NAMNA AMBAVYO NAWEZA KUSHINDA MAJARIBU



NAMNA AMBAVYO NAWEZA KUSHINDA MAJARIBU 



- Inafahamika wazi majaribu ni aina fulani ya vipingamizi au vikwazo vinavyo jipenyeza kwa siri au kwa uwazi katika maisha ya mwamini kwa lengo la kuathiri mahusiano ya mtu na baraka za Mungu.
- Jambo hili ni la kuwa nalo makini sana, lengo kuu la majaribu katika maisha ya mtu ni kuathiri mfumo wa Imani ya mkristo katika kumtafuta Mungu, ndio maana wakristo ambao bado hawajaimarika kiufahamu wanapoingia katika kipindi  cha kujaribiwa humuasi Mungu, mara nyingi hii huwatokea wakristo ambao hawana kina cha Neno la Mungu katika maisha yao ya kiroho.

- ( Mkristo ambaye bado hajairimarika katika msingi wa Neno ni vigumu kupenya katika majaribu atashindwa tu, kwa sababu ili kushinda jaribu kunahitajika nguvu ya Neno la Mungu katikati, kwa hiyo katika hili kunahitajika bidii ya ziada kuhudhuria mafundisho).

- Ili nijitambue kwamba nimeisha anza kudhoofika kiroho kuna mazingira haya yatajionyesha dhahiri katika maisha yangu :- 
 ( i ). Kushindwa kusoma Biblia, yaani nikianza kusoma Biblia nasikia hali ya mwili kuchoka, kupiga miayo, vile vile kusikia usingizi, wakati mwingine kazi zisizo maalumu kujitokeza ili mradi nikose muda 

 ( ii ). Uvivu wa kwenda kanisani au kushindwa kuhudhuria vipindi vya mafundisho ya Neno la Mungu 

-( watu wengi wanaoshindwa katika maisha inatokana  na kushindwa kuonyesha msimamo kwenye uso wa Mungu Kibibilia watu hawa huitwa wapunga pepo  Matendo 19:13.)

- ( nikiwa ni mkristo nisiye kuwa na msimamo katika maisha yangu ya wokovu nitaitwa nyumba ya matatizo (majaribu) )

- ( Jaribu likiwa zito kwangu inatakiwa niongeze bidii ya kuomba vilevile ya kujifunza Neno la Mungu )

- ( Majaribu hayakwepeki mpaka siku naingia kaburini, kila siku majaribu yatakuwepo tu cha msingi ni kujiimarisha katika misingi ya Neno la Mungu ili nipate ujasiri wa kukabiliana nayo )

- Wakristo wengi wanashindwa na majaribu kwa sababu ya ufahamu mdogo wa kumjua Mungu 

- Mkristo aliyejiimarisha  katika ufahamu wa Neno la Mungu hauwezi kumkuta anakata tamaa hata siku moja kwa sababu moyo wake unafahamu wazi kwamba hakuna lisilowezekana kwa Mungu sambamba na Neno katika Luka 1:37

- (Ni vigumu kuvuka katika majaribu ninayo kutana nayo kama moyo wangu haujamjua Mungu). 

- Ninapo uandaa moyo wangu katika kumjua Mungu maana yake natengeneza mtiririko wa baraka za Mungu zipate mahali pa  kupitia,vile vile ninapo unyima moyo wangu uhuru wa kumjua Mungu kupitia Neno lake kwanza kabisa kina cha maarifa ya rohoni kinajifunga, Pili baraka za Mungu zitakosa muunganiko na mahali pa kupitia, kwa hiyo mtu huyo hawezi kutoka katika tabu alizo nazo milele hata akiombewa.

- Kama moyo wangu umejaa Imani ya Yesu Kristo utatoa upendo, utatoa kuwasaidia maskini, utatoa huruma.

- Kama moyo wangu umejaa mawazo  mabaya utatoa hila, utatoa chuki, utatoa tamaa, utatoa majivuno, utanirithisha hali  ya kushindwa.

     NGUVU YA KUSHINDA MAJARIBU 

- Kwanza kabisa inabidi nifahamu nguvu ya majaribu ni nini na inatokana na nini?
Jibu: Ukweli ni kwamba nguvu ya majaribu ni dhambi 

- Majaribu yanapata nguvu ya kutesa maisha ya mtu kwa sababu ndani mwake yanakutana na dhambi, kwa hiyo ile dhambi inayokuwa ndani ya mtu ndiyo msingi wa majaribu yale

- ( nikitaka majaribu yaondoke kwangu inatakiwa nitubu dhambi kwanza )

- Majaribu yanapo iona dhambi katika maisha ya mwamini na mwamini huyo asipopata ufahamu atajikuta anaishi maisha ya majuto siku zote, kwa sababu kazi ya majaribu ni kudhalilisha utu wa mkristo siku zote.

- ( Mkristo ambaye atakuwa na tahadhari na maisha yake ataweza kuyalinda maisha yake yasinajisike ). 

- Tahadhari ni ya muhimu sana katika kila maisha ya mcha Mungu. 

- Ili niweze kupata nguvu ya kushinda majaribu inatakiwa nijifunze kwa Yesu Kristo asilimia mia moja

SWALI: Je nini maana ya kujifunza kwa Yesu Kristo ?

Jibu : Yesu kristo ni nabii peke yake katika Biblia ambaye hakutenda dhambi wala udhalimu kuonekana katika maisha yake, ndio maana Yesu Kristo akawa sababu ya wokovu wetu

- ( Nikijifunza kwa Yesu Kristo nitayashinda majaribu, hii inaonekana wazi hata katika maandiko matakatifu Luka 4:

- Silaha ya kwanza ya kuyashinda majaribu au kupata wepesi katika majaribu ni kuishi na Roho Mtakatifu 

- Nikiishi na Roho mtakatifu ataniongoza katika mambo yafuatayo :-
 a ). Kunipa ufahamu wa kumsogelea Mungu
 b ). Kunipa nguvu ya kushinda dhambi
 c ). Kunipa uwezo wa kuomba zaidi, hapa kupata hali ya mtiririko 

- Mkristo anayekutana na majaribu ikiwa hana Roho Mtakatifu ndani mwake anaweza akamkufuru Mungu jumla kwamba hamsikii kumbe ndani mwake hana muunganiko wowote, wakristo wa aina hii maisha yao ya ucha Mungu huishia kwenye kutangatanga kwenye makanisa na kwenye sehemu za maombezi lakini mwisho wa  yote hubaki sifuri vile vile bila jibu 

- Nikitaka kushinda kila aina ya jaribu linalo jitokeza kwenye maisha yangu inatakiwa niishi maisha ya ukweli na maisha hayo ndiyo humfanya Roho Mtakatifu kuweza makazi ndani  ya mtu.

-( Kuishi maisha ya ukweli kuna gharama, na gharama yenyewe ni kuikana nafsi kwa ajili ya Kristo).

- Na majaribu yanaogopa mlango wa mwamini anayeishi katika  kweli na haki 

- Jambo la kukumbuka inatakiwa nidhibiti udhaifu nilio nao ili mlango wa majaribu kutumia madhaifu nilio nao usiwepo.

Post a Comment

0 Comments