Posts

Showing posts from April, 2017

UNAPOHITAJI MFANIKIO TAFADHARI ACHANA NA MAMBO HAYA HARAKA SANA.

Image
1. Acha kutegemea mafanikio ya haraka.Mara nyingi hizi ndizo zimekuwa ndoto nyingi za watu wengi kutaka kuona mafanikio makubwa na ya haraka. Mafanikio yoyote huwa yanajengwa hatua kwa hatua. Tena kuna wakati huwa ni hatua za kutambaa mithili ya mtoto mdogo. Kama utategemea mafanikio ya haraka zaidi katika maisha yako hutayapata zaidi ya kujidanganya wewe mwenyewe. Acha kung’angania mafanikio ya haraka, utakwama. Jiwekee malengo kisha songa mbele. SOMA; Jinsi Ya Kuweka Malengo Utakayoyafikia. 2. Acha kuwa mtu wa visingizio.Hili ni jabo mojawapo ambalo umekuwa ukiling’ang’ania mara kwa mara katika maisha yako. Umekuwa ni mtu wa visingizio kwa kudai kuwa huwezi kufanikiwa kwa sababu hukusoma, huna mtaji ama umetoka katika familia maskini. Kutokana na visingizio hivyo umekuwa huchukui hatua yoyote zaidi ya kuzidi kufanya maisha yako kuwa magumu. Ili uweze kufanikiwa, achana na kung’ang’ania visingizio kama mkombozi wako. Badala yake, chukua hatua juu ya maisha yako. S...

SOMO: WOKOVU MKUU

Image
  WARUMI 5 –8 UTANGULIZI •Kwakuwa Mungu ametumia gharama kubwa kuleta wokovu duniani, katika huo, imeachiliwa nguvu inayo weza kuleta faida kubwa katika maisha ya mwanadamu •Ili tuweze kupokea faida   inayo ambatana na wokovu, lazima tuujali na kuuishi katika wokovu halisi katika maisha yetu. •Itakuwa rahisi kwetu kuujali wokovu kama tutatambua gharama iliyotumika kuleta wokovu MAANA YA WOKOVU 1.      WOKOVU NI ZAWADI YA MUNGU KWA WAMINIO Tofauti na mshahara (dhawabu) ambayo hutolewa kulingana na kazi ya mtu na kwa makubaliano, zawadi hutolewa kwa mtu kulingana na furaha ya yule anayetoa na sio kwa kazi ya yule anayepokea. Wokovu ni zawadi ya Mungu inayotokana na furaha yake kwetu tunapomwamini yeye, na Yesu kristo aliyemtuma. Kama ingetokana na kazi hakuna mtu angeyeweza kufanya kazi ya kustahili ijara inayolingana na thamani ya wokovu. Hivyo Wokovu si matokeo ya matendo mema, kusali, kufunga wala kutoa sadaka nyingi bali ni m...