AINA/HATUA TATU ZA MAJARIBU UTAKAYOKUTANA NAYO KATIKA MAISHA. MATHAYO 4:1-11..
AINA/HATUA
TATU ZA MAJARIBU UTAKAYOKUTANA NAYO KATIKA MAISHA. MATHAYO 4:1-11..
."Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani,ili
ajaribiwe na IBILISI.Akafunga siku arobaini mchana na usiku,mwisho akaona
njaa.Mjaribu akamjia akamwambia,Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu,amuru kwamba mawe
haya yawe mkate.Naye akajibu akasema,Imeandikw,Mtu hataishi kwa mkate tu, ila
kwa kila neno litokalo kinywani mwa Mungu.Kisha ibilisi akamchukua mpaka mji
mtakatifu ,akamweka juu ya kinara cha hekalu,akamwambia,Ukiwa ndiwe Mwana wa
Mungu jitupe chini; maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake;Na mikononi mwao
watakuchukua;Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.Yesu akamwambia,Tena
imeandikwa,Usimjaribu Bwana Mungu wako.Kisha ibilisi akamchukua mpaka mlima
mrefu mno,akamwonyesha milki zote za ulimwengu,na fahari yake,akamwambia, Haya
yote nitakupa,ukianguka kunisujudia.Ndipo Yesu alipomwambia,Nenda
zako,shetani;kwa maana imeandikwa,Msujudie Bwana Mungu wako,umwabudu yeye peke
yake.Kisha ibilisi akamwacha;na tazama,wakaja malaika wakamtumikia. Ndugu zangu ni vema mkajua kuwa,kabla shetani hajakuacha
uendelee na maisha yako kuikaribia ndoto na hatima ya maisha yako,uwe na
uhakika kwanza atakujaribu katika hatua hizi tatu..Ikiwa unapitia katika jaribu
fulani wakati huu,chunguza lipo katika kundi lipi kati ya haya kisha utambue ni
majaribu ya kundi lipi kati haya yamesalia ili uje wakati wa kuachwa na shetani
ijapokuwa yaweza kuwa kwa muda tu. Umewahi kujiuliza ni kwanini kuna jaribu ni
rahisi kulishinda kwa kutumia neno la Mungu na lingine linaonyesha kana kwamba
lina asili ya neno la Mungu na kila wakati unapotumia neno kupambana nalo
kunakuwepo hali ya mgongano baina ya neno moja na lingine na unabaki kwenye
mkanganyo.Kuna ahadi moja inagongana na nyingine,wazo moja linagongana na
lingine,neno linagongana na lingine,ufunuo mmoja unagongana na mwingine..ghafla
unajikuta ni vigumu kulishinda jaribu hilo kwa kutumia mstari wabiblia. YESU
alijikuta katika mazingira ambayo alilazimika kukabiliana na majaribu ya aina
tatu katika mazingira yale yale na kwa hakika haikuwa kazi rahisi kama wengi
wetu tunavyozani.Shetanj,katika kumjaribu mtu,huleta majaribu katika hatua
zifuatazo;
Hatua ya kwanza, JARIBU KWA MUJIBU WA TAMAA YA MTU.
Hii ni hatua ya awali kabisa ya majaribu.Ni aina za
majaribu ambayo huwapata watu ambao ni wachanga bado katika imani.Ni majaribu
ambayo shetani huyatumia kupima umakini wetu juu ya imani na neno la
Mungu.Kabla ya majaribu mengi yote shetani huanza na ya asili hii.Yesu alikuwa
pia mtahiniwa katika hili(MATHAYO 4:2-4).. ...mjaribu anamwambia,UKIWA NDIYE
MWANA WA MUNGU....GEUZA JIWE KUWA MKATE... Mstari wa pili unasema ....akafunga
siku arobaini...MWISHO AKAONA NJAA..
Kulikuwa na
uhusiano wa karibu kati ya TAMAA ya Yesu na kile ambacho shetani alimjaribu
kwacho yaani njaa.Majaribu haya,shetani huwa anajaribu kuitambua
"status" yako kisha kuitumia kukupa ushauri wa kutimiza haja
yako.Majaribu haya huwa yanakuwa na namna hii; "Nakujua wewe ni nani
lakini pia naijua shida yako" ...Nakujua wewe ni mwana wa Mungu lakini
najua pia unanjaa;Nakujua wewe ni mwana wa Mungu lakini najua unashida ya pesa;
Nakujua wewe ni mwana wa Mungu lakini huna na unahitaji mke au mume;Nakujua
wewe ni mwana wa Mungu lakini unahitaji kazi,nk... Ni majaribu ambayo shida
yako inakinzana na identity yako..unajikuta katika mazingira ambayo utii wako
juu ya uovu ndio njia pekee ya kutatua tatizo lako ama unashurutishwa kuitumia
karama na kipawa alichokupa Mungu kutimiza matakwa yako. Majaribu jinsi hii ni
ngumu sana kushinda kwa kutumia utashi na hekima ya kawaida isipokuwa neno la
Mungu.Ukikumbuka tu neno sahihi kwa wakati huo unaweza kulikabili jaribu la
jinsi hii;Ndio maana awali nilisema kuwa shetani huyatumia majaribu ya aina hii
kupima tu umakini wetu juu ya neno la Mungu.Yesu alikabili kwa jibu fupi
tu..."IMEANDIKWA....MTU HATAISHI KWA MKATE"... aliposhinda hili kwa
neno la Mungu,shetani akamjia na hatua ya pili ya jaribu akiwa na vifungu vya
biblia. Hatua ya pili,
JARIBU KWA
MUJIBU WA NENO LA MUNGU.
Pindi anapoona umakini wako juu ya neno kwa
majaribu ya aina hiyo ya awali,shetani huchukua biblia na kuanza kuunda jaribu
kwa mujibu wa maandiko.Majaribu ya jinsi hii huwapata watu ambao kwa sehemu
wamefanikiwa kuzikabiri tamaa zao kwa ajili ya Kristo.Watu wenye mitazamo ya
"kwa ajili ya Yesu nipo tayari kwa lolote" ama "ni heri nife
lakini niingie mbinguni" ama "hata nikiwa maskini,mgonjwa,njaa au
nimeshiba,katika dhiki na taabu,katika mauti au uzima;Yesu ni yeye yule Jana
Leo na milele".Ndugu yangu,kama umefikia hatua ya imani(ya kujikana
kwaajili ya Bwana) basi we ni mtahiniwa wa majaribu ya jinsi hii. Ni majaribu
ambayo Shetanj naye anakuja na mistari ya biblia kukabiliana na ile uliyonayo
moyoni ikupayo imani kwa Mungu..Yesu alikuwa mtahiniwa katika hili(MATHAYO
4:5-7)..IBILISI AKAMCHUKUA MPAKA MJI MTAKATIFU..JUU YA KINARA CHA
HEKALU....akamwambia UKIWA NDIWE MWANA WA MUNGU......KWA MAANA IMEANDIKWA...
Wakati jaribu la awali likuwa "fanya kwa kuwa unashida", hili la sasa
"fanya kwa sababu imeandikwa". Je! Unaweza kugundua tofauti baina
yake?..hapa Shetani huwa anachana kabisa na swala,la tamaa zako ni kukujia na
maandiko..Majaribu haya yana asili hii... "Ninakujua wewe ni mwana wa
Mungu lakini imeandikwa" ...Ninakujua wewe ni mwana wa Mungu lakini
imeandikwa utakula mema ya nchi,utakuwa kichwa,akuponya magonjwa yako
yote,hakuna tasa katika Israel,mke mwema atoka kwa BWANA;ghafla unajikuta kile
unachokijua kwa habari ya Mungu na hali halisi vinakinzana.Kila unapotumia
mstari
mmoja kulikabili
jaribu shetani anakuletea mstari mwingine unakuondolea uthabiti wa moyo juu ya
ule ulonao.. ...Imeandikwa nitakuwa kichwa na nimefeli,nimeponywa magonjwa na
ninaumwa,nitakula mema ya nchi na nimaskini,Bwana kasema nami kuwa ndiye mke
wangu na amenikataa,nk.... Katika hili Yesu hakutumia mistari ya kujitetea kama
mwanzo ila alimpa shetani tu ukweli kwamba ninajua unanijaribu ili hali unajua
kuwa mimi ni nani hivyo basi nakwambia wewe kama walivyoambiwa
wenzako...USIMJARIBU BWANA MUNGU WAKO..Majaribu haya unaweza kushinda pale tu
utakapopata mstari ambapo unagonga shetani moja kwa moja.Katika haya usiendelee
kulumbana na shetani kuhusu ahadi za Mungu.Mtakesha.
Hatua ya
tatu, JARIBU KWA MUJIBU WA OFA YA SHETANI KWAKO.
Baada ya kushinda
hatua hizo mbili,shetani atakuja kukupa ofa.Hii si kwa habari ya tamaa au neno
linavyosema ila zawadi yake kwako ikiwa utafanya matakwa yake.Haya ni majaribu
yanayowapata watu waliofanikiwa zaidi kiimani,kihuduma,kiuchumi au kimaisha kwa
ujumla.Kimsingi,ni watu wachache sana huwa wanafikia hatua ya kujaribiwa na
majaribu ya namna hii kwa kuwa haya ni maalumu kwa ajili ya '"profit maximazation".
Ni majaribu ambayo huyatumia shetani kuwaondoa watu katika kusudi la Mungu
katika majira ya kulitimiza kusudi.Inahitaji kustahimili mengi kabla ya kufikia
hapa.Katika hili shetani huja na mpango wa kukuinua na kukufanikisha zaidi.Si
kwa sababu ya tamaa yako au neno linavyosema ila tu kukupa zaidi ya pale
ilipofikia.Yesu alikuwa mtahiniwa wa hili(MATHAYO 4:8-10)....IBILISI
AKAMCHUKUA...AKAMWONYESHA MILKI ZOTE ZA ULIMWENGU NA FAHARI
YAKE...akamwambia,HAYA YOTE NITAKUPA...Utagundua kuwa majaribu haya huwapata
watu ambao tayari WAMESHATEMBEA na kuona fahari ya mambo mengi. Wakati jaribu
la awali lilikuwa "fanya kwa kuwa unashida", la pili"fanya kwa
sababu imeandikwa",hili la sasa "fanya ili nikupe"..naamini
unaendelea kuona tofauti ya aina/hatua hizi tatu za majaribu.Katika hili,tamaa
zako haziusiki wala neno la Mungu halihusiki.Fanya nikupe ndo habari ya mjini
katika hili.Katika hili shetani kisha jua kuwa wewe ni mwana wa Mungu na hana
haja ya kutaka umthibitishie.Majaribu haya yana asili hii; "Ukifanya hivi
utakuwa zaidi ya ulivyo sasa" ...Ukifanya hivi utaongeza washirika,upako
na miujiza katika huduma yako,ukifanya hivi utaongezewa cheo,biashara yako
itafanikiwa,utakuwa maarufu zaidi...katika hili si kwamba huna kitu ila kuna
ahadi ya kuwa zaidi ya vile ulivyo.Ukishindwa kupambanua roho hii ndo hukawii
kujikuta kuzimu kutafuta upako zaidi au kuwa na miujiza feki au kifanya
biashara za magendo na rushwa,ufisadi na usaliti huzaliwa katika hili pia.
Kulishinda jaribu
hili,ijapokuwa unampaswa bado kuwa na mstari wa kujibu lakini Yesu alichukua
hatua ya ziada ya ...NENDA ZAKO SHETANI...kumfukuza shetani.Hata hivyo majibu
matatu ya Yesu yalikuwa na Siri fulani.
1.Mtu hataishi kwa
mkate...lilikuwa ni jibu juu ya hoja ya haja au uhitaji wa Yesu(njaa).
2.Usimjaribu
Bwana Mungu...lilikuwa ni kumtiisha shetani juu ya mpango wake.
3.Msujudie
Bwana Mungu wako...lilikuwa ni jibu juu ya hoja ya haja au uhitaji wa
shetani(kusujudiwa)
Ikiwa unapitia katika jaribu lolote unaweza kujichunguza
ili kujua ni aina/hatua gani ya jaribu unapitia ili ikusaidie kujua shetani
anatumia hila gani na wewe unaweza kutumia hekima gani ili kushinda.Katika kila
jambo kumbuka kamwe hatujaribiwi kupita uwezo wetu na Mungu ni mwaminifu hata
kufanya mlango wa kutokea..usisahau KUOMBA NA KUMTEGEMEA MUNGU kwani hata
katika maarifa haya niliyokupatia bado neema ya Mungu ni kitu bora zaidi kukupa
wokovu.
Neema ya
Kristo iwe pamoja nawe.Amen
Comments
Post a Comment