SOMO KOMBOA NDOTO ZAKO




KOMBOA NDOTO ZAKO

Nini maana ya ndoto?

Ndoto ni hali fulani inayokuja kwa mtu akiwa amelala usingizi yaani viungo  vyote vya mwili vinakuwa havina ushirikiano.

Tafsiri ya pili
Ndoto ni malengo au matarajio anayokuwa nayo mtu na wakati huo huo anakuwa ana akili timamu yaani akiwa macho hajalala usingizi, vilevile ni mipango ya mtu.

Wakristo wengi wana ndoto lakini wameshindwa  kuzifikia ndoto zao, kwasababu wameyakataa maarifa ya Neno la Mungu.

(Jambo hili ni la kuwa nalo makini sana jinsi ninavyopwaya katika Neno ndivyo nitakavyopwaya katika mafanikio, kwahiyo lazima niweke bidii katika kutafuta maarifa ya Neno la Mungu)
Mithali 1:25-33.

(Nikipwaya kwenye Neno udhaifu nilio nao utanidhalilisha, hii yote inatokana na kukosa ufahamu wa Kimungu).

Chanzo cha ndoto zangu nilizo nazo kupoteza mwelekeo ni pale ambapo ninaukataa ufahamu wa Neno la Mungu.

Ninapoukataa ufahamu wa Neno  la Mungu maana yake nimeukataa mwonngozo wa Roho Mtakatifu, vilevile nisipotoa muda wa kusoma Biblia kwa siku maana yake moyo wangu sijautendea  haki ya kuzungumza na Roho Mtakatifu.

Nikisoma Biblia ninapata nguvu ya rohoni , kwahiyo  ni rahisi ndoto nilizo nazo  zikatimia bila kuathiriwa na adui.

Sababu kuu ya kutokusikiwa na Bwana wakati wa maombi inatokana na mimi kwa kutokujiwekea utaratibu wa kuyaishi Maandiko Matakatifu.

Ndoto zangu zitatimia iwapo nitafanya mambo makuu mawili:-
1)Nikiruhusu hali ya kuwepo kwenye uwepo wa Mungu mara kwa mara.
2)Nikiruhusu hali ya kujisomea  Neno la Mungu wakati wowote lakini isipite siku sijasoma.

Katika haya mambo mawili yatasababisha kibali cha Kimungu kuyavaa maisha yangu, kwahiyo nafasi ya upendeleo itakuwepo tu hata iweje.

Nikiweka mikakati ya usomaji wa Biblia na usikilizaji wa Neno la Mungu ,kwa maana zaidi kutokuruhusu hali ya kukosa kwenye uwepo wa Mungu ndoto zangu nitakuwa nimeziokoa.

Ikiwa nina ndoto na ninajifahamu kwamba nina ndoto za siku  zijazo inatakiwa niziatamie ndoto hizo ndipo zitapata wepesi wa kutimia.

Ndoto niliyo nayo itatimia iwapo maarifa ya Biblia yataniongoza, maarifa ya Biblia (Neno la Mungu) ,ndiyo yanayoshinikiza imani ya mtu kufika kile kiwango cha kuamuru jambo na likatimia.

NAMNA YA KUSIMAMIA NDOTO ZANGU
Ili niweze kutambua ni namna gani ya kuzisimamia ndoto zangu inatakiwa nijifunze kwa walionitangulia ambao ninawasoma  kwenye Maandiko Matakatifu (Biblia).

Mfano mzuri ambao tunaweza kuutumia ukatusaidia tunaupata kwa Yusufu Mwanzo 37:5-----.

Upofu wa kiroho mara nyingi husababisha ndoto za mtu kutotimia , mara nyingi  hii inatokana na mwamini kushindwa kupambanua pale ambapo Mungu anasema naye.

Watu wengi ndoto zao zimeathiriwa  kwasababu wanashindwa wao kama wao kusimama kuziatamia bali wanashirikisha watu wengine wasiokuwa na maharifa nayo, kinachotokea ni nini , hiushia katika kukatishwa tamaa na kuvunjwa moyo , ndiyo maana Mungu akasema kupitia Ezekieli 2:1.

Mungu anazungumza na mkristo ambaye ameamua maisha yake kuwa chini ya mwongozo wa Neno lake.

Wakristo wengi wasiposimama vizuri katika Maandiko Matakatifu, yaani katika kulisikiliza Neno la Mungu kwa undani mwisho wa siku watazikuta ndoto zao zimezimika .

Ndoto za wakristo zinazimika kwasababu asilimia kubwa ya waamini hawana msimamo katika suala zima la kumcha Mungu.

Mwamini mwenye uwezo wa kumsikia Mungu akisema huyo ana uwezo wa kuatamia ndoto zake mpaka zikatimia.

Kama simsikii Mungu akisema na mimi uwezo wa kuatamia ndoto zangu ni mdogo mno. Kwasababu ili ndoto za mwamini zitimie zinahitaji mwongozo wa Neno la Mungu.

Hii inasikitisha sana ndoto za waamini  wengi zimeishia njiani yaani hazijatimia hii imetokana na waamini kushindwa kuziatamia ndoto zao kupitia Neno la Mungu.

Neno la Mungu peke yake ndio lina uwezo wa kusababisha ndoto za mtu zikatimia.

Katika Mwanzo 37:11b pale anaposema  ‘baba alilihifadhi neno hili’’, ni ufahamu kwangu leo kwamba kila nitakayoiota ninahitajika kuandika yaani kuweka kumbukumbu mpaka siku itakapotimia.

Kila jambo linalotokea kwenye maisha yangu  ukweli ni kwamba Mungu alishanieleza kwenye ndoto shida inakuja kwamba kushindwa kupambanua vilevile kutokukumbuka, ndio maana inatakiwa kila ndoto niiandike kwa kumbukumbu siku za usoni.

JINSI YA KUZILINDA NDOTO ZANGU ZISIATHIRIWE
Ili niweze kuzilinda ndoto zangu zisiathiriwe inatakiwa niikuze  mamlaka italazimisha hali ya utiisho katika kila roho inayopambana na mimi, ndio maana Biblia ikazungumza Isaya 54:17.

Silaha ya shetani inakosa nguvu kwa mwamini mwenye mamlaka ya Neno la Mungu ndani mwake.

Hali ya kushindwa kwa mwamini inatokana na mamlaka aliyonayo imeshapoa yaani imepoteza uwezo.

Mwamini aliyepoteza mamlaka sanasana hukumbukwa na mambo yafuatayo:-
i)                    Hana kabisa ulinzi wa Mungu juu yake, ndio maana waweza kuwa kituo cha magonjwa , kwahiyo katika hili huwa tunapata matokeo  ya mwamini kudhoofika kiafya.
ii)                     Asili ya udhaifu alionayo kwenye mwili wake huwa inainuka , sasa basi hapa inategemea ni udhaifu gani alionao Mfano:Muongo, Mzinzi, Mlevi, Tapeli, na mengine mengi yanayofanana na haya.
iii)                  Shetani humwibia ufahamu wa kile anachosikia kuhusu Mungu, vilevile utayari wa kukaa chini  kufundishwa, ndio maana inaweza ikatokea mwamini asije kanisani asiwe na kazi maalumu hiyo yote  inatokana  kashaibiwa ufahamu.
iv)                 Maisha yake hufanywa jalala la kila matatizo.

Ndoto za  mwamini zinalindwa kutokana na jinsi mwamini anavyozidi kukua kiroho yaani kuongezeka zaidi kimaarifa, maarifa ndani ya mtu yakiongezeka  kina cha ufahamu wa rohoni hufunguka na mtu huyo mbekle za uwepo wa Mungu huitwa mtu wa imani.

Silaha itakayoweza kuyalinda maisha ya mkristo ni ile roho ya kupambanua itakayoyavaa maisha yake.

ANGALIZO :Nikiwa ni mkristo mwamini na wakati huohuo sina uwezo wa kupambanua ni vigumu kuvishinda vita vya kiroho , ndani ya kupambanua ndipo tunapopata ufahamu wa kujua sauti ya Mungu ni ipi na sauti ya roho zidanganyazo ni zipi, tofauti na hapo hutoki kwenye mtego.

Kutimia kwa ndoto za mwamini kutokana nay eye anavyoongezeka kiukaribu kati ya yeye na Mungu.

NINI KIFANYIKE ILI NDOTO ZANGU ZIZAE MATUNDA:
Ili ndoto zangu ziweze kuzaa matunda haitakiwi nitoke nje ya kanuni za Neno la Mungu, hata inapotokea nimekosea inatakiwa nijirudi haraka ili nisitoke nje ya ule mfumo wa Baraka za Mungu, ndio maana Yoshua alipewa maagizo katika Yoshua 1:7,8.

Jambo hili ni la kuwa nalo makini sana
Shetani anapitia katika lile jambo ninalolipenfda kuyaathiri maisha yangu.


Ili niweze kuidhibiti hali  hiyoiliyozungumzwa kwenye point ya juu inatakiwa ufahamu wangu niulazimishe kumheshimu Mungu ndipo nitakapopata uwezo wa kuyatambua mapenzi ya adui kabla hajaniumiza.

Post a Comment

0 Comments