WARUMI
5 –8
UTANGULIZI
•Kwakuwa
Mungu ametumia gharama kubwa kuleta wokovu duniani, katika huo, imeachiliwa nguvu
inayo weza kuleta faida kubwa katika maisha ya mwanadamu
•Ili
tuweze kupokea faida inayo ambatana na wokovu,
lazima tuujali na kuuishi katika wokovu halisi katika maisha yetu.
•Itakuwa
rahisi kwetu kuujali wokovu kama tutatambua gharama iliyotumika kuleta wokovu
MAANA YA WOKOVU
1.
WOKOVU NI ZAWADI YA
MUNGU KWA WAMINIO
Tofauti
na mshahara (dhawabu) ambayo hutolewa kulingana na kazi ya mtu na kwa
makubaliano, zawadi hutolewa kwa mtu kulingana na furaha ya yule anayetoa na
sio kwa kazi ya yule anayepokea. Wokovu ni zawadi ya Mungu inayotokana na
furaha yake kwetu tunapomwamini yeye, na Yesu kristo aliyemtuma. Kama
ingetokana na kazi hakuna mtu angeyeweza kufanya kazi ya kustahili ijara inayolingana
na thamani ya wokovu. Hivyo Wokovu si matokeo ya matendo mema, kusali, kufunga
wala kutoa sadaka nyingi bali ni matokeo ya kuukubali upendo wa Mungu kwetu na
kuiamini kazi ya Yesu Kristo msalabani.
Kwa
maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi
zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije
akajisifu(Efe 2:8-9).
2.
Wokovu ni badiliko
la kudumu la mtu wa ndani
Neno
la kiingereza lilotumika ni “trans-formation”maana yake ni mabadiliko
yasiyoweza kurudia hali yake ya kwanza. Ni mfano wa kuchoma karatasi na kupata
majivu ambayo hayawezi kuwa tena karatasi na sio mfano wa maji yanayoganda kuwa
barafu na baadaye kuyeyeuka tena kuwa maji. Mtu aliyepata wokovu halisi na
kuonja wema wa Mungu hapaswi kuwa na kigeugeu wala ndoto ya kurudi nyuma.
Wala
msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu,
mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu(Rum
12:2).
3.
Wokovu ni kuhamishwa
Kabla ya kuokoka ulikuwa unaendeshwa na ufalme wa giza kwa kumtii shetani na matakwa ya nafsi na mwili. Kuokoka ni kukubali KUENDESHWA na Neno la Mungu. Maanake ni kuishi kwa kukataa matakwa yako na kufuata matakwa ya Mungu. Kumtii Mungu kunakoambatana na kukana matakwa ya adui apitiaye nafsi na miili yetu tutafunga mlango wa kuonewa na ibilisi na kufungulia baraka za Mungu(Yak 4:7). Kwa hakika wokovu unatutoa kutoka mahali pabaya na kutuweka katika ulimwengu salama ndani ya Kristo Yesu katika Ulimwengu wa roho
Naye
alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme
wa Mwana wa pendo lake (Kol 1:13)
4.
Wokovu ni
kukombolewa
Wakati
mwingi tumesita kutumia neno “ukombozi”kwa sababu ya matumizi mabaya
yaliyozoeleka hivi sasa. Lakini ni moja ya neno kuu sana katika wokovu wetu.
Neno “ukombozi”limetukaje vibaya?
(A).Kwa
kutumia Neno kukombolewa kama njia ya kutoka kwenye magonjwa na shida mbali
mbali.
(B).Kwa
kudai sadaka au tendo fulani kama vile kufunga kama njia ya kuleta ukombozi
Matumizi sahihi ya neno “kukombolewa”ni
yapi?
(a)
Ni kibali cha kutolewa kwenye hukumu ya Mungu. Neno sahihi kwa habari ya
kutolewa kwenye magonjwa na shida/madhaifu mengine ni kuponywa.
(b)
Ni tendo linatokana na sadaka pekee na moja tu ya mauti ya Kristo na kumwagika
kwa damu yake msalabani.
Je, kuna tofauti gani kati ya
wokovu na ukombozi?
Wokovu
ni matokeo ya ukombozi kamili. Baada tu ya mwanadamu kuanguka pale Edeni pale
pale iliandikwa hati ya mashitaka kwa wanadamu wote mbele za Mungu na nakala (copy/kivuli)
zikatumwa duniani. Naye shetani akazichukua kama ushahidi kwamba hakuna
mwanadamu atakayekwenda Mbinguni, Na hiyo ndiyo ilkuwa hukumu, yaani kutengwa
na Mungu(mauti ya milele).Watakatifu wa zamani walipolala walizuiwa kuingia
Mbinguni kwa sababu ile hati.Walisubiri ukombozi wao wakiwa kifuani kwa
Ibrahimu (Ebr 11:13). Hata baada ya kufufuka kwao walisubiria siku tatu hapa
hadi hati ilipofutwa (Mt 27:52-53)
Je, kuna tofauti gani kati ya
wokovu na ukombozi?
Kwa
muda wote huo alikuwa natafutwa mtu ambaye angeweza kuingia maeneo yote matatu
ili kuzifuta hati zote za mashitaka. Ndio maana baada tu ya Bwana Yesu kumwaga
damu yake alienda nayo patakatifu pa hapa duniani(kitambaa cha hekalu
kilipasuka) ili kufuta nakala ya hati ya mashitaka, kisha akaenda kuzimu nako
akabatilisha ushahidi uliokuwemo na hatimaye akaenda hadi Mbinguni ilimokuwa
hati halisi akaifuta kwa damu yake, kisha akaandika hati nyingine pale pale ya
kutangaza ukombozi kwa wanadamu wote tangu Adamu (Ebr 9:22-24, Kol 2:14-15, 1Pet 18-19, Ufu
5:1-10). Haya yatufanye kujua kwamba wokovu tuliopewa ni mkuu sana (Ebr 2:3)
Wokovu ni ukombozi
Kwa
hiyo ukombozi ni kitendo cha kufutwa kwa hati ya uadui kati ya Mungu na
mwanadamu na kuandikwa kwa hati ya kukubaliwa na Mungu. Wokovu ni kitendo cha
kukubali/kupokea ukombozi wa Yesu kristo katika maisha ya mtu binafsi. Kitendo
cha Yesu kufa msalabani na kufuta hati ya mashitaka na nakala zake kilitangaza
majira ya ukombozi kwa wanadamu wote, na kutoa nafasi kwa kila mtu kuokoka. Kinachopaswa
ni kusaini hati hiyo kwa kumwamini Yesu kristo (Lk 4:18-19).
Wokovu ni kukombolewa
Ukombozi
manake ni kulipiwa deni na deni tulilopiwa ni kutolewa kwenye hukumu ya
Mungu(1Pet 1:18-19). Mkataba wa ukombozi ni kwamba baada ya kulipiwa deni
tunakuwa mali ya yule aliyetununua yaani Yesu Kristo na hivyo tunarudi kwa
Mungu na muumba wetu, naam (1Kor 6:19). Kwa njia hiyo, yanarejeshwa mahusiano
yaliyokuwa yamevunjika wakati wa anguko la Edeni
Wokovu
ni mchakato wa MATENGENEZOya
mfumo mpya wa maisha
Ili
tuweze kudumisha wokovu wetu Lazima kilasiku tu elekeze nia zetu katika kuvua matendo
yazamani na kujivika tabia mpya za waenda Mbinguni.Njia yakujithibitisha katika
wokovu ni kuhakikisha kuwa kilasiku, katika maeneo yote ya maisha yako, kuna mabadiliko
endelevu katika mtazamo wako, vipaumbele vyako, usemi, matendo, utoaji, huduma,
ibada, kusomaneno, maombi nk.
Mvue
kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani,unao haribika
kwa kuzifuata tama zenye kudanganya;na mfanywewapya katika roho ya nia zenu;
mkavae utu mpya, ulio umbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wakweli
(Efe4:22-24)
0 Comments