Kesheni, mwombe, msije mkaingia MAJARIBUNI



MATHAYO 26;41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia MAJARIBUNI.roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

Unaweza Ukaomba Mungu  asikuingize majaribuni  nawe ukakwepeshwa ukajikuta hauingii
..Pia unaweza ukaomba ukiwa ndani ya jaribu Mungu akupe mlango wa kutokea na Mungu akakupa mlango nawe  ukatoka humo 1KOR 10:13
Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze  kustahimili..

Pia unaweza ukaomba usiingie au ukaomba Mungu akupe mlango wa kutoka ktk jaribu lakini usipewe badala yake Mungu akaamua kupita na wewe ktk hilo jaribu hadi mwisho

YAKOBO1;1-2 Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali, mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
Hivyo wakati mwingine unapita ktk bonde lenye uvuli wa mauti unatakiwa usiogope maana yeye bado yupo na wewe mnapita wote ktk hayo mateso

.Anao uwezo wa kukukwepesha usiingie ktk hilo jaribu lakini ameamua kupita na wewe ili kukufundisha kitu,na mwisho wake ni ushindi nawe utapewa heshima mmoja wa askari wa Kiroho..Na pia Mungu anaruhusu uingie ili ajipatie utukufu kwa jamii za wanadamu wajue kweli Mungu yupo na anaokoa

..Ndo maana Kina   Meshaki, Shadraka na Abednego  walipotupwa ktk moto hawakuwa peke yao naye akawa ndani ya moto na kuwaokoa mwisho wa siku Mungu akajipatia utukufu kwa mfalme Nebukadreza (DANIELI 3;28) Mungu wao akatukuzwa ktk jamii yote ndiye Mungu  aokoae..

Hata Danieli  alipotupwa ktk  tundu la simba wakali ndani ya tundu la simba Danieli hakuwa peke yake malaika alikuwa naye akamlinda na simba hawakumdhuru..Akatoka salama na Mungu wa Danieli akatukuzwa ktk jamii  YOTE YA DUNIA  kuwa ndiye Mungu aponyaye, aokoaye na kutenda ishara na maajabu..(DANIELI 6;25)
Unapopita ktk jaribu nawe ukishinda Mungu wako anapata sifa kwa jamii na kutukuzwa ndo maana wakati mwingine lazima upite ktk jaribu ili Mungu wako apate kutukuzwa nawe pia unaposhinda unapandishwa cheo  ktk ulimwengu wa roho huwi vilevile,Yesu aliposhinda  alipewa mamlaka mbinguni na Duniani.. 

Basi km Mungu akiruhusu uingie ktk jaribu usidhani km utapita peke yako naye atakuwepo,utatembea naye ktk hilo jaribu mwisho wake ushindi,sifa na utukufu zitamwendea Mungu wako aliyekushindia..
MBARIKIWE.

Post a Comment

0 Comments