MAHUSIANO YA SADAKA, BARAKA, MAFANIKIO NA ULINZI.



MAHUSIANO YA SADAKA, BARAKA, MAFANIKIO NA ULINZI.



- Wakristo wengi tunajitahidi kutoa sadaka kwenye uso wa Mungu lakini ukweli ni kwamba hatujui maana halisi ya tunacho kifanya kwenye uso wa Mungu, kwa sababu
kama ningelijua nguvu iliyoko ndani ya sadaka katika maisha yangu ningelitoa kipaumbele katika utoaji wa sadaka.

- Sadaka ni ulinzi wa mambo yafuatayo katika maisha ya mtu anaye mtegemea Mungu : 
  i). Afya
  ii). Uchumi
  iii). Familia 

 - Kinacho leta shida katika maisha ya Wakristo hawajajua usahihi wa sadaka katika nyumba ya Mungu, na jambo hili shetani amepofusha macho ya watu wengi ili wasitambue uthamani,kwa sababu chanzo cha baraka za mwamini ni madhabahuni.

- Maisha ya watu wengi wanaomwamini Mungu yanaathirika kwa sababu ya kutokutii agizo ambalo Mungu analizungumza katikati yao kupitia madhabahu. 

- Ufalme wa Mungu umesimama ndani ya madhabahu kwa sababu matamko ya baraka, matamko ya kuponywa, matamko ya kufunguliwa hayatoki nje na madhabahu bali yanatoka ndani ya   madhabahu, kwa hiyo madhabahu ni kitu cha kuheshimiwa sana kuliko kitu chochote.

- Sadaka ina nguvu kubwa ya ushawishi ndani yake, kwa hiyo nikitaka mambo yangu yafunguke kiwepesi kila jambo ninalo lifikiria kulifanya nilitolee sadaka kwa sababu 
Malaki 3:10b, inadhibitisha maneno haya.

- ( Nikiombewa bila mimi kufuata kanuni bado sitapata mpenyo, kwa sababu kanuni ndizo zinazo fungua baraka )

- ( Mungu anajaribiwa na sadaka kwa sababu sadaka ndio inayo gusa moyo wa Mungu )

- Sadaka ina uwezo wa Kukata rufaa ya maisha ya mtu akaendelea kuishi hata kama muda wake umeisha.
 2 Wafalme 19 : yote na 20: yote .

- Sadaka ina uwezo wa kuugeuza moyo wa Mungu akamuwazia mtu tofauti na alivyo kuwa anamuwazia mara ya kwanza.

- ( Waamini walio wengi hawaoni umuhimu wa sadaka kwa sababu macho ya kiroho yamepofuka ).

 HII NI TAHADHARI
 - wachungaji wanapo fundisha utoaji wa sadaka makanisani waumini wengi wanaanza kujenga hoja tofauti hiyo ni laana.

- Sadaka ni hatua ya mwisho ambayo Mungu anaitazama na kutimiza baraka katika maisha ya mtu, hili jambo liliwakuta wana wa Israeli wakati wamezidiwa nguvu.
1 Samwel 7: 1-11

- Katika 1Samwel 7:6, sababu ya wana wa Israel kuingiwa hofu mpaka kufika kiwango cha kuwaogopa wafilisti ni kwa sababu ya dhambi, na kawaida ya dhambi huwa inaondoa ujasiri kabisa katika moyo wa mtu anaye mtegemea Mungu.

- Sadaka ina nguvu ya kukata na kubomoa laana inayo tembea na maisha ya mtu ili mradi tu muhusika awe mwaminifu katika utoaji.

- ( Ndani ya sadaka kuna nguvu ya msamaha, hili jambo tunaliona wazi katika 1 Samwel 7:9 ).

- Mwamini akiwa ajatoa sadaka kwa Mungu ya kujitenganisha na roho ya dhambi hata kama ametubu dhambi ile roho haita ondoka mitaani mwake, nini kifanyike?
 Inatakiwa nitoe sadaka ya kujitenganisha na dhambi ndipo niwe huru jumla

- Maisha ya mtu yanabadilika pale ambapo mtu anaamua kufuata kanuni za Mungu zilizo andikwa kwenye maandiko matakatifu.

- Kama ninahitaji maisha marefu chini ya Mbingu inatakiwa nielekeze nguvu zangu katika sadaka, kwa sababu sadaka ndio nafasi ya mwisho ambayo Mungu anaitazama katika maisha ya mtu, ili liko wazi kwa maana jinsi hii Mungu alimtoa mwanae wa pekee  Yohana 3:16

- Sadaka ya Agano ina nguvu kubwa sana ndani yake ya kulinda maisha ya mtu anaye mwamini Mungu yasiathiriwe na uvamizi wa nguvu za giza kwenye ulimwengu wa roho, hili jambo tulitazame hata katika Biblia.  2 Samwel 24:yote 

- Nguvu iliyoko ndani ya sadaka inayo uwezo mkubwa wa kutiisha hata mauti, ndio maana inaonekana wazi katika 2 Samwel 24: 25- Sadaka ya Daudi iliharibu nguvu ya mauti iliyo kuwa imekuja kwa njia ya tauni. 

- Hatuwezi kuiepuka adhabu yoyote iliyoko mbele yetu isipokuwa tunaweza kuibadilisha  kwa njia ya sadaka, ndio maana suala la sadaka inatakiwa liwe ni tendo endelevu katika maisha.

Post a Comment

1 Comments