Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU. BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu. Karibu tujifunze Neno la MUNGU. Kanisa ni jumuia ya Wakristo. Kanisa ni watu walioitwa na kutengwa na mambo ya dhambi. 1 Kor 6:17-18 '' Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema BWANA, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. Nitakuwa BABA kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,'' Maandiko hayo ni sehemu tu ndogo ya maandiko yanayolitambulisha Kanisa la KRISTO duniani. Kanisa hai wametengwa na uovu wa dhambi na wametengwa na mambo ya kidunia yaliyo machukizo(Machafu). Ndio maana huwezi kumuona Askofu akiwa disko akicheza. Huwezi kumuona Mkristo aliyeokoka akiwa kwa mganga wa kienyeji. Huwezi kumuona Mchungaji anatoa talaka. Huwezi kumuona Mteule wa MUNGU akivuta sigara wala bangi na tena huwezi kumuona mteule wa KRISTO akitumia madawa ya kulevya. Huwezi kuona kanisa wakichukua mapanga na mikuki wakienda kul...
Comments
Post a Comment