NINI KIFANYIKE ILI NIWEZE KUSAHAU NILICHO KISAMEHE




Nikijiona ninashindwa kusahau jambo ambalo nimemsamehe mtu hiyo ni picha wazi kwamba bado sijamsamehe, kwasababu kitendo cha kukumbuka  nilicho kisamehe kitanifanya maumivu kurudi upya, hapo utakuwa mwanzo wa moyo wangu  kuishi katika maumivu ya ndani kwa ndani .


(Maumivu ya ndani kwa ndani  yanayotokana na kutokusamehe  ndani ya moyo yanaathiri utendajikazi wa imani).

Mkristo anayeshindwa kusahau jambo ambalo amemsamehe  mtu haishi na Roho mtakatifu, kwa maana zaidi ni mkristo kwa nje yaani kimwili, kiroho ni mpinga kristro , na hao ndio wamejaa katika makanisa ya kiroho.

Hakuna majibu ya maombi yoyote yale yatakayo toka kwenye uso wa Mungu nakuja kwenye maisha ya mwamini kama moyo wake hajautakasa  usiwe na hila na mtu yeyote , ni kitu ambacho hakiwezekanikani .

(Nikitaka Baraka za Mungu inatakiwa nitakase moyo wangu  inatakiwa moyo wangu  usiwe na visasi na watu walioumbwa kwa mfano wa Mungu).

(Wakristo wengi wanashindwa kupokea Baraka za Mungu kwasababu mioyo yao inakuwa mizito kuachilia na kusahau waliyotendwa).

Nikisamehe na kusahau maumivu niliyotendwa  ninaonyesha uhai wa Mungu waziwazi katika maisha yangu ya wokovu,hata katika kitabu cha waebrania limethibitishwa jambo hili sura ya 8:12,

( Nikiamua kuvaa vazi la wokovu inatakiwa nijikane waziwazi nafsi yangu)

( Yesu nisaidie kwenye maisha yangu mimi siku zote niitwe haki )

Yesu Kristo ndiye mwanzilishi wa kusamehe na kusahau ndio maana anatusisitiza sana juu ya kusahau tuliyoyasamehe kwa watu, hata katika kitabu cha Nabii Isaya enzi za babu zetu wakina Ibrahimu, Isaka na Yakobo walilisoma andiko hili Isaya 43:18.

Muda ninaotumia kukaa chini kuhojiana mambo yasiyokuwa na utukufu kwenye uso wa Mungu ni bora ningeutumia muda huo kusoma angalau kurasa mbili za Biblia kitu kipya kitazaliwa katika maisha yangu.

Imani za wakristo zimeathiriwa sana na mambo yasiyo kuwa na maana wanayoyaruhusu kuingia kwenye mioyo yao, hapa inabidi nipate ufahamu wa ziada wa kupambanua kwa sababu nikiruhusu moyo wangu kuvaliwa na mambo yasiyokuwa na utukufu kwa Mungu ndio mwanzo wa kujeruhika kiroho.

Msingi wa kuijenga imani ni kusamehe na kusahau, hapo ndipo unapofunguka ukurasa mpya wa ushindi katika maisha ya ucha Mungu.
ANGALIZO NO. 1
        Ninapoamua kuokoka maana yake nimeamua kuyaishi maisha ya Yesu Kristo aliyoishi katika mwili , kwa hiyo lazima nijikane kwelikweli bila kutazama mazingira yaliyonizunguka au ninayo yapitia yaani hapa ni kutimiza sheria yote ya Mungu hata kama ndani yake kuna maumivu “ Ee Yesu nisaidie ’’

Ninasisitizwa kusamehe na kusahau kwa sababu darasa la Roho Mtakatifu lina mambo mengi sana.
Bila kupita kwenye darasa la Roho Mtakatifu maono niliyonayo ni vigumu kutimia kwa sababu darasa la Roho Mtakatifu ndilo linalotuimarisha katika misuli ya imani.

Kila hatua ninayo ipitia katika maisha yangu ya imani haijalishi ni ugumu wa aina gani hilo ni darasa la kunijenga kwa ajili ya kustahimili makubwa zaidi yatakayo jitokeza kesho.
2 Timotheo 3:12 

Maandiko kutimia katika maisha ya mwamini ndiko kunako sababisha mpenyo kutokea.

Yesu Kristo alipotangaza msamaha wakati yuko msalabani alikuwa akifundisha wazi ulimwengu maisha ya visasi hayana Baraka.

KINACHOFANYA MWAMINI ASHINDWE KUSAMEHE
Kinachofanya mwamini ashindwe kusamehe ni udhaifu alionao katika imani ya kumwamini Mungu, kwa sababu mtu anaye mwamini Mungu lazima awe na asili moja na Mungu, kwa hiyo suala la yeye kusamehe ni lazima ili asifarakane na uwepo wa Mungu, mbona Biblia imesema wazi katika wakorinto ?
1 wakorinto 6:17 .

Kama kweli ninamcha Yesu Kristo suala la kusamehe halitanisumbua kichwa, lakini kama ni muigizaji kwenye uwepo wa Mungu kamwe siwezi kusamehe na kusahau.

MBINU ZA KUMJUA MTU AMBAYE HANA TABIA ZA KUSAMEHE NA KUSAHAU
i.                     Hawezi kuomba, mtu wa aina hii akiingia kwenye maombi ile hali ya maumivu ya kutendwa ndiyo inayo jidhihirisha ndio maana utamkuta anaishia kulia na kupiga kelele, sikwamba Roho Mtakatifu anakuwa amemshukia hapana bali kumbu kumbu ya kutendwa ndio inayo kuja ndani mwake.

MBINU YA KUMFAHAMU MTU MWENYE HILA NA ROHO YA VISASI NDANI YAKE.
i.                     Picha ya mtu mwenye hila na roho ya visasi ndani mwake hujidhihirisha kwa njia ya kinywa, namna ambavyo hutoa maneno ya uchochezi, uchonganishi, uzushi, uongo watu wa aina hii hata Mtume Paulo alikutana nao, Yesu Kristo alikutana nao, Musa Nabii alikutana nao, ndio maana 2 Timotheo 3: Nikiisoma yote nitaona namna ambavyo walizusha mambo mengi kuhusu watumishi wa Mungu, ndio maana Paulo Mtume anatoa tahadhari dhidi ya watu kama hao 2 Timotheo 3: 6-9, vilevile Timotheo alitoa tahadhari sanasana 2Timotheo 2:16-18 .

Post a Comment

0 Comments