SADAKA
INAYOMFANYA MUNGU AKUKUMBUKE
*NA
MWL MWAKASEGE*
>>Katika
kujifunza somo hili nataka tuangalie point kama tano hivi.
*1
KUNA SADAKA UNAYOWEZA KUMPA MUNGU NA IKAWA UKUMBUSHO MBELE ZAKE ILI AWE
ANAITUMIA KUKUMBUKA*
_’’Matendo
ya mitume 10:1-4, 31 Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa
kikosi kilichoitwa Kiitalia, mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake
yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima. Akaona
katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na
kumwambia, Kornelio! Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana?
Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za
Mungu. akasema, Kornelio, kuomba kwako kumesikiwa, na sadaka zako zinakumbukwa
mbele za Mungu’’_
>>Hii
si sadaka kama zilivyonyingine maana Mungu huwa anaitumia kukumbuka.
*2
KUNA VITABU VILIVYOKO MBINGUNI AMBAKO KUNA ANDIKWA VITU AMBAVYO MUNGU ANATAKA
VIWE KUMBUKUMBU KWA AJILI YAKE NA KWA AJILI YAKO*
_’’Malaki
3:16 Ndipo wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. Naye Bwana
akasikiliza, akasikia; na *kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake*, kwa
ajili ya hao waliomcha Bwana, na kulitafakari jina lake’’_
>>Mbinguni
kuna Vitabu vya ukumbusho zinakoandikwa kumbukumbu mbali mbali, Ngoja
nikuoneshe kwenye maandiko
*a)
Kitabu cha uzima cha wenye uhalali wa kukaa na Bwana milele*
_’’Ufunuo
3:5 Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake
*katika kitabu cha uzima*, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na
mbele ya malaika zake’’_
*b)
Kitabu kilichofungwa kwa mihuri (seal)*
_’’Ufunuo
5:1 Kisha nikaona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti
cha enzi* kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma, kimetiwa muhuri saba*’’._
>>Yesu
ndiye aliye na uwezo wa kukifungua na kufungua hiyo mihuri saba. Na baada ya
kufunguliwa kuliandikwa matukio na nyakati yaliyo katika nyakati.
*c)
Kitabu cha hukumu*
_’’Ufunuo
20:12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha
enzi; na *vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha
uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile
vitabu, sawasawa na matendo yao*’’_
_’’Daniel
7:10 Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na
elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na *vitabu
vikafunuliwa*’’._
*d)
Kitabu cha mashtaka yanayopelekwa na mshitaki ibilisi*
_’’Wakolosai
2:14 akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake,
iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;’’_
*e)
Kitabu wanachopewa watumishi*
“_Ufunuo
wa Yohana 10:1-10, 8 Na sauti ile niliyoisikia kutoka mbinguni ilinena nami
tena, ikisema, Enenda, ukakitwae kile kitabu kilichofunguliwa katika mkono wa
yule malaika, aliyesimama juu ya bahari nag juu ya nchi.9 Nikamwendea malaika
yule nikamwambia kwamba anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, Kitwae, ukile,
nacho kitakutia uchungu tumboni mwako, bali katika kinywa chako kitakuwa kitamu
kama asali. 10 Nikakitwaa kile kitabu kidogo katika mkono wa malaika yule,
nikakila; nacho kikawa kitamu kama asali kinywani mwangu, na nilipokwisha
kukila tumbo langu likatiwa uchungu.”_
katika agano la kale walitumia neno gombo na
walikuwa wanaitwa chuo au gombo la chuo. Mfano Kitabu cha Isaya kiliitwa chuo
cha nabii Isaya. Utumishi kitabu ambacho Mungu kawapa watumishi ili waweze
kwenda kama kilivyoagiza. _”Yohana 1:8 8 Kitabu hiki cha torati kisiondoke
kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia
kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo
utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana”_
*f)
Kitabu cha ukumbusho*
_”Waebrania
9:18-22 Kwa hiyo hata lile la kwanza halikuanzwa pasipo damu. Maana kila amri
ilipokwisha kunenwa na Musa kwa hao watu wote, kama ilivyoamuru sheria,
aliitwaa damu ya ndama na ya mbuzi, pamoja na maji na sufu nyekundu na hisopo,
akakinyunyizia kitabu chenyewe, na watu wote, akisema, Hii ni damu ya agano
mliloamriwa na Mungu. Na ile hema nayo na vyombo vyote vya ibada alivinyunyizia
damu vivyo hivyo. Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na
pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo._
Jinsi Musa alivyokuwa anaweka wakfu vitu vya
hema. Na maandiko yanasema kilichokuwa kinafanyika kwenye hema kilikuwa ni
kivuli cha mambo ya ulimwengu wa roho yaliyo halisi.
Vitu vyote ndani ya hema vilikuwa vinatakaswa
kwa damu na Musa alikuwa anasema hii ni damu ya agano , Pia katika agano jipya
tunaona _”Basi, Mungu wa amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu Mchungaji Mkuu
wa kondoo, kwa damu ya agano la milele, yeye Bwana wetu Yesu, Waebrania 13 : 20”_
Vitabu vilivyoko mbinguni aliye na uhalali wa
kuvifungua ni Yesu ili na sisi tupate uhalali wa kuvifungua tunahitaji damu ya
Yesu. kufuta hati za mashtaka tunahitaji damu ya Yesu, uzima wa milele
unahitaji damu ya Yesu ili kufuta dhambi zako. Pia katika utumishi napo ili
utumike vema unahitaji kunyenyekea chini ya damu ya agano.
*Yesu alijitoa kuwa sadaka ili iwe ukumbusho
wa agano Jipya*
*3
SADAKA YAKO INAPOINGIZWA KATIKA KITABU CHA KUMBUKUMBU CHA MUNGU NA MUNGU
ANAITUMIAJE*
_”Malaki
3:16’18 16 Ndipo wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. Naye Bwana
akasikiliza, akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa
ajili ya hao waliomcha Bwana, na kulitafakari jina lake. *17 Nao watakuwa
wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa
hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe
mwenyewe amtumikiaye* 18 Ndipo mtakaporudi, nanyi mtapambanua kati ya wenye
haki na waovu, na kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.
_Malaki
4:1-3 “1 Kwa maana, angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuru; na watu
wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile
inayokuja itawateketeza, asema Bwana wa majeshi; hata haitawaachia shina wala
tawi. 2 Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenye
kuponya katika mbawa zake; nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa
mazizini. 3 Nanyi mtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu chini ya nyayo za
miguu yenu; katika siku ile niifanyayo, asema Bwana wa majeshi.”_
angalia kwa makini hapo mstari wa 17,
utajifunza kitu kikubwa sana . Anaposema nitaifanya siku, lakini tukienda
kwenye Mwanzo tunaona siku ziliumbwa sasa anaposema *ataifanya siku ina maana
ni siku ambayo haikuwepo na ni tofauti na zile siku za kawaida na hii siku ni
maalumu kwa ajili ya kukusaidia ili usiangamie. Tunakwenda sawa sawa..
Sasa anaposema siku ile inakuja ina maana sio
siku nzuri (hapa nazungumzia siku ya kwenye Malaki 4:1-3). Na hiyo siku ni ya
kuteketeza au siku ya uharibifu sasa hii ni tofauti na ile siku ya kwenye
Malaki 3:16-18. Ndio maana ukitoa sadaka yako Mungu anaiweka kwenye kitabu cha
kumbukumbu kwa ajili ya kukutengenezea siku ili kuja kukutoa au kukuokoa na
katika siku ya uharibifu. Na ile Mungu kukuandalia siku ina maana anakuja
kukutembelea yaani anapanga special .. ziara maalumu kwa ajili yako .
*4
SADAKA HIYO YA UKUMBUSHO INAMFANYA MUNGU AKUKUMBUKE WEWE NA JAMAA YAKO NA
RAFIKI ZAKO KWA SABABU YA SADAKA YAKO ULIYOITOA*
_”Matendo
ya Mitume 10:23-24 23 Akawakaribisha wawe wageni wake. Hata siku ya pili, Petro
akaondoka akatoka pamoja nao, na baadhi ya ndugu waliokaa Yafa wakafuatana
naye. 24 Siku ya pili yake wakaingia Kaisaria. Na Kornelio alikuwa akiwangojea,
hali amekusanya jamaa zake na rafiki zake.”_
Siku ile ambayo Malaika anaenda kumtembelea
Kornelio na kumwambia Yale yampasayo kufanya alikuwa na marafiki zake yaani
walipewa VIP treatment kwa sababu ya sadaka za Kornelio zilizokuwa zimewekwa
kwenye kitabu cha kumbu kumbu cha Mungu. Wayahudi walikuwa wanashangaa sana
kuwa imekuaje sasa hili jambo, lakini Yesu ndiye mwenye control ya vitabu ni
Yesu ambaye aliangalia kwenye vitabu vya kumbukumbu mbinguni na kuona inatakiwa
Kornelio apewe maelekezo juu ya juu ya mambo yampasayo kufanya.
>>Sadaka
za aina hii huwa zinatoa VIP treatment ya Mungu kuja kukupa instructions kwa
watu wake _Mwanzo 19:29 Ikawa Mungu alipoiharibu miji ya Bondeni, *Mungu
akamkumbuka Ibrahimu, akamtoa Lutu katika maangamizi alipoiangamiza miji hiyo
aliyokaa Lutu*._
>>Lutu
alipona kutokana na sadaka alizokuwa anatoa Ibrahimu kwa Mungu, haijalishi wako
Sodoma na Gomora lakini Mungu alimkumbuka kwa sababu ya Ibrahimu, hii neema
sana kukumbukwa na Mungu kwa ajili ya sadaka ya mtu mmoja.
>>Pia
kwa ajili hiyo maandiko yanasema _*’’Kumbukumbu la Torati 2:9Bwana akaniambia,
usiwasumbue Wamoabi, wala usishindane nao katika mapigano; kwa kuwa sitakupa
katika nchi yake kuimiliki; kwa sababu Ari nimewapa wana wa Lutu kuimiliki’’*_
>>
Umeona hata wana wa Israel hawakuweza kupigana na wana wa Lutu, Mungu
aliendelea kuwakumbuka kwa ajili ya ile sadaka aliyotoa Ibrahimu, na
wanakumbukwa mpaka leo. Tunakwenda sawa sawa.
_Kutoka
2:24-25 Mungu akasikia kuugua kwao, *Mungu akakumbuka agano lake alilolifanya
na Ibrahimu na Isaka na Yakobo*. Mungu akawaona wana wa Israeli, na Mungu
akawaangalia._
Hapa
tunaona namna Mungu alivyowakumbuka wana wa Israel, kwa sababu si ya kilio chao
bali ni kwa sababu aliangalia agano alilofanya na Ibrahimu na agano alilifanya
kwa njia ya sadaka na ndio maana maandiko yanasema _*Zaburi 50:5 Nikusanyieni
wacha Mungu wangu Waliofanya agano nami kwa dhabihu*_
Sasa
katika kiingerea wamesema Sacrife yaani sadaka na sadaka ilitolewa angalia
Mwanzo 15:8-19 Akasema, Ee Bwana MUNGU, nipateje kujua ya kwamba nitairithi?
Akamwambia, *Unipatie ndama wa miaka mitatu, na mbuzi mke wa miaka mitatu, na
kondoo mume wa miaka mitatu, na hua, na mwana njiwa*. Akampatia hao wote,
akawapasua vipande viwili, akaweka kila kipande kuelekea mwenzake, ila ndege
hakuwapasua. Hata tai walipotua juu ya mizoga Abramu akawafukuza. Na jua
lilipokuwa likichwa usingizi mzito ulimshika Abramu, hofu ya giza kuu
ikamwangukia. Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa
mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa
miaka mia nne. Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye
watatoka na mali mengi. Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa
katika uzee mwema. Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa
Waamori bado. Ikawa, jua lilipokuchwa likawa giza, tazama, tanuru ya moshi na
mwenge unaowaka ulipita kati ya vile vipande vya nyama. *Siku ile Bwana
akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa
Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati*,
Umeona
hapo uhusiano wa sadaka na agano, ndio maana pale katika Kutoka Biblia inasema
Mungu alilikumbuka agano na agano ndilo hilo nililokuonesha hapo juu. Na ndio
maana katika matendo ya mitume tunaona Mungu akimtuma malaika na kuwambia
Kornelio aende kwa Petro yaani kupata instructions. Na kwa wana wa Israel Mungu
alimtuma Musa, maandiko yanasema _Kutoka 6:2-5 Kisha Mungu akasema na Musa,
akamwambia, Mimi ni YEHOVA; nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama
Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao._
>>Walitolewa
Misri kwa sababu ya kumbukumbu na ndio maana siku ile walipojirahibu nafsi zao
Musa alisema _Kutoka 32:13-14 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli,
watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha
kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena
nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele_ ndio maana Mungu aliacha, kwa
sababu ile sadaka aliyoitoa Ibrahimu katika lile agano ilikuwa inambana Mungu
kwa sababu aliahidi kufanya kuwapeleka Kanani. Japo walikuwa wanaabudu ndama
bado walipewa VIP treatment kwa sababu ile sadaka ya Mzee Ibrahimu na Mungu
aliendelea kuwakumbuka.
>>Japo
shetani alimtengenezea Yusufu mashtaka ya uongo na kutupwa jela na kusahauliwa
kwa miaka miwili jela lakini Mungu alihakikisha Farao anaota ndoto na ile ndoto
Yusufu aliitafsiri na baadae alitolewa jela na akawa huru na kuwa waziri mkuu.
Leo ni siku yako ya wewe Mungu kukumbuka saa ikifika hamna mtu wa kukuzuia na
ataikumbuka sadaya yako na atawavusha na ndugu zako.. ooh haleluyaa haleluyaaa.
>>
Hata Paulo alipo okoka na alikuwa hakubaliwi na wanafunzi, Mungu alimuinua
Anania na alipomwekea mikono na Kumwacha Paulo alijua kuwa atakubalika kwa
wanafunzi, lakini haikuwa hivyo, na bado Mungu alimwinulia Barnaba wa kumtambulisha
kwa wanafunzi hadi alikubalika maandiko yanasema na walipoona neema niliyopewa
walinipa mkono wa shirika, na wewe leo ni siku yako kupitia sadaka yako
unayoitoa Mungu atakukumbuka na kukuinulia watu mbele yako ili kukuvusha kwa
hiyo usikate tamaa.
_*’’Mwanzo
30:22-24 Lea akasema, Mungu amenipa mahari njema, sasa mume wangu atakaa nami,
kwa kuwa nimemzalia wana sita. Akamwita jina lake Zabuloni. baadaye akazaa
binti, akamwita jina lake Dina. Mungu akamkumbuka Raheli; Mungu akamsikia,
akamfungua tumbo’’*_
>>Lea
alipozaa mtoto alijua ndiyo nafasi kupendwa na Mungu alimpomkumbuka Raheli,
haikuwa mimba ya kawaida maana ndiyo mimba iliyombeba Yusufu na Yusufu alikuwa
kabeba kitu kikubwa sana. Pia ukisoma katika kitabu cha Samweli utakutana na
habari za Hana, na utaona namna Hanna alivyotoa sadaka ya nadhiri ya kumtoa
Samweli kama mtumishi wa Mungu na Mungu alimwezesha kumpata mtoto.
>>Ukijua
kilichoko ndani ya Sadaka, nakwambia utamtafuta Mungu kwa spidi sana maana
sadaka ya Ibrahimu ilimfanya Mungu akumbuke kizazi chake kilichokuwa Misri kwa
miaka 400. Na Mungu alikitoa kizazi cha Ibrahimu utumwani.
*5
Unatoaje sadaka iwe ukumbusho mbele za Mungu*
>>Kuna
tofauti gani kati ya sadaka unayoitoa kuwa ukumbusho kwa Mungu au Sadaka ya
Hazina.
Sadaka
ya ukumbusho inamfanya Mungu kakuumbia siku maalumu ya kuja kukutoa kwenye
shida
*i)
Toa sadaka kwa imani ili Mungu asikusahau siku ya uhitaji wako mkubwa na
aingilie kati*
_Waebrania
11:1,31 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo
yasiyoonekana., Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao
walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani._
Toa
sadaka yako kwa Imani, maana hiyo sadaka itakusaidia sana kuvuka katika magumu
utakayokutana nayo au kukutoa kwenye hali hiyo, sadaka aliyoitoa (Ya
kuwakaribisha wapelelezi) Rahabu ilikuwa msaada sana kwake
Ukisoma
_Yoshua 2:9-13 akawaambia wale wanaume, Mimi najua ya kuwa Bwana amewapa ninyi
nchi hii, na ya kuwa hofu imetuangukia mbele yenu, na ya kuwa wenyeji wote wa
nchi wanayeyuka mbele yenu. Maana tumesikia jinsi Bwana alivyoyakausha maji ya
bahari ya Shamu mbele yenu, hapo mlipotoka Misri, tena mambo hayo mliyowatendea
wafalme wawili wa Waamori waliokuwa huko ng’ambo ya Yordani, yaani, Sihoni na
Ogu, mliowaangamiza kabisa. Na mara tuliposikia hayo mioyo yetu iliyeyuka, wala
haukusalia ujasiri wo wote katika mtu awaye yote, kwa sababu yenu; kwa kuwa
Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu, katika mbingu juu na katika nchi chini.
*Basi sasa, nawasihi, niapieni kwa Bwana, kwa kuwa nimewatendea ihisani, ya
kwamba ninyi nanyi mtaitendea ihisani nyumba ya baba yangu; tena nipeni alama
ya uaminifu*; ya kwamba mtawaponya hai baba yangu na mama yangu, na ndugu zangu
wanaume na wanawake, na vitu vyote walivyo navyo, na kutuokoa roho zetu na
kufa._
>>Kilichokuwa
ndani ya Rahabu ni imani na ndio maana aliamini kuwa watu hawa walipoingia
kwake na yeye alisema ndio sehemu yenyewe ya kutokea na aling’ang’ana na
aliomba Mungu amtoe kwenye ile hali ya ukahaba aliyokuwa nayo. Na ndio maana
maandiko yanasema kuwa Yoshua aliwaambia kuwa watakapofika katika ile nchi ya
Yeriko wasije wakamsahau Rahabu, na walipomchukua Rahabu tunaona wakimuweka nje
ya matuo maana walikuwa hawaamini kabisa kuwa anaweza changamana nao, lakini
baadae tunaona akija kuingia katika ukoo wa Yesu.
*ii)Unganisha
sadaka hiyo na maombi*
_Isaya
43:26 Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako._
eleza mambo yako unapokuwa unapeleka sadaka yako kwa Mungu.
*iii)
Kuna maombi yanayowekwa kwenye kumbukumbu za Mungu juu mbinguni*
>>Mungu
alimwambia Kornelio kuwa sadaka na sala zako zimefika Mbinguni, na kuwa
ukumbusho mbele za Mungu.
Mwaka
1985 nilikuwa naombea nchi kuwa Mungu atuinulie watumishi wazawa, na nakumbuka
ilikuwa siku moja (saa za kazi) kule Arusha nilienda kwa mchungaji wa Anglican,
na niliomba ufunguo wa kanisa na nilienda madhabahuni na niliomba Mungu naomba
tuinulie watumishi wazawa kama ulivyofanya kwa nchi zingine. Na utakapowanuia
naomba usinisahau na *kweli Mungu hajanisahau mpaka leo kanikumbuka* na kipindi
kingine nilikuwa naamka usiku kuomba na bendera ya Tanzania na ndipo Mungu
alinifundisha kutoa sadaka kila msimu, kila msimu mpya ukianza huwa natoa
sadaka, ili Mungu anisaidie.
>>Hii
siku haikuwepo kabisa na Mungu kaifanya maalumu kabisa, Mzee Mmanyi anajua kitu
naongea. Lakini Mungu kaifanya maalumu siku ya leo hapa Diamond jubilee.
*iii)
Unganisha na wimbo wa kumtukuza Mungu*
>>Hesabu
10:10,9 _Tena katika siku ya furaha yenu, na katika sikukuu zenu zilizoamriwa,
na katika kuandama miezi kwenu, *mtapiga hizo tarumbeta juu ya sadaka zenu za
kuteketezwa, na juu ya dhabihu za sadaka zenu za amani; nazo zitakuwa kwenu ni
ukumbusho mbele za Mungu wenu; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu*_.
_Tena
hapo mtakapokwenda kupiga vita katika nchi yenu, kupigana na adui awaoneaye
ninyi, ndipo mtakapopiga sauti ya kugutusha kwa tarumbeta; nanyi mtakumbukwa
mbele za Bwana, Mungu wenu, nanyi mtaokolewa na adui zenu_.
>>Kama
unatoa sadaka na kuna hali ndani unasikia kuimba endelea na huo wimbo usiache
endelea nao na imba, na siku umepata shida utaona huo wimbo ukikurudia na
utashangaa msaada wa Mungu ukikujia. Na Mungu atakukumbuka na kukusaidia. Mwaka
huu kule Arusha kwenye semina dada mmoja alikuja kushuhudia ambavyo Mungu
alimsaidia kupata mtoto baada ya kukosa mtoto kwa miaka 9. Na kampa jina lake
Christopher kwa sababu siku moja nilienda wanapofanya kazi na nilikuwa
nimemsindikiza mke wangu. Nilipokuwa kwenye gari binti alikuja na akanieleza
kuwa baba nina shida ya mtoto sijapata kwa miaka 9 sasa. Na nilimuuliza unataka
mtoto wa aina gani akainiambia wa kiume na nilimuombea nikiwa kwenye gari,
baada ya muda akapata mimba na sasa kajifungua mtoto wa kiume kama tulivyoomba.
*iv)
Unapokula chakula cha Bwana, na unganisha na moambi ili jambo lako liwe
ukumbusho mbele za Mungu*
>>Yesu
alisema fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu, haijalishi unapita mazingira gani
siku ya leo Mungu akukumbuke na akusaidie na unapota sadaka hakikisha unaomba
na tamka nano.
*Mungu
akubariki sana kwa kusoma somo hili, na liweke kwenye matendo hakikisha unatoa
sadaka yako kwa Mungu na hakika Mungu atakukumbuka, Kasome biblia na angalia
sadaka moja ya Ibrahimu aliyoitoa inadumu mpaka leo, na wewe fanya hivyo Mungu
atakumbuka kizazi chako. Bwana akubariki na uwe na mwaka mwema 2017 ukafanyike
Baraka sana kwako na hakika ukamuone Mungu akikusaidia na kukuvusha*.
Kupanda
Kanda hii ya somo hili piga namba hii 0754249590 au 0754766517
Ubarikiwe
sana na kila la kheri.
0 Comments