NINI MAANA YA NEEMA
watu wengi wamekuwa wakitafsiri kuwa NEEMA ni ' hali ya kupewa kitu ambacho haukukidhi vigezo ama haukustahili kupewa lakini unapewa kwa sababu ya maamuzi ya anayetoa kitu hicho'. sina tatizo na tafsiri hiyo ila leo nimeona tuangalia tafsiri ya NEEMA kama ilivyoelezwa Katika kitabu cha TITO ambayo inamaanisha hivi ' NEEMA ni uweza wa MUNGU utuwezeshao kuukataa UBAYA na TAMAA za KIDUNIA' Kwa kuwa MUNGU Alijitoa NAFSI yake kwa AJILI yetu ili atukomboe na MAASI YOTE. Tito 2;11-14 UWE NA WAKATI MWEMA , NEEMA YA YESU IWE NAWE
MAOMBI YA KUTUMA MAPIGO KWA WACHAWI WANAOKUTESA.
Na Peter Mabula. Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU. BWANA YESU atukuzwe. Karibu tujifunze na tuombe maombi ya ushindi sana. Yeremia 15:20-21 '' Nami nitakufanya kuwa kama ukuta wa boma la shaba juu ya watu hawa; nao WATAPIGANA NAWE; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, ili nikuokoe, na kukuponya, asema BWANA. Nami nitakuokoa na mkono wa watu wabaya, nami nitakukomboa katika mkono wao wenye kutisha. ' ' Neno la MUNGU linasema kwamba adui zako katika ulimwengu wa roho watapigana na wewe. Maana yake wewe na adui zako kwenye ulimwengu wa roho mtapigana. Katika mapigano au vita kuna mambo mawili; kuna kushinda na kuna kushindwa. Lakini ashukuriwe MUNGU maana ukiwa katika wokovu wake utashinda. Ukiwa muombaji sahihi hakika utashinda. Changamoto ya wakristo wengi huwa hawapigani na adui kimaombi bali wanamkemea tu adui. Kwenye ndoto najua kabisa ni mara nyingi sana umeonyeshwa juu ya vita inayokukabili. Najua kabisa kwenye ...
1 Comments
Amen ubarikiwe
ReplyDelete