SOMO: NAMNA YA KUFANYA ILI FIKRA ZAKO ZITUMIKE KUFANIKISHA MAISHA YAKO(8)

SOMO: NAMNA YA KUFANYA ILI FIKRA ZAKO ZITUMIKE KUFANIKISHA MAISHA YAKO(8)

SEMINA: NENO LA MUNGU
ENEO: DAR ES SALAAM
MWL: C. MWAKASEGE
SIKU: 8
▶Lengo
Kuweka ndani yako maarifa ya Kiblia yatakayokuwezesha kutumia FIKRA zako ili ufanikiwe ktk maisha yako
*Mith 23:7(a)*
*HATUA.....*
5⃣Jiulize maswali yanayofanya FIKRA zako zifikiri kiubunifu
*MAENEO MACHACHE UNAYOHITAJI KUFUATILIA*
1) Kufikiri juu ya soko kwanza kabla ya kitu ulichonacho kuuza
➡Wengi ulima kwanza,ufuga kwanza, uanzisha duka kwanza kisha ndo wanatafuta wateja na soko..Anza kwanza na soko na wateja ndipo uende kwenye kufuga, kulima na n.k
➡FIKRA zako zifikiri soko kwanza kabla ya chupa ya mafuta
➡Hata kama una pesa zako ukipeleka mradi wowote Benki wakiukataa usiutekeleze hata kama unapesa zako maana wao ufikiri kama ulipa au la!
2) Zizoeshe FIKRA zako kufikiri kiubunifu maana ichi ndicho kinazaa viwanda
➡Soma na jifunze uchumi wa Japan, South Africa, Marekani n.k
3)Tafuta mahitaji ya muda
➡Muda una mahitaji yake
➡Fikiri kwa namna ya kutafuta majibu ya mahitaji ya muda
✳Hayo ni masomo tosha ila leo nimepanga tujifunze kwa habari ya
*KUJIBU MALALAMIKO*
*Jizoeze FIKRA zako kujibu malalamiko*
➡Zifanye FIKRA zako zifikiri kiubunifu
✅Unaposikia mahali popote pale pana malalamiko usiziamshe FIKRA zako nazo kulalamika
✅Haijalishi malalamiko hayo ni halali kiasi gani
✅Zizoeshe FIKRA zako kufanya utafiti ktk malalamiko hayo,
⚫Nani analalamika andika, ⚫wanalalamika sababu gani andika,
⚫juu ya nini andika!
⚫Muda gani wanalalamika
*MIFANO KADHAA YA KUJIFUNZA KUTOKA KWENYE BIBLIA*
1⃣Wapelezi 12
*Hes 13,14*
✅Walipewa kazi ya kwenda kufanya utafiti ktk nchi ya Kanani na utafiti ule ulikuwa ulikuwa wa kiuchumi mno tazama maswali ya utafiti wao.
✅Kuleta ushahidi kuwa walienda huko ni kurudi na kichanja cha Zabibu.
✅Kazi ya utafiti ni kusaidia watu kufikiri zaidi.
✅Wale 10 FIKRA zao zilijioanisha na walichokiona kule na kujiona ni mapanzi, waliandika FIKRA zao zilichokiona *Hes 13:33*
✅Wengine baada ya kusikia habari hizo nao wakaanza kulalamika hata kusema kwanini tulitoka Misri. *Hes 14*
✅Joshua na Kareb wakasema tunaye MUNGU tutasonga mbele na kuingia kanan. FIKRA zao zilifikiri ubunifu na jibu la kulalamika kwa wengine
*TUNAJIFUNZA NINI HAPA KWA JOSHUA*
*1)* MUNGU akikuonyesha tatizo ina maana anataka kuamsha FIKRA zako zijiandae kutatua tatizo hilo pamoja naye
*Mith 3:5-6*
✅Akili hazikuumbwa zifanye kazi zenyewe bali na NENO LA MUNGU na ROHO MTAKATIFU
✅MUNGU anataka akili zako zikae mkao wa kutatua tatizo
✅MUNGU aliijua Kanani na hivyo kuvuka kuingia ilikuwa ni hatua lazima FIKRA zao ziwaze majibu na zione chakula na si majitu
*2)* Kulalamika ni ishara ya kuwa FIKRA hazioni jibu la tatizo na zinalitafsiri kuwa ni tatizo
✅Ndiyo maana walijona kama mapanzi na ndivyo walivyowaona
*3)* FIKRA ziliumbwa zione na kutafsiri changamoto zilizo katika FIKRA ya mtu na kuzitolea ufumbuzi
✅ FIKRA ziliumbwa ili zione
*2Kor 4:3-4*
✅FIKRA kama hazioni haziwezi kutafsiri ilivyo sahihi na sawasawa
✅NENO NURU tafsiri yake ni MAENDELEO KIBLIA
✅Hapo mwanzo kulikuwa na giza MUNGU akasema na iwe NURU=MAENDELEO
✅Mahali popote alipo mtu wa MUNGU mwenye HAKI lazima awasaidie wengine kufikiri. Sisi ni changamoto na chachu ya maendeleo.
*4)* Ile kwamba mtu amekutanguliza ktk jambo haina maana unafikiri vizuri kuliko wewe
✅Wapepelezi 12 walipewa nafasi na kutangulia kufikiri kabla ya wenzao lakini FIKRA zao wale 10 zilikwama na kushindwa kuona
✅Ukifuata FIKRA za mtu aliyekwama na wewe utakwama
✅Usiruhusu FIKRA zako kulalamika pamoja na walalamikao
✅Ukifuata FIKRA za kiongozi aliyekwama utakwama na wewe
*PALIPO NA MALALAMIKO NI ISHARA YA KUWA HAPO KUNA FURSA YA CHAKULA*
👆🏽Daka hiyo👆🏽
✅Kwa hyo fanya utafiti mahali hapo
✅ROHO MTAKATIFU anakupa fursa namna ya kujibu kulalamika kwako au sehemu hyo
✅Kalisha FIKRA zako ktk mkao wa kiutafiti. Tafuta chakula kati ya walalamikao, tafuta ndani ya nchi,mkoa,wilaya,kanisa,familia,umoja tafuta walalmikao we kaa hapo fanya utafiti
✅Tofauti ya Joshua na Kareb na wale wengine ilikuwa ni kutafsiri kwao
✅Ilihitaji ubunifu kuyageuza majitu kuwa chakula. Maana katikati ya jangwani na Kanani kuna FIKRA
✅We zipe kazi FIKRA zako utaona
*MFANO WA PILI*
*Hes 11:11-15*
✅Mussa alimlalamikia MUNGU
✅Kulalamika kwa Mussa kulitoa ajira kwa watu 70
✅Kiongozi anapolalamika ama kazi imemzidia jua kuna fursa ya ajira inakuja jipange, jiandae
✅Usimsaidie kiongozi ktk kulalamika maana atakapochagua wale 70 hatakuchagua, atakuacha
*MFANO WA TATU*
*Habakuki 1,2:1*
✅MUNGU alijibu kulalamika kwake, hakujibu kilichomfanya alalamike maana hakujua kuwa hicho kilichomfanya alalamike kinajibiwa na FIKRA
✅Kualamika kwenye maombi hakusaidii, maana njozi imebeba jibu na njozi bila matatizo haina thamani
✅Maono bila kujibu matatizo na maswali ya watu hayana thamani. _"Vision must has problems to solve otherwise has no value"_
✅Kulalamika kwenye maombi hakusaidii ikiwa uwezi kiunganisha njozi na jibu
*HOME WORK*
✳Tafuta mahali penye malalamiko utapata chakula
*..."Jesus Up"...*
*****SIKU YA NANE NA MWISHO*****

Post a Comment

0 Comments