Posts

Showing posts from September, 2016
Image
MAOMBI YA KUMUOMBA MUNGU ILI AFANYE JAMBO JIPYA. Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU. BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu. Karibu tujifunze Neno la MUNGU na kisha tuombe maombi ya ushindi sana. Leo tunamuomba MUNGU afanye jambo jipya katika maisha yetu. Kama magonjwa yalitutawala leo MUNGU BABA anafanya jambo jipya kwa kuleta uponya wake. Isaya 43:19 '' Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.''    MUNGU wetu anaenda kufanya jambo jipya, Hata baraka ambazo tuliziona haziwezekani kwetu leo kwa maombi yetu kupitia jina la YESU KRISTO tunaenda kufanikiwa. Kwanini MUNGU afanye jambo jipya? Ni kwa sababu  ''  hakuna neno lisilowezekana kwa MUNGU.-Luka 1:37'' Kwanini JEHOVAJ MUNGU wetu atende jambo jipya? Yeye MUNGU anakuuliza wewe akisema;  '' Tazama, mimi ni BWANA, MUNGU wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisilol...

MAOMBI YA KUMILIKI MILANGO YA BARAKA ALIYOKUWA AMEISHIKILIA ADUI.

Image
Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU. BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu. Karibu tujifunze kisha tuombe maombi ya ushindi mkuu.   Isaya 60:11 ''   Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; Hayatafungwa mchana wala usiku; Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.'' Katika ulimwengu wa roho baraka zako zote huwa ziko katika maeneo ambapo ili upate baraka yako uitakayo unatakiwa kubisha kwenye ulimwengu wa roho wa nuru ili ufunguliwe na kuchukua baraka yako, ndio maana katika maombi imani ni jambo la muhimu sana. Kuna baraka nyingi sana ambazo unazihitaji katika maisha yako. Kuwa na afya njema ni baraka, kuna na mchumba kisha ndoa ni baraka, kufaulu masomo ni baraka, kuwa na ufahamu mzuri ni baraka, kumiliki nyumba au kiwanja ni baraka, kupata kazi nzuri ni baraka , Kununua gari ni baraka, kupandishwa cheo kazini ni baraka na hata kuwa na uchumi mzuri ni baraka, N.k maana baraka ...

VIJANA KATIKA HARAKATI ZA KUPATA WACHUMBA

Image
VIJANA KATIKA HARAKATI ZA KUPATA WACHUMBA.  Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU. VIJANA KATIKA HARAKATI ZA KUPATA WACHUMBA. BWANA YESU atukuzwe sana. Karibu tujifunze Neno la MUNGU aliye hai. Mithali 31:10A ''   Mke mwema, ni nani awezaye kumwona?'' Mwanaume anayetarajia kuingia katika uchumba anaweza kujiuliza kwamba ''Mke mwema nitamjuaje?'' Mwanamke anayetarajia kuingia katika uchumba naye anaweza kujiuliza '' Mume mwema nitamjuaje?''  Huwa kuna maswali mengi sana katika kumjua mwanamke anayefaa kuwa mke. Huwa kuna maswali mengi sana katika kumjua mwanaume anayefaa kuwa mume. Leo sikuchagulii mtu anayetakiwa kuwa mchumba wako ila kazi yangu ni kukufundisha wewe unayetarajia kuingia katika uchumba au una mchumba kisha unatarajia kuingia katika ndoa.  Binti au kijana unatakiwa uwe msafi kiroho na kimwili wakati wote, hiyo itakusaidia Kuolewa au kuoa mapema na katika usahihi. Kijana au Binti naomba u...

HII NAYO YA MUHIMU SANA KWA YULE UNAYEJIANDAA KUWA MME/MKE WAKE!

Image
HII NAYO YA MUHIMU SANA KWA YULE UNAYEJIANDAA KUWA MME/MKE WAKE! Na Mwl  Dickson Kabigumila Luka 1:5 inasema kitu kuhusu Kuhani Zekaria, na Mke wake Elisabeth...na kuna mambo kadhaa ya kujifunza; 1.Zekaria alikuwa kuhani, lakini Elizabeth alikuwa wa Kabila la Lawi Hii inaonesha wazi ya kuwa, hawa watu [Zekaria na Elizabeth] walikuwa watu wanaoishi kwenye SAME PURPOSE...Zekaria alikuwa Kuhani, aliyetumika madhabahuni, na ili huduma yake na wito wake na kusudi la Mungu kwake litimie, alihakikisha anampata mtu ALIYEKO KWENYE SAME DIRECTION na yeye, ndio maana Elizabeth alitokea kabila ya Lawi; Kabila ambalo Mungu alilitenga lote liwe linatoa makuhani na watu wa madhabahuni...ili iwe rahisi kwa Zekaria kutumika vema kwenye KUSUDI LA MUNGU ilibidi awe na mtu mwenye maono kama yake! [NINYI WAKAKA NA WADADA MNAOPENDA KUANGALIA PHYSICAL MATERIALS, BADALA YA SPIRITUAL CONTENTS MTAKUJA KULIA KARIBUNI]...Mke ni Msaidizi wako katika kulitimiza kusudi la Mungu...Ataitwaje mke, waka...

KAMA UMEZALIWA, UNATAKIWA KUKUA

Image
KAMA UMEZALIWA, UNATAKIWA KUKUA Na Mwl Nickson Mabena Bwana Yesu asifiwe, karibu kwenye mada inayosema JINSI YA KUUKULIA WOKOVU,  Hapa nitakushirikisha kidogo, vitu vichache vitakavyokusaidia kufanya tathimini ya UKUAJI WAKO!.  Kicha cha ujumbe, nimekwambia KAMA UMEZALIWA, UNATAKIWA KUKUA!.  Biblia inatufundishwa kwamba, Mwanadamu baada ya Kuzaliwa mara ya kwanza, anatakiwa kuzaliwa mara ya pili,  "Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu" YOHANA 3:3 " *Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho*". YOHANA 3:6,  Roho ndiye anaizaa roho yako kwa NENO la Kweli,  Ile siku unaokoka,  Kama hujaokoka, maana yake, umezaliwa na MWILI, bado unatakiwa kuzaliwa tena mara ya pili,  Ndio maana kuokoka ni LAZIMA,  Ndio Maana Kuokoka sio Dhehebu,  Ndio Maana hauokoki kwa sababu umerithi kwa Wazazi,  KUOKOKA NI KUZALIWA MARA YA PILI,  Angali...

MAMBO YA KUFANYA ILI FIKRA ZAKO ZITUMIKE KUFANIKISHA MAISHA YAKO_

Image
Na Mwl Christopher Mwakasege. *Lengo la Somo:* _Kutambua maarifa ya kutumia fikra zako kupata Mafanikio maishani._ *MSINGI WA SOMO.* Mithari 23:7a *_Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo._* *Omba MUNGU akusaidie uweze kupata kutoka kwenye vitabu maarifa unayoyahitaji ili uhitajike.* Danieli 12:4 4" Lakini wewe, Ee Danieli, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka. 1. Ni vyepesi mtu kuhitajika akiwa ana maarifa yanayohitajika katika kipindi husika.  Danieli 1:17~21 17' Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Danieli naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto.18' Hata mwisho wa siku zile alizoziagiza mfalme za kuwaingiza, mkuu wa matowashi akawaingiza mbele ya mfalme Nebukadreza. 19' Naye mfalme akazungumza nao; na miongoni mwao wote hawakuonekana waliokuwa kama Danieli, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria; kwa hiyo wa...

UTUMIE UJANA WAKO VIZURI

Image
UTUMIE UJANA WAKO VIZURI Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU. BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu. Karibu tujifunze Neno hai la MUNGU. Ujana ni Umri kuanzia miaka 18 hadi miaka 45.  Ni muhimu sana kuutumia ujana wako vizuri na njia muhimu sana ya kuutumia ujana wako vizuri ni kumcha MUNGU wakati wa ujana. Kama kuna ujana basi na kuna uzee pia hivyo Utumie Ujana Wako Vizuri. Yohana 21:18 ''   Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka.''  Andiko hili linaonyesha jambo fulani kuhusu ujana na kuhusu uzee pia, kuna  madhara ya kuutumia ujana vibaya maana katika uzee unaweza kukosa mwelekeo mzuri. Ukiwa kijana unakuwa na nguvu za kwenda popote na kufanya chochote lakini ukiwa mzee utategemea zaidi matokeo ya kile ulichokifanya katika ujana wako. Kama ujana wako uliutumia vizuri kwa MUNGU h...