1. Acha kutegemea mafanikio ya haraka.Mara nyingi hizi ndizo
zimekuwa ndoto nyingi za watu wengi kutaka kuona mafanikio makubwa na ya
haraka. Mafanikio yoyote huwa yanajengwa hatua kwa hatua. Tena kuna wakati huwa
ni hatua za kutambaa mithili ya mtoto mdogo. Kama utategemea mafanikio ya
haraka zaidi katika maisha yako hutayapata zaidi ya kujidanganya wewe mwenyewe.
Acha kung’angania mafanikio ya haraka, utakwama. Jiwekee malengo kisha songa
mbele.
SOMA;
Jinsi Ya Kuweka Malengo Utakayoyafikia.
2. Acha kuwa mtu wa visingizio.Hili ni jabo mojawapo ambalo
umekuwa ukiling’ang’ania mara kwa mara katika maisha yako. Umekuwa ni mtu wa
visingizio kwa kudai kuwa huwezi kufanikiwa kwa sababu hukusoma, huna mtaji ama
umetoka katika familia maskini. Kutokana na visingizio hivyo umekuwa huchukui hatua
yoyote zaidi ya kuzidi kufanya maisha yako kuwa magumu. Ili uweze kufanikiwa,
achana na kung’ang’ania visingizio kama mkombozi wako. Badala yake, chukua
hatua juu ya maisha yako.
SOMA;
Mambo 7 Yanayo kufanya Ushindwe Kutimiza Ndoto Zako.
3. Acha kuogopa sana kushindwa.Kushindwa ni hatua mojawapo
muhimu ya kuweza kukufikisha kwenye njia halisi ya mafanikio. Unaposhindwa
unakuwa unajifunza kutokana na makosa unayoyafanya na kisha kuendelea zaidi.
Kama utaendelea kuogopa kujaribu mambo mapya kila siku kwa sababu ya kushindwa,
tambua hutaweza kufanikisha mambo makubwa katika maisha yako. Ili uweze kufikia
mafanikio makubwa hutakiwi kuogopa kushindwa kwa namna yeyote ile. Unatakiwa
kuachana na woga huu mara moja ili kufikia mafanikio makubwa.
SOMA;
Jiulize “Kwa Ni Nini Maisha Yangu Yako Hivi”
4. Acha kufanya kazi kutegemea pesa.Kama utaendelea kufanya
kazi na kuwaza pesa! Pesa Pesa!, hutaweza kufika mbali sana. Fanya kazi kwa
lengo la kujifunza na kisha baada ya hapo pesa ndiyo ifuate. Ukiwa unafanya
kazi kwa lengo la kupata pesa utajikuta unafanya mambo yako mengi sana chini ya
ufanisi. Badili fikra zako na acha kung’ang’ania kufanya kazi kwa kutaka pesa
tu. Ukitengeneza huduma iliyobora zaidi pesa kama pesa itake isitake itakufuata
tu huko ulipo.
SOMA;
FEDHA; Kama Unataka KuwaTajiri, Acha Kufanya Makosa Haya Unapokuwa Na Pesa.
5. Acha kuwa Kufikiria sana makosa yaliyopita.Kwa kuendelea
kufikiri sana makosa uliyoyafanya hiyo itakufanya uzidi kupoteza mwelekeo wa
mafanikio yako. Njia sahihi ya kufanikiwa ni kuachana na kufikiria makosa hayo.
Vinginevyo utakuwa unapoteza nguvu zako nyingi kun’gang’ania jambo ambalo
haliwezi kukufikisha kwenye mafanikio ya kweli. Hili ni jambo mojawapo ambalo
unatakiwa kuliacha mara moja ili uweze kufanikiwa.
Kwa vyovyote vile, kwa kadri unavyozidi kun’gang’ania mambo
hayo ndivyo ambavyo unajikuta unazidi kuharibu maisha yako bila kujua. Ili
kuweza kufanikiwa na kutimiza ndoto zako halisi ulizojiwekea, unatakiwa kushika
wajibu mmoja tu. Huu ni wajibu wa kuweza kun’gang’ania mambo yatakayokusaidia
na kubadili maisha yako kabisa. Kwa kifupi, hayo ndiyo mambo unayotakiwa
kuyaacha mara moaj ili uweze kufanikiwa
0 Comments