KUENENDA KWA IMANI (2Kor. 5:7)



Kadri siku zinavyokwenda ndivyo mambo MAPYA yanaibuliwa ili kusindikiza imani!
Katika suala la maombezi, hasa nchini Tanzania, ilikuwa mtu anaombewa tuu kwa kuwekewa mikono na kwa IMANI anapokea uponyaji na anaondoka amepona.



Mambo yaliendelea hadi ikafikia mtu anapewa kitambaa, mafuta, bangiri au kitu chochote kinachobebeka kwa urahisi, kwamba UPONYAJI WAKE UKO NDANI YA HICHO KITU. Anapewa na kuelekezwa namna ya kukitumia!


Mambo yameendelea na sasa, kwa mfano, Watu inabidi Wapite, wakanyage mafuta au wapite kwenye beseni la maji, kwamba kwa kufanya hivyo watapokea UPONYAJI au Majibu ya mahitaji yao. Na mengine mengi!

Jee, Katika Hali ya namna hii bado kweli IMANI IPO au sasa TUNAENENDEA KWA KUONA?



Ni wapi ambako Ukristo Unaelekea?

Haya mambo yanayofanyika wakati wa maombi, mfano wa hayo yaliyotajwa hapo juu, LENGO LAKE NI ZURI au BAYA?

Post a Comment

0 Comments