NAMNA YA KUSIKIA NA KUIELEWA SAUTI YA MUNGU ILI IKUSAIDIE KATIKA KUFANYA MAAMUZI

 


1

Mada: Mambo mhumu kujua kuhusu sauti ya Mungu

Katika sehemu ya kwanza ya ujumbe huu niliandika kuhusu mambo matatu ambayo ni kujenga mahusiano na Roho Mtakatifu, kuongeza ufahamu wako kuhusu alama za mawasilano na tatu ujue namna ya kutofautisha sauti ya Mungu na isiyo ya Mungu. Ili kusoma sehemu ya kwanza bonyeza link hii  https://sanga.wordpress.com/2015/04/02/namna-ya-kusikia-na-kuielewa-sauti-ya-mungu-ili-ikusaide-katika-kufanya-maamuzi-sehemu-ya-1/ Sasa fuatana nami tuendelee na mabo mengine muhimu kujua:
  • Vifahamu vikwazo vinavyopelekea kutokusikia sauti ya Mungu
Biblia imeainisha vikwazo kadhaa vyenye kupelekea mtu kutokuisika sauti ya Mungu. Vikwazo hivyo ni pamoja na moja kutenda dhambi au kuishi maisha ya dhambi (Isaya 59: 1-2), pili kukosa uaminifu (Hesabu 12:7-8, 1 Samweli 2:35). Biblia katika Isaya 59: 1-2 inasema ‘Lakini maovu yenu, yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia’ Pia katika Hesabu 12:7-8 imeandikwa ‘Sivyo ilivyo kwa mtumshi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote; Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si mafumbo.

2
  • Ongeza ufahamu wako kuhusu njia anazotumia Mungu kuzungumza
Ni dhahiri kwamba zipo njia mbalimbali ambazo Mungu hutumia kusema na wanadamu. Namna Mungu anavyosema na huyu sivyo atakavyosema namtu mwingine. Tofauti hizi zipo tegemeana na mahusainao yaliyopo kati ya Mtu na Mungu na pia ngazi ya kiroho aliyonayo mtu katika ulimwengu wa roho. Hivyo ni muhimu sana kuwa na uelewa wa hizi njia mbalimbali ili kuelewa mazingira yake na hivyo kutafuta kumsika Mungu kupitia njia hizo ili kudumisha mahusiano na mawasiliano yako na Mungu. Katika sehemu ya tatu ya somo hili nitaanza kufundisha njia husika hivyo naamini ufahamu wako utaongezeka.
  • Unahitaji kufahamu umuhimu wa Mungu kuzungumza/kusema nawe
5
Zipo sababu nyingi za Mungu kuzungumza na wanadamu laikini kubwa yenye kuzibeba zote ni ile iliyoandikwa katika Zaburi 32:8 kwamba ‘Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama’. Ni muhimu ukakumbuka kwamba kwa mujibu wa Wayumi 8:28 umeitwa ili kulitumika kusudi la Mungu katika siku zako. Ili uweze kulitumika ipasavyo sharti akuongoze katika njia sahihi. Naam njia mojawapo ya kukuongoza na kukufundisha ni kwa yeye kusema na wewe.
Lengo lake katika kusema na wewe ni kukuongoza katika njia sahihi kwa kukuondoa kwenye makusudi ambayo yapo nje na mapenzi yake kwenye maisha yako maana imeandikwa ‘Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam hata mara ya pili ajapokuwa mtu hajali, ili amwondoe mtu katika makusudio yake, Na kumfichia mtu kiburi’ (Ayubu 33:14, 17).
  • Ongeza ufahamu wako kuhusu ulimwengu wa roho
Mambo yote yanayotokea katika ulimwengu wa mwili yameanzia katika uilimwengu wa roho, naam maamuzi ya kile ambacho hutokea katika ulimwengu wa mwili hufanyika katika ulimwengu wa roho. Zaidi hata mapambano (vita vya kiroho) yote aliyoanayo mwamini katika kulitumikia kusudi la Mungu hufanyika katika ulimwengu wa roho.
Hivyo kuwa na ufahamu wa ulimwengu wa roho hususani namna ya kuishi na  kuwasiliana katika ulimwengu huo ni muhimu sana kwa mwamini mwenye kutafuta kujua na kuisikia sauti/mawazo ya Mungu katika maisha yake kwa kuwa Mungu ni roho kama alivyo na Shetani pia. (Rejea 2 Wafalme 6:8-17 na Waefeso 6:10-12).

3

Mpenzi msomaji usiruhusu yale unayoyapitia au yale ambayo watu /mazingira yanasema juu yako yabadilishe au kuongoza maisha yako, bali tafuta kuijua na kuielewa sauti ya Mungu kwenye maisha yako. Na ndiyo maana somo hili limekuja ili kukusaidia kufika mahala ambapo utaweza kuyatenda mapenzi kamili ya Mungu kwenye maisha yako.
Baada ya kuwa tumeangalia mambo haya saba ambayo ni muhimu kujua kuhusiana na sauti ya Mungu, katika sehemu ya tatu nitaanza kuandika kuhusu njia mbalimbali ambazo Mungu hutumia kusema na wanadamu. Somo litaendelea….

Na: Patrick Sanga

Post a Comment

0 Comments