha.
Na mradi wanakataa kuongozwa na neno la Mungu, haishangazi kwa hiyo kuona
kwamba matendo yao pia huwa ni ya kimwili, Rumi 1:21-24. Ikiwa tutajiondoa
kutoka kwenye neno la Mungu ndipo tutakuwa tunajiondoa pia kutoka katika maisha
matakatifu yaliyo takasika. Yesu alisema, “watakase kwa kweli.” Yoh 17:17.
Maisha ya watu hayajajengwa juu ya mwamba wa Yesu Kristo; juu ya mwamba wa
kulitii neno la Mungu. Kwa hiyo si jambo kubwa la kushangaza kuona watu wengi
wakipitia katika maisha ya taabu – katika nyakati hizi kunaonekana kuenea
kwingi kwa watu kuondoka kutoka katika neno la Mungu ambavyo inaleta matokeo
katika hali ya maisha kuwa ni ya kimwili na yasiyo imara kwa wakristo,
ikiwafanya watu kuanguka katika aina fulani ya dhambi na shida na kuchomana wao
kwa wao na kupitia kwenye huzuni nyingi. Katika mtiririko wa habari hii ni
rahisi kwa waandishi hawa kusema kuwa watu wanapambana na matatizo katika
maisha yao “kwa sababu” ya kujihusisha kwao katika aina hii ya vita vya kiroho,
kwa sababu wapo wengi wenye matatizo tayari, lakini chanzo halisi cha matatizo
yao kwa hakika yaweza ikawa ipo sehemu fulani.
Watu hawa
hawaingii katika mapambano ya kiroho kabisa, bali wanaingia kwenye ulimwengu wa
maroho unaotofautiana kabisa – pale wanapokuwa katika kudanganywa na kutokana
na hilo huwajia “Injili nyingine”, “Yesu mwingine” na “roho mwingine”. Wanazitengeneza
nguvu za “maroho ya kibinadamu” na kufanyika kuwa ni shabaha ya maroho
yadanganyayo, ambayo ndiyo yanayowashawishi kuona kuwa wanajishughulisha na
vita vya kiroho na kwamba watu wengi wanaendelea kudanganywa kunyang’anywa
ufahamu wa kweli wa Mungu ambao umo ndani ya Kristo. Ndiyo naweza kuhisia
kwamba mtu yeyote anayeifuata elimu ya mtindo huu na kuamini huku katika uzoefu
unaofanana, lazima watajitumbukiza katika matatizo makubwa. Wanalivunja neno la
Mungu, na wanalivunja ndani ya milki isiyo halali.
Inaweza
ikatusaidia tukitazama katika 2Kor.11:1-15 ili kutusaidia kuelewa jinsi gani
mambo haya yanavyoweza kuwa. (Tafadhali angalia katika makala ya kwanza ambamo
hali ya kanisa la wakorintho pamoja na misingi ya udanganyifu wao
ilivyoangaliwa). Katika kanisa la Korintho wengi wa watu wa Mungu huko walikuwa
wanaenenda kimwili. Walipenda kupata “uwezo na utukufu”. Na hiyo hali ya
kimwili pamoja na hayo matamanio ya kimwili ya kupata uwezo na vyeo ili
wasababishia kupotelea mbali na mafundisho ya Kristo. Kung’ang’ania
kudumu katika mwenendo na tabia hizo kuliwaletea kuonekana wazi na kuwafanya
wawe ni kafara ya udanganyifu wa shetani – ni udanganyifu wa kutisha! Tunaambiwa
kuwa shetani mwenyewe hujigeuza katika sura ya “malaika wa nuru”, ule mstari
wa 14. Ninaamini kwamba baadhi ya uzoefu wa watu hawa unapaswa ueleweke katika
habari hii. Katika mstari wa 13 anaongea kuhusu “mitume wa uongo, wafanyakazi
wenye hila, wakijibadilisha wenyewe kuwa mitume wa Kristo”. Katika mstari ule
wa 4 anatueleza kwamba hata watu wa Mungu wanaweza kuongozwa na udanganyifu huu
katika kumpokea Kristo “mwingine”, roho “mwingine” na Injili “nyingine”.
Hatujaelezwa, kuwa mambo yanaweza kuwaje, lakini yanaweza kutokea iwapo mtu
analiacha neno la Mungu, hilo limewekwa wazi sana kwetu. Na iwapo hilo liliweza
kuwatokea wale ambao mtume Paulo mwenyewe aliwashuhudia na kuokoka ambao pia
walikuwa katika hesabu ya kuongozwa na kuangaliwa kwa karibu na mafundisho
yake; hivyo tusifikiri kuwa mambo haya basi hayawezekaniki nyakati za leo! Na
hiyo ndiyo sababu inayoelekea kuandikwa kwa makala hii, kwa sababu mafundisho
hata ya kisasa yanatuletea hila za shetani ili kuzichafua fikira za watakatifu
kutokana na unyofu uliomo katika kristo – msitari wa 3. Katika Yeremia 5:30,31,
tunakuta kufanana kunako shangaza juu ya yale anayoyasema mtume Paulo kwenye 2
Kor.11:13-20. Manabii wa uongo wakiwadanganya watu wa Mungu, viongozi wao
wakiwatawala kwa nguvu, na bado watu wa Mungu wakiyapenda hayo yote! Mungu
anaisema juu manabii kwenye Yeremia 14:14, “ndipo Bwana akaniambia, hao manabii
wanatabiri uongo kwa jina langu mimi, mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru ,
wala sikusema nao; wanawapeni unabii wa maono ya uongo na uaguzi na neno la
ubatili na hadaa ya mioyo yao“. Mambo kama haya yamewai kutokea na hata leo
yanatokea pia.
Ijapokuwa
yanawezekana kuwa mambo katika habari hii ambayo si rahisi kueleweka,
inaonyesha wazi kuwa mtu yeyote asiye na haki anaweza akawasiliana na ulimwengu
wa maroho, lakini umaarufu wake kwa watu wa Mungu ni kuwachafua iwapo angepata
nafasi ya kufanya hivyo. Nimenukuu habari hapo juu ili kuonyesha kuwa watu
wanaweza kuwasililana kimakosa na maroho, hata wakristo wanaweza kufanya hivyo.
Ijapokuwa bila shaka sio habari yote hiyo ambayo inaweza kuwahusu waandishi
hawa wa kisasa, bado kwa namna fulani, ninafikiri wameiharifu mipaka halali
kama ilivyoonyeshwa katika 2 Kor.11:1-15.
Nilikuwa nasoma
kitabu kimoja ambacho kimezungukia kasoro zote nilizo zitazama katika makala
hizi tatu. Nilipokuwa nikisoma, niliamini kuwa mwandishi huyo amehalifu na
ametumbukia katika udanganyifu. Kisha nikasoma kuwa mwandishi wa kitabu hicho
yeye mwenyewe alikuwa analifahamu hilo. Yeye ni mwenye historia ya nyuma ya
Kimarekani ya asili, naye anashuhudia kuwa, akiwa kama mkristo, bado mambo ya
siri zake za hapo kale (au pengine tungeweza kusema kwamba unajimu au uchawi)
ule uwezo wake wa kinajimu alioupata kutokana na desturi au mila za kihindi,
ungeweza kujitokeza tena ndani yake na angeweza kufanya mambo yenye fumbo za
kiunajimu (akiendesha ndani ya ulimwengu wa roho) ambao kwa uaminifu kabisa
anakiri wazi kuwa hiyo haikuwa karama ya Roho Mtakatifu. (Ninaamini kuwa
mambo kama hayo yanaweza kutokea na yanatokea siku za leo). Lakini ndipo
anaendelea kusema kuwa alimwomba Bwana ili aondoshe na kuangamiza kabisa uwezo
huo aliokuwa nao hapo kale. Hilo ni jambo jema. Lakini tena anaendelea
kusema kwamba Roho Mtakatifu alishuka chini na kufikia kwenye ujuzi huo wa
zamani na akawasafisha ili kuwatumia kwa ukamilifu zaidi! Hilo sio jambo
jema! Na kadiri mtu anavyosoma kitabu, mtu huyo anaona kuwa huo ni ushuhuda wa
uwezo wake wa mambo yake ya “kiunajimu” ya hapo kale yakimpeleka kwenye
udanganyifu wa mambo ya uzoefu wa maroho ya kigeni ambayo hayatokani na Mungu.
Wamebuni mafundisho mapya na uzoefu ambao wao wanauita “Baraza la Bwana” ambapo
unaitwa mbele ya uwepo wa Bwana kwa ajili ya aina fulani ya mazungumzo. Sio
uchaguzi wako. Mwandishi wa kitabu hicho wakati fualni alijisikia “ameitwa”
kwenye uwepo wa Mungu pamoja na mtu mwingine, ambako Bwana aliwauliza iwapo Mungu
sasa anaweza kuihukumu dunia hii. Na eti kwa sababu ya maombezi yao, ulimwengu
uliachiliwa kutokana na hukumu ya dunia nzima kwa wakati ule, hii ni kulingana
na watu hawa wawili wote kwa pamoja walivyoona na kuskia katika maono yao!
Katika aliamini kuwa yeye mmoja na rafiki zake wanane walikuwa wakiitwa kwenye
baraza la Bwana, lakini sasa yeye alishangaa kuona kuwa imekuwaje watu wote
tisa waweze kusikia kitu kile kile na kuyaona maono yale yale (yanayofanana)
kwa wakati mmoja. Hata hivyo alijisikia kuwa anapaswa “kutii na”
wakaondoka pamoja, naye anasimulia jinsi ambavyo wote walivyoona kitu kile kile
“katika roho” na kusikia kitu kile kile – sauti na maono ambayo wote kwa pamoja
walipata kuyajua! Huo ndio upuuzi wa makutaniko ya mizimu, unajimu na ulozi!
Hakuna hata moja kati ya hayo inayotokana na Mungu. Halifanani na chochote
katika maandiko ya neno la Mungu. Wamefanya makosa ya nje hatari sana na
wamedanganywa vibaya na hali hiyo italeta madhara mabaya. Kwa hakika huu ni
“moto wa kigeni”! Yeye anasimulia maono hayo kwa kirefu katika kitabu chake
lakini bado ni ya tabia ya kigeni na wala hayaleti sura yoyote ile ya kibiblia
au hayana misingi yoyote ile ya Kimungu ndani yake. Ni kutokana na wanaume na
wanawake wa jinsi hii ndio wanao leta mafundisho ya aina hii. Kama ilivyo
kuwa kule Korintho nyakati za Mtume Paulo, ndivyo inavyotokea nyakati za leo
pia. Watu wamejazwa maono yao wenyewe, wakimleta roho mwingine, Yesu
mwingine, Injili nyingine. Wao wanaamini, kwa kadiri mnavyojua kuwa kwa kufanya
hivyo wanakuwa wakimtumikia Mungu, lakini kwa ujumla kwa huzuni kubwa
wamekosea.
Mambo haya yote
huwaletea huzuni watu wengi wa leo kadiri wanavyo ona udanganyifu wa aina hii
na kuchanganyikiwa kunako sababisha maumivu ya moyo, pamoja na matengano
ikiwasababisha watu wa Mungu kukosea na kuwaondoa kutoka katika kweli na
kuwaingiza kwenye vifungo Inaonyesha kuwa nyakati hizi shetani anajitahidi
kufanya kila awezalo kudanganya ikibidi hata wateule. Je, anatumia njia gani
kujaribu kufanikisha jambo hili? Kwa mujibu wa Yesu Kristo. Wakristo wa uongo
(hii inamaana kuwa, ni wale wenye upako wa uongo) na watatokea manabii wa uongo
nao watatoa ishara kubwa na maajabu. Ishara, maajabu manabii wa uongo na upako
wa uongo ni vitu ambavyo shetani atatafuta kudanganya ikiwezekana hata wateule
Mt. 24:24. Ikiwa mtu yeyote anaweza kutoa aina yoyote ya ishara na maajabu,
au wanajifanya wenyewe kuwa ni mitume wenye nguvu au manabii, hapo ndipo wengi
wa watu wa Mungu huonekana kuwa tayari kupokea mafundisho yoyote yale
yanayoambatana nao! Hizo ndizo nyakati tunazoishi.
Kwa hiyo, ikiwa
watu wanapata matatizo katika maisha yao, sababu kuu ni kwamba wamechagua
kuishi pasipo imani na kutokuwa na utii wa neno la Mungu. Na nyakati za leo ni
yote mawili hufanyika; yaani mafundisho ya uongo na uzoefu wa uongo ndiyo
yanayowapeleka watu wa Mungu kuwa mbali na kweli na kuishi kwa ile kweli; sio
kule kujiingiza katika mapambano ya maandiko kiroho ambako ndiko kunako
sababisha matatizo, isipokuwa ni mafundisho yaliyokosewa ya aina hii ya vita
vya kiroho, hiyo ndiyo chanzo cha mchanganyiko mkubwa, udanganyifu pamoja na
matatizo.
Fungu la
Maandiko Wanayoyatumia
Sasa tutaangalia
aina ya aya ambazo waandishi hawa hupenda kuzilinganisha ili wapate
kuyahalalisha makosa yao. Moja kati ya zile kuu inapatikana katika Efeso 6 na
tutaanza kwanza kuitazama sura hii, pamoja na kufikiria kwa kifupi juu ya vita
vya kiroho ni nini hasa, kabla hatujaendelea kuangalia katika sura
nyinginezo.
EFESO 6:10-20
Hii penginepo ni
sura ya msingi mkuu na ambayo mara nyingi hunukuriwa vibaya, ambayo hutumiwa
kuunga mkono mafundisho yao kuhusu roho zitawalazo katika nchi. Mara nyingi
hutumiwa na hawa waandishi wa kisasa ili kuainisha mapambano ya kiroho kuwa
yanahusika na kuomba dhidi ya, na kuzifunga mamlaka na uweza ambayo inahusisha
na roho zile za kiinchi, hii ni kulingana na tafsiri yao. Kama tunavyoangalia
katika sura hiyo tuliyoitaja hapa, tunaona kuwa sura nzima haihusiki na
chochote juu ya mambo kama hayo (niliishughulikia kwa makini sura hii pia pale
nilipokuwa nafikiria ju ya maombi katika Agano Jipya kwenye makala yangu ya
kwanza). Katika mstari wa 10 na wa 11, mtume Paulo anatusihi tuwe hodari katika
Bwana tukizivaa silaha zote za Mungu ili tupate kuzipinga hila za shetani. Kwa
nini tunahitaji silaha za Mungu? Ni kwa sababu adui yetu ni wa kiroho na
kushindana kwetu ni kwa kiroho. Ule mstari wa 12 unatuambia kwamba kushindana
kwetu, au vita vyetu sisi, sio juu ya damu na nyama, bali ni juu ya falme na
mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili juu ya majeshi ya pepo wabaya katika
ulimwengu wa roho”, (katika hali hiyo hatuhitaji kufafanua majeshi hayo yote ya
kiroho, isipokuwa ni bora kuendelea kufuata hoja za mtume Paulo hapa). Kwa
sababu ya hilo, tunahitajika kukamilika kiroho. Peke yetu wenyewe tu, hatuwezi
kuushinda upinzani huu wa kiroho na hila! Sasa, baada ya kuliweka hili wazi
katika ule mstari wa 12 mtume Paulo anatusihi kufanya nini hapo? Je, yeye
anasema kwamba, “kwa kuwa upinzani wetu ni wa kiroho, jichukulieni wenyewe
silaha za Mungu ili kwamba unaweza kuomba dhidi ya mamlaka hizi na uweza na
kuzifunga kwa jina la Bwana”? Je, hivyo ndivyo mtume Paulo anavyozielewa vita
vya kiroho? Je, hii ndiyo njia ya kupata ushindi? Hapana! Hivyo siyo hoja yake
kabisa!
Anatuambia
katika ule mstari wa 13 kwamba tutwae silaha zote za Mungu, ili tupate
kuweza kushindana siku ya uovu na tukisha yatimiza yote kusimama! Mtume
Paulo anazungumza kuhusu silaha ambazo zitatuwezesha kuyashinda majaribu na
vishawishi mbali mbali ambavyo majeshi ya kiroho ya uovu yanaweza kutuingizia,
na hatimaye tuweze kushinda. Anazungumza kuhusu mwenendo wetu kiroho katika
Bwana. Hivyo mtume Paulo anatutia moyo kwamba “tupate kusimama”, hiyo ina
maana kumpinga shetani na kuyashinda vishawishi vyake katika maisha yetu ya
kila siku. Ili kuyafanya hayo tunapaswa kuipata kweli ya Mungu, na kuvaa dirii
ya haki (mstari wa 14). Kweli ya Mungu itashughulikia uongo wa shetani na pia
itatuadilisha na kututia moyo. Kusimama katika haki tuipatayo katika Kristo
kutaitunza mioyo yetu ikiwa imesafishwa na kulindwa. Ushuhuda wa Kristo
unapaswa mara zote uwe hai ndani yetu ili kwamba tuwe tumejiandaa
kuwashirikisha watu wengine Injili hii (mstari wa 15). Kisha katika ule mstari
wa 16 mtume Paulo anatusihi, “zaidi ya yote, tuitwae ngao ya imani ambayo kwa hiyo
itatuwezesha kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu”. Anachokiongelea
hapa ni kujishughulisha na kukataa malaumu yote, uongo na mashauri ya shetani
ambao anatutupia ili kutufanya tumtilie mashaka Mungu pamoja na upendo wake
kwetu, ili kutufanya tujisikie wenye kuhukumiwa, tusio na maana; na pweke ili
kutufanya tujisikie wasikitivu au tunao jihurumia. Tunapaswa kuyashughulikia
hayo yote kwa kuiweka imani yetu na matumaini yetu kwa Mungu na katika yale
aliyokwisha yasema. Wote huwa tunashawishiwa na kujaribiwa kama ilivyo katika
mstari huu; sote tunajua yanafananaje mambo hayo. Lakini sasa hayo ndiyo
mapambano yetu kiroho na tunapaswa kuchukua ngao ya imani na wala tusijiachie
wenyewe kudhurika kwa uongo wa shetani na mashauri yake. Ni kweli kuwa katika
hali hii wengi wetu huanguka. Hatusimami kama mtume Paulo anavyo tusihi, na
hivo tunaupoteza ujasiri wetu, furaha na amani yetu katika Bwana. Tunaishia
katika kujisikia kuhukumiwa na tusio na maana, tukishangaa iwapo ni kweli Mungu
anatupenda na kutujali. Katika hali ya jinsi hii, kwa kweli hatuwezi kukua
katika Bwana na bado kuna upungufu wa matunda juu ya Mungu. Sura hii inapiga
moja kwa moja nyumbani katikati ya mwenendo wetu na vita vyetu kiroho.
Ukweli ambao
mtume Paulo anauelezea hapa ni wa lazima kwa ajili ya mwenendo wetu kiroho na
kimapambano. Ni wa maana na ni dhahiri. Wanakaa katika moyo wa maisha ya kiroho
na ya ushindi. Hivyo ndivyo inavyohusika na vita vya kiroho. Sio kuanza
kuikunja “mikono ya kiroho” na kupiga kelele na kumkemea shetani na maroho ya
nchi. Pasipo maswali yoyote, ni vyepesi zaidi na inaashiria kimwili zaidi mtu
kuomba dhidi ya roho mbaya katika maombi ya mikutano, kuliko ilivyo katika
maisha ya kila siku katika imani, upendo na utii kwa Mungu kusimama katika
silaha za Mungu; hi ya mwishoni inawakilisha vita vya kiroho kulingana na
maandiko, lile la kwanza halina lolote!
Mtume Paulo
anaendelea katika kutusihi tuchukue chepeo ya wokovu – ambayo itatunza na
kulinda akili zetu katika kristo – na upanga wa roho, ambao ni neno la Mungu.
Tukiwa tumevaa silaha zote za Mungu, Paulo anatusihi sasa kuomba (mstari wa
18). Haya, je sasa tunatakiwa kuomba dhidi ya mamlaka na uweza na kuzifunga? Sasa,
kwa kuwa tumepata silaha za Mungu, tunapaswa kusimama dhidi ya roho zitawalazo
maeneo na kufunga uweza wake? Hapana. Sio hivyo, kulingana na mtume
Paulo. Lakini Je, hivyo si ndivyo silaha inavyotakiwa kuwa? Kutujaza nguvu
katika maombi kuzifunga roho mbaya? Hapana; sio hivyo, kulingana na mtume
Paulo. Mtume Paulo hataji kuomba dhidi ya maroho na kuzifunga. Anazungumza
kuhusu “kuomba kwa sala zote, na maombi kila wakati katika roho, mkikesha kwa
jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote na kwa ajili yangu
mimi…..”
Kwa hiyo
kuenenda kiroho, na kuzishinda kwa mafanikio hila za shetani katika vita hivi
vya kiroho katika maisha yetu ya kila siku, kunatuwezesha kuomba kwa ufasaha
kwa ajili ya watakatifu. Kwa uwazi kabisa maombi ni sehemu muhimu ya
mwenendo wetu kiroho mbele za Mungu, lakini tunawezaje kuomba kwa ufasaha pale
tunapolitilia shaka pendo la Mungu na matunzo yake kwa ajili yetu, pale
tunapojisikia kuhukumiwa watu tusio na maana, au tusiopendwa, pale tunapokuwa
na uchungu, kutokusamehe na ugumu mioyoni mwetu; pale tunapokuwa katika
kutokuamini! Kwa hiyo tunaweza kuona kuwa, mtume Paulo anatupatia amri sahihi
katika sura hii – uhusiano wetu na Mungu, pamoja na mwenendo wetu mbele zake
lazima uwe safi kabla hatujaweza kuwa wenye mafanikio kiroho katika maeneo
mengine. Kwa hiyo vita vya kiroho vinahusika na kupinga vishawishi vya shetani
na uongo wake katika mwenendo wetu wa siku kwa siku na Bwana – tukivaa silaha
zote za Mungu. Hilo ndilo linatuwezesha kuomba kama itupasavyo kwa ajili ya
watakatifu.
Sura hii yote ya mtume Paulo haiwakilishi mbinu fulani fulani au maagizo
ya kuyashambulia na kufunga maroho mabaya kupitia maombi! Kwa urahisi tu anasema kwamba, kwa sababu adui yetu ni wa kiroho, kwa
hiyo silaha zetu zinapaswa kuwa za kiroho, katika mapigano yanayotuhusu ili
kupinga vishawishi, uongo na mashauri ya kutokuamini ambayo shetani atayapanda
ndani ya mioyo yetu na maisha yetu. Kwa kweli, mbali ya mapepo kufukuzwa nje ya
mtu mmoja mmoja, haupo mfano hata mmoja katika maandiko unao mwonyesha
mtakatifu yeyote moja kwa moja akishambuliana na kuzifunga mamlaka zozote zile,
uweza au roho zitawalazo maeneo, katika maombi. Maombi yote katika Biblia
yanaelekezwa kwa Mungu.
Katika maombi
watu wa Mungu wanakiri na kutukuza Uungu wa matoleo yake na wanatoa haja zao
kulingana na mafunuo ya neema ya tabia ya uungu wake. Na maombi yao mengi ni
kwa ajili ya watu wa Mungu. Kama inavyoonyeshwa na mtume Paulo katika sura hii.
Vita vya Kiroho
Kulingana na Maandiko – kwa kifupi.
Hatutakwenda
kuangalia kwa undani juu ya somo hili katika makala hii, lakini ningependa kutoa
muhtasari wa ukweli huu wa lazima; huku tukifikiria juu ya Efeso sura ya 6.
Hebu tuanze
mwanzoni kabisa; katika bustani ya Adeni mambo yote yalikuwa mema, lakini
baadaye nyoka alikuja katika bustani. Je, hiyo ilikuwa ni kuvamiwa kwa nchi ya
Mungu na mapepo? Je, haya yalikuwa ni mashambulizi ya ghafla na upenyezaji
usiotakiwa ili kuharibu kusudi la Mungu? Kibinadamu, tunaweza kufikiri, kuwa ni
jambo la kuhuzunisha kuona shetani kupewa nafasi katika bustani, wakati kila
kitu kilikuwa salama na pengine tunashawishiwa kufikiri kuwa Adamu na Hawa
wangeweza kufanya maendeleo iwapo kama isingekuwa huo upenyezaji wa shetani.
Tunaweza kufikiri ingeweza kuwa ni vema kuitisha mkutano wa maombi na kuanza
kumfunga na kumkemea shetani au kumtaka Mungu atumie uwezo wake kumfukuza
shetani. Lakini pengine tunaweza kupata ufahamu mzuri zaidi na undani wake juu
ya tukio hilo kwa kuyatazama maandiko mengine.
Kama tutaangalia
katika kitabu cha kumbukumbu ya torati sura 8:2,3, Ayubu 1:6-12 na Mathayo 4:1,
kwa uangalifu na moja baada ya nyingine, tunaona kuwa Mungu aliruhusu watu
wake pamoja na mwanae pekee ili aweze kujaribiwa na kushawishiwa kwa kupitia
mazingira na kwa mashauri ya shetani. Kusudi la Mungu ni kuona kuwa hakuna
mtu hata mmoja awezaye kuumizwa, kuharibiwa au kuanguka katika dhambi bali
waweze kupitia katika mazingira hayo yanayowajaribu na kuwapima. Na ilikuwa ni
mazingira hayo ambayo ndiyo yangewataka kufanya uchaguzi! Kupitia mambo yote
mawili lile linalohusu namna walivyofikiri na lile lihusulo jinsi walivyoweza
kufanya. Na ilikuwa ni kupitia uchaguzi huu sahihi, kwa kuchagua kumwamini
na kumtii Mungu ndiko kutakako wafanya wakue kiroho katika maumbile na katika
kumfahamu Mungu. Majaribu na shida za jinsi hiyo kwa kweli ndizo zilizokuwa ni
njia yao ya kukua katika neema na kumfahamu Mungu. Mungu hakuhitaji watu
wake waanguke au watende dhambi. Hiyo ni kinyume cha tabia yake! Yeye alipenda
kuwaleta katika ufahamu na sura yake yeye mwenyewe, kwa wao kuukataa uovu na
kuchagua mema. Mistari inayofuatia inabeba ukweli huu tunao uangalia hapa Rumi
5:3-5; Heb.5:8,9,13,14; Yak.1:2-4; 1Pet.1:6-8.
Kusudi la Mungu
la kumturuhusu shetani amjaribu Adamu na Hawa ilikuwa ni kuwawezesha kukua
katika neema na haki ya Mungu wao, na katika upendo wao kwa yeye. Na
walipokabiliana na mashauri ya shetani jibu la Adamu na Hawa halikuwa ni
kuitisha mkutano wa maombi ili kumfukuza shetani nje ya Adeni; isipokuwa ni
kuvaa silaha zote za Mungu na kuupinga uongo wa shetani na sio kuyaruhusu
mashauri ya shetani yapate sehemu katika mioyo na akili zao! Hili la
mwishoni linawakilisha vita vya kiroho; lakini lile lililo tangulia
halihusiki na lolote. Kama wangaliweza kulifanya hilo la mwishoni, ndipo
shetani angewaachia Yakobo 4:7. Shetani alipomjia Hawa angepaswa kutumia
upanga wa roho dhidi yake shetani kwa sababu alilijua neno la Mungu kwamba
watakufa iwapo watakula mti wa ufahamu wa mema na mabaya. Lakini yeye
hakuuchukua upanga wa kiroho dhidi ya uwongo wa shetani; hakuchukua ngao ya
imani dhidi ya mashauri yake yanayoendelea. Mungu alikuwa ni mwema sana kwa
Adamu na Hawa kwa kuwaumbia kila kitu kwa ajili yao naye kuwaumbia kwa mfano
wake mwenyewe ili kwamba waweze kuwa na ushirika pamoja naye.
Yule nyoka
alipomjia, Hawa angeweza kutumia upanga wa kiroho dhidi yake, kwa vile alilijua
neno la Mungu kwamba wangekufa iwapo wangekula tunda lile. Lakini Hawa
hakuushika upanga wa Roho wala ngao ya imani juu ya maongo ya Shetani. Alisahau
ule wema wa Mungu kwao akiona tunda lile alilolitaka ili kujipendeza. Hivyo
shetani anawadanganya na kuwaongoza kuelekea kwenye kiburi. Na hasipo dirii ya
haki na chepeo ya wokovu kwa kule kumruhusu mawazo mabaya kuhusu Mungu yaweze
kupandwa ndani ya moyo wake na akili zake. Mawazo mabaya ya kutokuamini ambayo
shetani aliyapanda ndani ya moyo wake, ilimfanya Mungu aonekane kama ni mtu
asiyetujali na kutupenda, kana kwamba anayekataza mambo mazuri yasitupate,
kwamba aonekane ni mtu asiyetutakia mema ila mabaya. Mungu alikwisha
waambia wasile mti ule kwa ajili ya manufaa yao wao wenyewe na wokovu wao. Yeye
alipenda wawe kama yeye alivyo, lakini shetani aliwashauri kuwa Mungu alikuwa
anawazuia kula tunda la mti ule, kwa sababu hakupenda mambo mema yawajie.
Hakupenda wao wawe kama yeye alivyo! Ni kweli shetani ni baba wa uongo! Anaweza
tu kuzungumza uongo, na kusudi lake ni kutokumheshimu Mungu na tabia yake
ndani ya mioyo na akili za watu, ili kwamba watu hao wasiweze kuweka imani zao
na matumaini yao kwa Mungu. Kwa hakika pasipo imani haiwezekani kumpendeza
Mungu, naye asiyeamini amemfanya Mungu kuwa ni muongo, 1Yoh.5:10. Pasipo imani
hatuwezi kuufaidi wokovu wa Mungu pamoja na neema yake ambao tumepewa kupitia
Kristo. Jambo hili kwa hakika shetani analijua na hapo ndipo anapopazingatia na
kuelekeza shughuli zake, ambayo ni kutufanya sisi tumtilie shaka Mungu!
Shetani huja kupanda
hoja na mawazo yasiyo na faida ndani ya mioyo ya watu, ikiwa pamoja na watu wa
Mungu. Kwa kutumia mashaauri yake yanayoendelea, yeye hutafuta kuziinua hoja
zake hizo kinyume na ufahamu wa Mungu; na kuangamiza ile sura na ufahamu wa
Mungu. Mashauri yake hayo yakudanganya yanaendelea kushikilia akili za watu
wale wanaoyakubali. Ni “mambo ya juu” yanayopinga maarifa na utukufu wa Mungu,
2 Kor.4:4-5. Katika sura hii, ndani ya waraka wa Wakorinto wa pili, Mtume Paulo
anaelezea ukweli unaofanana na ule ulioko katika Efeso 6, yaani, vita vyetu sio
vya kimwili, lakini silaha zetu zina nguvu kupitia Mungu, na kuziangusha “kila
ngome” za aina hii, hoja za udanganyifu ndani ya akili za watu, ambazo
zinapinga ukweli na ufahamu wa Mungu. Sura hii haiwakilishi mbinu ya kuzifunga
roho zitawalazo katika maeneo ambazo ziko mahala fulani huko angani, bali
inakusudia kuonyesha silaha za ki-Mungu ambazo tunazo pale tunaposhughulika na
hoja za udanganyifu za shetani! Ufumbuzi kwa Hawa, haikuwa ni kujaribu kumfunga
shetani, isipokuwa ni kupinga na kukataa uwongo wake na ndipo angeweza
kumkimbia, Yak. 4:7.
Majaribu ya
jinsi hii yanaruhusiwa na Mungu. Kristo alipokuwa anabatizwa, mara moja akaongozwa
na Roho Mtakatifu kwenda nyikani kujaribiwa na shetani, Mt. 4:1. Hayo
yalikuwa ni maongozi ya ki-Mungu. Wala haikuwa ni kujipenyeza kwa mapepo!
Hiyo ilikuwa ni msingi wa makusudi alioudhamiria Mungu; haikuwa ni ajali ya
bahati mbaya ili kuiharibu kazi ya Mungu. Ilikuwa ni kupitia majaribu
haya halisi, ndiyo yanayotufanya tuwe imara katika Mungu na kukua kiroho.
Tunasoma katika Injili ya Luka kuwa Yesu alienda nyikani akiwa amejaa
Roho. Na baadaye alirudi akiwa na nguvu za Roho (Luka 4:1-14), na hilo
ndilo kusudi la Mungu kwetu. Lakini sasa Mungu anatutazamia tumchague, kumpenda
na kumwamini yeye! Ikiwa hatuwezi, ndipo majaribu yanafunua udhaifu,
kujipendeza kwetu au matendo maovu katika mioyo yetu, Kumb.8:2,3. Sura hii
yenye msingi katika kumbukumbu ya Torati inatuonyesha kwamba Mungu anayaruhusu
majaribu ili kutufanya tuweze kujifunza kumtumaini yeye kuliko kitu kingine
chochote kile. Hata mbele ya mahitaji mengi na masumbufu; neno lake ndilo
lipaswalo kuwa la maana zaidi kwetu kuliko baraka zozote za muda zilizo nje.
Upendo wetu na imani unapaswa uendelezwe na kutumbukia ndani zaidi nyakati kama
hizo – na hivyo haitatusababishia sisi kukua katika maumbile kiroho tu – bali
pia itamtukuza Mungu!
Hebu angalia
jinsi Yesu anavyomshughulikia shetani pale nyikani. Yesu hakumpigia makelele
shetani na kumfunga kwa kujaribu kumfuata yeye! Kwa hakika, yeye ameongozwa
katika nyika ili aweze kujaribiwa na shetani. Na shetani mara zote huja na aina
hiyo hiyo ya mashauri: “Mungu wako yuko wapi? Je, wewe ni mwana wake hasa? Una
njaa na ni muhitaji. Je ni kweli anakujali wewe? Kwa nini hufanyi kitu kingine
chochote kile sasa ili kutimiza hitaji lako? Fanya ili kujisaidia wewe
mwenyewe! Fanya ili kujipanga mwenyewe. Ikiwa utajifurahisha mwenyewe, tazama
utanufaikaje na jinsi gani ambavyo mambo yako yatakuwia rahisi!” Mambo kama
hayo ndiyo tabia ya mashauri yake. Lakini Yesu alijibuje? Alijibu kwa upanga
wa roho – kwa neno la Mungu. Naye ananukuru katika kumbukumbu la Torati
8:31 Israel wamekuwa wakitembea jangwani kwa miaka 40; na Yesu aliitumia siku
moja nyikani kwa ajili ya kila mwaka wa miaka hiyo, akiwa anajaribiwa, kama
vile na wao walivyojaribiwa. Lakini Yesu hakuhusika na “mahitaji” yake
mwenyewe, wala hakuweza kumpatia muda wowote ule shetani kwa kuyasikiliza
mashauri yake – Yesu yeye aliishi kwa neno la Mungu, akimheshimu na kumwabudu
Mungu zaidi kuliko lolote lile lingine! Yesu alimpinga shetani na shetani
akamwachia kwa muda.
Lakini Israel
alishindwa kule jangwani. Wao hawakuishi kulingana na neno la Mungu pale
walipokabiliana na shida na mahitaji. Hawakuchukua upanga wa imani bali
waliruhusu shetani ajaze mioyo yao na akili zao kwa mashauri ya uongo kumhusu
Mungu. Na hivyo mashauri hayo yakajenga ngome katika fikara zao nao wakampinga
Mungu na kukufuru tabia yake. Asili ya vita vya kiroho vya shetani ni
kuwaelekeza watu waingie katika hali ya akili na moyo ambapo watakuwa
wakifikiri kama Israel walivyofikiri. Katika Kumb. 1:27, tunaambiwa kuwa kwa
kweli Israel waliamini kuwa Mungu alikuwa amewachukia na kwamba amewaleta
jangwani ili kuwaangamiza! Na hivyo ndivyo walivyoweza kufikiri hata baada ya
kuona yale maajabu ya Mungu aliyowafanyia huko Misri na katika jangwa! Huo
ndio udanganyifu wa dhambi na kutokuamini! Na hizo ndizo mbinu za shetani
kutufunga sisi tufikirie mambo mabaya kuhusu Mungu na kuutilia shaka wema wake
juu yetu. Ni kwa njia hiyo ndivyo shetani anavyo tafuta kutuleta au kutuweka
nje ya neema ya Mungu, wokovu na urithi ambao ametuwekea. Tunaweza kutenda
dhambi, lakini ikiwa tutajinyenyekeza wenyewe na kumtumainia Mungu kuutafuta
msamaha wake, ndipo atatusamehe kulingana na neno lake. Lakini ikiwa mtu
atautilia shaka wema wake na asili yake Mungu, mtu huzo atawezaje kupokea
chochote toka kwa Mungu? Tunaelewa kuwa Israel alipoteza kutokana na
kutokuamini. Lakini hawakuweza kumlaumu shetani kwa ajili ya hali ya mioyo
yao. Mungu alikuwa anawategemea wamwamini na kumtii yeye. Majaribu hayo
yaliweza tu kufunua hali ya mioyo yao.
Ni kazi ya
shetani kuwapata watu ili waweze kuamini mambo haya, lakini sisi tunahusika
kama wana wa Mungu, ikiwa tutajiruhusu kushawishika katika kuamini mambo hayo!
Hivyo ndivyo moja ya sababu kuu za kwa nini Paulo anaandika yale anayofanya
katika Efeso 6.
Kama ilivyokuwa kwa Hawa katika bustani, na ilivyo kwa Israeli kule
jangwani, na ilivyo kuwa kwa Yesu kule nyikani, ndivyo itakavyokuwa kwako wewe
na mimi. Shetani hutujia ili kupanda
mashaka ndani ya mioyo yetu dhidi ya Mungu. Dhambi hii ya kutoamini inavunja
ushirika wetu na Mungu na inatuzuia kupokea mambo mema aliyo tuwekea Mungu,
inapofusha mioyo yetu isione kweli na inampa nafasi shetani kutufanya
mateka kwa aina zote au mwenendo mbaya. Hivyo tunapaswa kumpinga na kupigana
vita vizuri vya imani, ambavyo kwa hiyo tumetunzwa salama na kukua na ambavyo
kwa hiyo Mungu anaheshimika!
Mmoja wa
wahamasishaji wakuu wa mafundisho hayo ya kisasa anashauri kuwa Yesu alishiriki
katika “vita vya kiroho vya kiwango cha mbinu” (strategic – level spiritual
warfare) ambapo alijaribiwa nyikani. Anasema kuwa, eti hayo majaribu
aliyoyapata Yesu kule nyikani yanawakilisha kiwango cha juu cha mapambano ya
kiroho na shetani, ambayo wachache wetu tu au hakuna hata mmoja awezaye
kuyapata. Kwa vyovyote vile jambo kama hilo ni uwongo mtupu! Sote huwa
tunapitia katika majaribu yanayofanana vile vile kama hayo, ndani ya maisha
yetu! Shetani hatokezi kwetu kama aina fulani ya dudu baya lenye mapembe
kutushurutisha kufanya makosa. Ingekuwa ni wazi! Tungeweza kuona kupitia mbinu
hizo na kushituka! Shetani yeye hutumia hila. Huja katikati ya majaribu na
shida; na kujaribu kupanda lile linaloonekana kama la “maana” au “mashauri
yenye kusihi” na mawazo katika “akili” zetu. Lakini mashauri yote hayo yanalo
lengo moja tu na yanatuongoza kuelekea katika aina moja ya hali ya akili –
kutufanya tumtilie mashaka Mungu na tutende kwa kujitegemea! “Yuko wapi sasa
Mungu wako? Je, ni kweli anakujali? Kwa nini basi huchagui njia nyepesi?” Haya
ndiyo aina ya mawazo ambayo shetani anaweza kuyapandikiza ndani ya akili zetu.
Nasi tunaweza kuona kutokana na mistari iliyotajwa hapo juu, kwamba iwapo
tutakuwa tunaonyesha haja ya kutaka kutosheleza miili yetu au sisi wenyewe,
kuliko kumpenda na kumtii Mungu, ndipo majaribu ya shetani yatatujia. Kwa
vyovyote vile shetani hawezi kutujia na kutusimamisha juu ya jengo, wala
hataweza kuja na “kutupatia” ulimwengu iwapo tutamwabudu yeye. Mazingira haya
maalum kwa hakika ni ya kipekee kabisa kulinganisha na majaribu ya Yesu. Lakini
lile ambalo sio la kipekee ni kwamba shetani anatujia na aina ile ile ya
majaribu kwetu kila mmoja. Ikiwa shetani hatafanikwa kutupata tumtilie mashaka
Mungu, ndipo anajaribu kutupata tutumbukie mbali zaidi katika yale
tunayoyaamini ili kwamba tuweze kuwa na kiburi na tuishie katika kumjaribu
Mungu – ambayo ndiyo yale ambayo shetani anajaribu kuyafanya kwa vyovyote vile,
ili kumtia moyo Yesu aweze kurukia juu ya hekalu, au shetani atajaribu kutia moyo
au kuweka katika akili zetu chanzo cha tendo fulani ambalo litatufurahisha,
kufanya mambo yawe rahisi kwa ajili yetu, kutupatia faida au litutukuze sisi.
Hii ndiyo ilikuwa tabia ya jaribu la mwisho la Yesu. Lakini maandiko yote
yanatusihi kujikana wenyewe, kumpinga shetani na tujikabidhi wenyewe kwa Mungu
na kuyaweka matumaini yetu kwake. Hivyo ndivyo alivyofanya Yesu, ambaye katika
maeneo yote alijaribiwa kama tunavyojaribiwa sisi, (Heb. 4:15), na hivyo ndivyo
itupasavyo na sisi kufanya. Hivyo ndivyo tunabyokua kiroho kiroho, na hivyo
ndivyo tunavyoweza kuingia katika urithi ambao Mungu ameutayarisha kwa ajili
yetu katika Kristo.
Tabia halisi ya
vita vya kiroho kama ilivyo kuwa kwa Adamu na Hawa, kama ilivyo kuwa kwa Israel
kule jangwani, kama ilivyo kuwa kwa Yesu kule nyikani na kama ilivyo kwako wewe
na mimi, inatupasa kupinga na kukataa mashauri yote ya aina hii ili kusudi
yasipate nafasi katika mioyo yetu. Na tunapaswa kufanya hivyo hasa tuwapo
katikati ya majaribu, wakati wa shida na maumivu, tukiwa na juhudi katika imani
ya Mungu pamoja na wema wake ambayo inalikumbatia neno lake. Na katika hili
agano jipya sasa tumepewa nguvu ya kumpinga na kumshinda yule adui kwa roho na
ule uzima wa Kristo uliomo ndani yetu.
Nimewahi
kuhudhuria katika makanisa ambayo tumeweza kuomba dhidi ya shetani na kuzifunga
roho chafu. Wakati fulani mtu mwingine angeweza kuomba, angeweza kumfunga
shetani na kumtupa katika bahari au shimoni! Ninakiri ya kuwa niliweza
kushangaa niliona ni jinsi gani shetani alivyoweza kutoka huko alikotupiwa
baada ya kuwa tulikwisha “mfunga” katika mikutano ya maombi yetu! Nilijiuliza
iwapo yale tuliyokuwa tukiyafanya yalikuwa ni mambo ya kiroho au la, na iwapo
ilikuwa na ufanisi wa kweli mbali ya kutufanya sisi “tujisikie vizuri”. Na
ilitufanya sisi tujisikie vizuri na “wenye ushindi” kule kupandisha sauti zetu
na kupiga kelele na kuzifunga roho chafu – kwa vyovyote vile kulikuwa upande wa
washindi! Ninaamini kuwa shetani na roho chafu na kwamba wapo kazini kupinga
kazi ya Mungu ndani na kati ya watu, lakini kwa uaminifu kabisa siwezi kusema
kuwa kwa kelele katika mikutano ya maombi yetu ambayo inakazia juu ya shetani
na kuomba moja kwa moja dhidi yake, kuwa inaweza kuwa na ufanisi wowote ule wa
kweli. Hapa sisemi kuwa haitupasi kuomba juu ya mazingira ambayo yanaonyesha
kuwa shetani anaingilia, au haitupasi kupiga kelele katika maombi. Sisemi
hivyo. Napenda tu kuwatia moiyo watu wa Bwana katika maombi, lakini iwapo
tutaangalia katika maandiko kwa uaminifu, hatuwezi kupata kuiona aina hii ya
uombaji kuwa ndio njia ya kumshinda adui.
Niliwahi
kujihusisha na aina hii ya maombi hapo zamani, na bado sijabadili kuamini
kwangu juu ya Mungu au shetani, lakini ninatakiwa kukabiliana na yale ambayo
kwa kweli maandiko yanaonyesha na kufundisha, kuhusiana na kuomba pamoja na
vita vya kiroho. Vile vile nilipaswa kukabiliana na ukweli kwamba, mbali ya
kutufanya tujisikie wazuri, hatukuweza kwa hakika kuelewa au kusikia ushahidi
wowote kwamba kumfunga shetani kwetu au roho chafu kuliweza kuleta ufanisi
wowote ule. Katika hayo yote kuhusika kwangu ni kwamba tunajaribiwa na Ibilisi
mwenyewe kutuingiza katika kiburi. Mbinu moja wapo ya shetani, pale
aliposhindwa kumpata Yesu ili ajifurahishe mwenyewe na kuyabadili mawe yawe
mkate, ilikuwa ni kumshawishi Yesu zaidi ya njia nyingine. Kwa kuwa Yesu
alikuwa akiishi kwa neno la Mungu, shetani angejaribu kutumia hilo ili
kumpeleka Yesu katika kiburi. Shetani alimpandisha Yesu juu ya hekalu, akanukuu
maandiko kutoka katika kitabu cha Zaburi kuhusu malaika wakimwangalia Yesu ili
kwamba asiweze kudhurika. Na tena akasema ikiwa yeye ni mwana wa Mungu basi
ajidhihirishe kwa kuruka kutoka juu ya hekalu! Yesu hakufanya hivyo, akanukuu
maandiko “usimjaribu bwana Mungu wako”, Kumb. 6:16. Katika majaribu hayo
tunaona kwamba shetani ananukuu maandiko lakini anafanya hivyo ili tu aweze
kumpata Yesu ili afanyemambo kipekee pasipo Mungu. Yesu hakuhitaji kufanya
mbinu maalum kwa ajili ya shetani ili kuhakikisha kuwa yeye ni mwana wa
Mungu.Yesu anaishi tu katika kumtukuza na kumpendeza Baba yake!
Lakini hivyo
ndivyo ambavyo shetani atajaribu kututendea kutujaza akili zetu na mambo ya
hakika yaliyo na ukweli fulani wa kimaanddiko, lakini yote hayo ni ili
kutufanya tuende mbali zaidi na yale ambayo Mungu ametuamuru ili atusababishie
maumivu au hasara kwa namna fulani. Hivyo watu wanaweza kufikiri, “sawa, sisi
ni wana wa Mungu naye ametupatia uwezo kumshinda shetani! Basi hebu tuombe
dhidi yake na kuzifunga nguvu zake!” Lakini mtazamo wa aina hii sio wa
kibiblia. Ni majivuno. Na inaenda mbali zaidi ya yale ambayo Mungu ametuagiza
kuliko kumshinda shetani, inalenga uangalifu wetu tuutupie kwa shetani na hivyo
kutufanya tumtukuze yeye na kumhesabia yeye kuwa ni maarufu na mwenye uwezo
kuliko ile aliyonayo kwa hakika au inayompasa! Hii kwa kweli inapora utukufu wa
Mungu na uweza wake katikati yetu! Bwana Yesu alisema kuwa – walipo wawili au
watatu wamekusanyika pamoja kwa jina langu; yeye atakuwa katikati yao. Hakusema
kuwa – pale wawili au watatu wamekusanyika pamoja kwa jina lake, shetani
atakuwa hapo na kwa hiyo kanisa litahitajika kuomba na kuzifunga na kukemea
roho chafu kutoka katika kusanyiko lao! Lakini ikiwa tutafanya aina hii ya
mambo nje ya aina fulani za desturi zetu tulizo nazo, hapo tutakuwa
tukidhirisha kutokuamini katika Mungu na katika neno lake na tutakuwa
tunamwabudu shetani kwa yale matendo ya ushirikina ambayo tunayaita ni vita vya
kiroho! Ninalifahamu kanisa fulani katika mji ninaoishi, ambako mchungaji wa
hapo aliwachukua watu ili kuombea jengo lote la kanisa – kuzifukuza roho chafu
ambazo alisema ndizo zilizokuwa zinaishi katika jingo lile na zinapinga kazi ya
Mungu sehemu hiyo! Jambo hili ni aina ya kutokuamini na ushirikina, tunaweza
kutumbukia humo kwa mafundisho haya ya kisasa!
Vita vya kiroho
inatuhusisha kusimama huku tukiwa tumeshika silaha ya imani katika Mungu pamoja
na neno lake kinyume na uongo wote, mashutumu na majaribu ya shetani. Hiyo
ndiyo inayoelezwa katika Efeso 6 yote. Haihusiki na kuvaa aina fulani ya silaha
za kiroho ili kwamba tuweze kupigana mieleka moja kwa moja na aina fulani ya
roho chafu au ya kieneo, tukipiga kelele na kukemea katika maombi. Kuhusiana na
kupiga kelele na kukasirika kwa ajili ya shetani, ambayo imeenea sana kwa
baadhi ya watu siku hizi, yapo maandiko fulani ambayo yanatuelekeza vizuri.
Tumekwisha kuona tayari jinsi Yesu alivyoweza kumkabili shetani kule Nyikani.
Hakuweza kupata joto na kukasirika kuhusiana na Ibiilisi, ampigie makelele kana
kwamba hapaswi kuwepo pale. Pengine tunaona kushangazwa jinsi ambavyo Mungu
alivyomwelezea yule shetani kule katika sura ya kwanza na ya pili ya kitabu cha
Ayubu. Mungu anamruhusu Shetani aseme maneno yake na anaruhusu mabishano yake
na matendo yake – lakini tu ni kulingana na kusudi lake mwenyewe. Mungu yu
salama na mwenye uhakika katika haki yake ya umilele. Yeye anatawala katika
haki, na kila mmoja kule mwishoni atahukumia kwa haki ya Mungu. Yeye pia ni
mwenye mamlaka juu ya mambo ya wanadamu na yeye anayemruhusu shetani kuwajaribu
watakatifu wake. Mungu hachanganyikiwi kuhusu shetani – hukumu yake ya mwisho
ni yenye uhakika. Shetani anatupwa katika ziwa la moto. Mpaka hapo, shetani
anachofanya ni kuzunguka huku na kule kama Simba angurumaye, naye anatafuta
kunyang’anya, kuua na kuangamiza. Bado anawadanganya watu na kupinga kazi ya
Mungu. Kwa wale wanao mwamini Krsito, nguvu za shetani zimevunjwa naye hana
uwezo dhidi yao, ingawaje kama tulivyokwisha kuona. Mungu anamruhusu shetani
hatua fulani, lakini yote hiyo ni kwa ajili ya kuwajaribu watu wake ili kwamba
imani yao ipate kuwa kama dhahabu! Lakini katika mfano wa hapo juu si Kristo
hapa duniani wala Mungu kule mbinguni aliyechemka kwa kumkaripia shetani.
Amepewa nafasi na fursa kulingana na hekima yake Mungu mwenyewe na mamlaka
zake, lakini kazi za shetani pia hukemewa na kuvunjwa pale anapoingilia kazi ya
Mungu ya kuokoa roho kama tulivyokwisha kuona katika Matendo ya Mitume. Sasa ni
Yuda anayeandika katika Agano Jipya anatupatia neno la kutuonya kuhusiana na
jambo hili. Yuda 1:8-10. Hapa anatuambia kuwa hata malaika mkuu Mikaeli hakutoa
mashutumu ya kukemea dhid ya shetani. Sisemi hapa kuwa shetani anayo nafasi
maalumu na uwezo ambao yatupasa sisi kuogopa. Hapana! Hapana kabisa! Aliye
ndani yetu ni mkuu kuliko yeye aliye nje ulimwenguni.
Lakini ninapenda
tuone maandiko yanavyotufunulia kuhusiana na jambo hili na yanavyofundisha.
Lengo langu katika kusema haya yote ni kuona kuwa, hatumpatii shetani nafasi
kubwa na uwezo katika kufikiri kwetu na ndani ya maombi yetu kwa kumhesabia
umaarufu ambao hastahili kuwa nao; au kwa kwenda mbali na maandiko kwa kujaribu
kupigana naye na kumkemea au kupambana na roho zitawalazo maeneo (roho za
kimaeneo) kama zinavyoitwa! Yuda hapa anaongelea kuhusu watu wanaoongea uovu
juu ya mambo wasiyo yajua au wasiyoyaelewa. Na hivyo ndivyo sawa sawa na hawa
waandishi wa kisasa na walimu wa kisasa wanavyofanya. Bila shaka roho chafu ni
ushetani. Lakini sasa hawa waandishi wa kisasa wanaongea mambo kuhusu hao
pasipo kuelewa wanasema nini hasa! Wanatutaka tukazie macho yetu kwa shetani na
roho chafu, tukiwapatia uwezo na mamlaka juu ya miji ambayo kwa kulingana na
maandiko hawanavyo! Kisha wanatutaka tujihusishe katika mapambano binafsi ya
kirogho pamoja na maroho hayo na kukemea dhidi yao katika maombi! Mambo hayo
yote yanaenda mbali zaidi na maandiko na pia yanaenda mbali zaidi na yale yote
ambayo Mungu ametuagiza.
Sipendi
nikupatie kanuni ya jinsi ya kuomba au kutokuomba katika mazingira maalum
ambayo utakabiliana nayo mbali ya kuelekeza maandiko halisi na ukweli wa kiroho
ambao unapaswa kutulinda katika kuomba kwetu. Pia sisemi kwamba hatuwezi kupiga
kelele au kuomba kwa sauti kuu inapohatijika tunapofanya maombezi – inategemea
na aina ya maombi. Ninaloandika ninaliandika juu ya kujaribiwa kwetu tupige
kelele kwa hasira dhidi ya Shetani kupita kiasi na bila kujali mafundisho ya
Biblia na mfano wa Yesu Kristo. Tunaweza kuhakikishiwa kuwa Kristo
aliziangamiza kazi zote za shetani juu ya msalaba na kuharibu mamlaka na uweza
pale msalabani. Hii inaweza kutufariji tunapoomba kwa Mungu kuhusu mazingira
ambayo tunaamini kuwa shetani anapinga kazi ya Mungu, lakini pasipo
kujishughulisha na mambo hayo yao yasiyo ya kibiblia ambayo yanahamasishwa na
waandishi hawa wa kisasa!
Nimewahi
kuwasikia, watu wakisema miaka mingi sasa, “namchukia shetani” hasa kama mtu
ametenda dhambi vibaya au ameumia vibaya. Haya, haikusaidia chochote kumchukia
shetani kwa ujumla haitoshi na wala sio hoja yenyewe. Hoja hapa ni kwamba iwapo
mtu atajikana mwenyewe na kumpenda pamoja na kumtii Mungu. Ile kinachoweza
kutusaidia zaidi katika maisha yetu kiroho ni iwapo tunazichukia dhambi na
kuipenda haki (Heb 1:9), ikiwa tunamwamini na kumtii Mungu. Tunapaswa kumpinga
shetani kwa moyo wetu wote na wala tusikubaliane na mashauri yake ya
udanganyifu au matoleo yake ya kujaribu watu. Hii ndiyo njia kuelekea kwenye
furaha, amani, na haki. Kutoka katika maandiko ningeweza kusema kuwa, ni jambo
jema sana kutokujihusisha mwenyewe na hisia zozote zile kuelekea kwa shetani.
Yesu kule nyikani hakupenyeza uso wake mbele kwa hasira yenye dharau na kuanza
kumkemea shetani, akirusha ngumi yake hewani! Je tunapaswa kufanya hivyo?
Lakini tunaona kuwa shetani hakuwa na uwezo wowowte juu yake, na Yesu alirudi
toka nyikani akiwa amejaa nguvu za Roho – baada ya kuwa amepinga vishawishi vya
shetani. Ikiwa unapenda kuchukia kitu chochte hapa duniani, basi uichukie
dhambi na katika hali ya kuwa hupendi kufanya lolote lile navyo. Na kama
tunawaona wengine wanatenda dhambi, basi hebu tumwombe Mungu ambaye ni tajiri
wa rehema na neema 1Yoh 5:16. Hebu tumfuate Yesu ambaye alipenda haki na
akachukia maasi (Ebr.1:9) ambaye alipinga na kukataa vishawishi vya shetani
pasipo kukemea juu yake kwa hasira, na ambaye kama kuhani mkuu huchukua majina
yetu mara kwa mara kifuani pake mbele za Mungu katika maombi! Kut 28:12, 29,
Heb 7:25. Nasi tuzifuate nyayo zake, Efs. 6:18.
0 Comments