Jinsi Ya Kushinda Kukata Tamaa

Halipo jambo moja pekee unaloweza kulifanya sikuzote kwa sababu kama tulivyokwisha kuona, sababu za kukata tamaa hazifanani. Lakini zifuatazo ni baadhi ya hatua unazoweza kuchukua:



-Watambue Wababe Walioko Langoni
 
Wababe wawili wanaolinda lango la kuingilia kwenye nchi ya ahadi hata leo wanaitwa hofu na kukata tamaa. Ikiwa sasa unasikia sauti zao, na kuhisi msukumo wa ushawishi wao, basi ujue kwamba upo karibu sana na ahadi zako.
Katika kipindi hiki muhimu, kama ilivyokuwa kwa Yoshua, unapaswa kuwa hodari na moyo wa ushujaa na kusonga mbele katika neema anayokupa Mungu (Yos 1:9).

Elewa Kinachoendelea
 
Katika 2Kor 4:16,17 Paulo anasema tusilegee kwa sababu kwa kupitia dhiki yetu utu wetu wa ndani unafanywa upya. Anasema dhiki yetu nyepesi na iliyo ya muda mfupi tu, inatufanyia kitu chema katika Mungu.
Tumaini Kwa Mungu 

Hata kama imani yako ni ndogo, bado unaweza kumtumaini Mungu na kuamini kwamba Mungu wa amani atamseta Shetani mara chini ya miguu yako (Zab 42:5) (Rum 16:20).

Kiri Hitaji Lako, Mshirikishe Mwenzako Kisha Mwombe
 
Katika Mhu 4:12 tunaona kwamba uwezo wa watu wawili ni mkubwa kuliko wa mtu mmoja. Usihifadhi tu mawazo yako, mshirikishe mwenzako na halafu mwombe pamoja, na kumfunga Shetani.

Pokea Kutoka Kwa Mungu
 
Fungua moyo wako na umwachie Roho Mtakatifu akuhudumie kwa habari ya saburi na faraja ya Mungu, tumaini, furaha na amani (Rum 15:5, 13).

Shughulikia Sababu Za Asili
Wakati Eliya alipokuwa amechoka na kukata tamaa, Mungu alimpelekea chakula na pumziko kabla hajashughulika na sababu zenyewe na kumpa neno jipya, mwelekeo mpya, na tumaini jipya (1Fal 19:3-18).

Simama Kwenye Ahadi Ya Mungu
Petro anatuasa kuwa wanyenyekevu chini ya mkono wenye nguvu wa Mungu, kumtwika Yeye fadhaa zetu, kuwa na kiasi, kumpinga Shetani na kuwasaidia wengine wanaoteseka. Anatupa tumaini kubwa kwa kusema kwamba Mungu wa neema yote atatujia mara ili kututengeneza, kututhibitisha na kututia nguvu (1Pet 5:6-11). 

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina

Post a Comment

0 Comments