MWL. CHRISTOPHER MWAKASEGE
UTANGULIZI
Wafilipi 4:6-7
“Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika
kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na
Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia
zenu katika Kristo Yesu.”
Swali ninalotaka kujibu ni hili linalosema
“KWANINI TUYAOMBEE TUNAYOTAKA KUYAFANYA WAKATI
TUNAWEZA KUYAFANYA BILA KUYAOMBEA?”
Kwa sababu una malengo yako mwaka huu
(biashara, kazi fulani, masomo). Ni mara nyingi watu wengi huombea vile vitu
ambavyo hawana uwezo wa kuvifanya hapo ndipo huona kuwa wanamhitaji
Mungu. Lakini mambo mengine huwa hawaombi na kama wanaomba basi ni watu
wachache sana ambao wanaombea kila jambo.
Lakini huo mstari unasema tusijisumbue na neno
lolote, bali katika kila neno (kila tunachokifanya). Hii ni kati ya mistari
iliyonisumbua tokea pale nilipookoka miaka ile ya 1980s na Mungu alinisukuma
sana hasa kwenye heshima ya neno la Mungu na suala la maombi. Kwa hiyo hili
jambo nilienda nalo kwa muda mrefu sana hasa katika uhusiano kati ya mtu na
Roho Mtakatifu na kujua Mungu anataka nijue nini kuhusu maisha.
Kwa hiyo kuna mambo manne yaliyonisumbua sana
tangu wakati huo Nilipo okoka.
Nikiwa nasoma kuhusu maombi mstari wa Wafilipi
4:6 - 7 ulinisumbua sana kuelewa kwa sababu Biblia inasema “kila
neno kwa kusali”. Unaombaje kila wakati na kila leo? Ukisoma mahali pengine
panasema “dumuni/kesheni katika kuomba”. Ningekuwa nafikiri kibinadamu ingekuwa
tabu sana maana sasa nina ufahamu kidogo na kupata kusoma mistari
mbalimbali kwenye Biblia na kuelewa maana yake nini.
Nilijiuliza, unadumuje kwenye maombi wakati
unafanya kazi?. Kwa maana hiyo ni rahisi sana ukaacha kazi na kukaa kwenye
maombi ukafikiri ndio Mungu anataka. Roho Mtakatifu anaweza akakuambia unatega
kazi “nenda kafanye kazi”.
Tunapo omba maombi ya mwaka huu 2019, natamani
tupate angalau majibu machache kuwa “kwa nini tuombee kila tunalotaka kufanya
2019? Na kwa nini tusiyafanye bila kuombea kila jambo?” Ziko sababu nyingi sana
ndani ya Biblia lakini mimi nataka nikupe nne tu ambazo Mungu amenipa. Sababu
hizo ni:-
SABABU
YA KWANZA
1. BILA MSAADA WA MUNGU, HATUWEZI KUFANYA
TUNACHOFANYA KWA KIWANGO CHAKE MUNGU
Yohana 15:5
“Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye
ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi
kufanya neno lo lote.”
Waefeso 2:10
“Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo
Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili
tuenende nayo.”
Hapo kwenye Yohana 15:5 Yesu mwenyewe amesema
“pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.” na hakusema pasipo mimi kuna
mambo mengine mtafanya lakini tunajua kuna vitu vingi tunafanya na Yesu
hahusiki.
Kama umesoma Biblia yako utakuwa unaelewa
Waefeso 2:10 ukiunganisha na Yohana 15:5 vitu vilivyozungwa hapo. Ukianza na
hiyo juu ya vitu ambavyo Waefeso 2:10 inazungumzia kuwa kuna mambo ambayo
tuliumbiwa nayo yaani Mungu kaweka ndani yetu na hatuyakuti hapa duniani;
tuliumbiwa tuenende nayo, tulitengenezwa maalumu kwa ajili ya vitu fulani yaani
aina fulani ya maisha. Ni sawa na Matendo ya Mitume 17:28
“Kwa maana ndani yake yeye tunaishi,
tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi
alivyosema, Maana sisi sote tu wazao wake.”
Kwa hiyo kuna vitu tuliumbiwa kitabia na
kikazi.
Kwenye Yohana 15:5 inamaanisha hakuna
mwanadamu aliyeumbwa akae nje ya Yesu halafu anafikiri atafanikiwa. Kila kitu
kiliumbwa katika Kristo lakini tuna muunganiko na Yesu ambapo hutaweza kuta
muunganiko huo katika mimea, ndege, wadudu na wanyama. Binadamu ni kiumbe
ambacho Mungu alikiumba kwa mfano wake kwa kumwekea sura na roho yake.
Mwanadamu haku umbwa ili ajitengeneze au
amtengeneze mwanadamu mwingine; Mungu tayari ameshaweka sura na roho yake ndani
ili mwanadamu anapozaa azae mtu ambaye ana sura na mfano wa Mungu na kupaswa
kuenenda Ki-Mungu na kwa kiwango cha Mungu.
Dhambi ilipoingia kitu kibaya kimojawapo
iliichofanya ni kutunyang'anya uso na mfano wa Mungu ndani yetu. Kwa
kutunyang'anya vitu tunavyovifahamu kama uzima wa milele na uzima wa Mungu
ndani yetu lakini Yesu alipokuja alisema katika
Yohana 10:10
“mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe
nao tele.”
Uzima ni maisha ya Mungu ndani ya mtu
iliyodhihirishwa ndani ya Kristo. Huwezi kupata huo uzima kama hutamjua huyo
Mungu katika Kristo Yesu sawa na Yesu alivyosema katika
Yohana 17:3
“Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe,
Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.”
Kwa hiyo huwezi kuwa na uzima wa milele kama
hujamjua Mungu katika Kristo Yesu. Na huu uzima wa milele ni Uungu ndani ya
mtu. Ni uzima wa Mungu ndani ya mtu ambao dhambi ilipoingia iliondoa ndani ya
mtu, na baada ya kuondolewa ndani ya mtu kukatokea kitu kinaitwa udhaifu ndani
ya mwanadamu.
Tangu wakati huo mwanadamu bila Mungu hawezi
kufikia kiwango kile ambacho Mungu alimkusudia kukifikia, ni Adamu peke yake mpaka
wakati huo ambao Yesu alipozaliwa na alipokufa msalabani na akafufuka na watu
wakaanza kuokoka na Yesu akaanza kuingia ndani yao ndio kidogo kidogo tunaanza
kuonja maana yake nini Mungu alikuwa amekikusudia ndani ya Adam kabla dhambi
haijaingia. Kwa sababu tulikuwa hatufahamu na sidhani kama tumefikia hiyo picha
kwamba mwanadamu aliumbwa na kitu cha namna gani na Mungu alimuwekea kitu gani
ndani yake na faida ya kuwa na Mungu katika maisha ni nini na hasara za
kutokuwa naye ni nini.
Kuna namna ambavyo Mungu alimuumbia mtu na
akibadilisha vitu vyovyote ndani yake kila kitu kinaharibika. Mfano mzuri ni
kutumia gari ya diesel kuweka mafuta ya petrol. Na ndivyo mwanadamu alivyofanya
alikataa Roho ya Mungu akachukua roho ya shetani halafu anaendelea na maisha
akifikiri yuko sahihi. Vile vitu ambayo havikuwa vya kawaida vimekuwa vya
kawaida. Mungu anapotutazama anatutazama katika kiwango ambacho tulitakiwa tuwe
na twende nacho
Hivyo ni muhimu sana uweze kujua hili ya
kwamba dhambi ilipoingia ilitunyang’anya uzima wa Mungu ndani yetu, maana yake
maisha ya Mungu ndani yetu ambayo kwa sasa tunayapata ndani ya Kristo. Ndiyo
maana tunapokuwa ndani ya Kristo tumesulubiwa pamoja na Kristo siyo sisi
tunaoishi bali Kristo ndani yetu, uhai tulionao tunauona katika imani ya Mwana
wa Mungu aliye hai aliyekufa na kufufuka kwa ajili yetu. Unapokuwa ndani ya
Kristo huwezi tena kuishi kwa ajili yako mwenyewe bali unaishi kwa ajili yake
yeye aliyekufa kwa ajili yako.
Ndiyo maana Biblia inasema kwenye
Luka 9:23 ya kwamba
“Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka
kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.”
Maana yake ni kwamba huwezi tena ukaishi
kibinafsi, nafsi yako haiwezi tena kuwa na agenda yoyote kwenye maisha yako
bali agenda yako inapotea saa ile unapomkaribisha Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa
maisha yako, agenda yako inaisha na ndani yako inaanza agenda ya Yesu. Agenda
ya Yesu ni ile ambayo tokea awali alikuumbia ili uweze kuenenda nayo ya kwamba
utakapokuwa pamoja naye ufanye yale yake na yale yote akuagizayo.
Kwa hiyo sababu mojawapo ya kuingia kwenye
maombi ni kumwambia Mungu;
pasipo wewe siwezi kufikia kiwango unachotaka,
pasipo wewe siwezi kufikia kiwango ulichoweka juu yangu
pasipo wewe siwezi kufikia kiwango ulichoweka juu yangu
Hakuna mwanadamu ambaye anaweza kukuwekea
hicho kiwango, kiwango kipo ndani ya Biblia, na utakikuta ndani ya Kristo na
ndiyo maana Biblia inasema “kuweni mpaka mfikie kimo cha utimilifu wake
Kristo" huwezi kukipata kiwango hiki nje ya Kristo bali utakipata ndani ya
Kristo.
Kumbuka kuna kimo/kiwango Mungu alikikusudia
katika jambo lolote unalolifanya. Huwezi kukipata mahala pengine isipokuwa
ndani ya Kristo. Na unapoingia kwenye maombi ni ishara ya kumwambia Mungu
ninahitaji mkono wako katika hili maana pasipo wewe mimi siwezi kufanya katika
kiwango unachotaka.
SABABU
YA PILI
2. MAOMBI YANAMPA MUNGU NAFASI YA KUWA MTENDA
KAZI PAMOJA NAWE/NASI
1Wakorintho 3:9
“Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu;
ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.”
Waefeso 3:20
“Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya
ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo
kazi ndani yetu;”
Yesu anapoingia ndani yako hakupi tu
uzima wa milele wala kuishi tu ndani yako bali anataka aishi pamoja na wewe.
Kwa hiyo anakuwa mtendaji pamoja na wewe. Tabia unayokuwa nayo ya ki-Mungu siyo
yako ni ya Mungu lakini Mungu anataka ujue namna ya kushirikiana na hiyo mbegu
ya tabia iliyoko ndani yako. Anataka ujue namna ya kushirikiana na Roho
Mtakatifu aliye ndani yako ili usifanye kitu peke yako wala kwa nguvu zako
mwenyewe bali mshirikiane kufanya jambo analotaka mfanye pamoja.
Na kwa sababu unapozaliwa mara ya pili
nguvu za Mungu na Roho Mtakatifu anapokaa ndani yako, Mungu anakupa
nafasi ya kuingia na kuendelea kukaa hapa duniani. Roho Mtakatifu atakufundisha
kujifunza, kutenda, kutembea na kuishi pamoja na Yesu kila siku za maisha yako.
Waefeso 3:20 inaeleza namna ambavyo Mungu
anajibu kuliko yale tuyaombayo au tuyawazayo. Kwa sababu unaweza uka tune
mawazo yako yakaa kimaombi au kukaa kiuhitaji kumhitaji Mungu masaa yote. Kwa sababu
Yesu anaishi ndani yako ataona ndani yako kabla ya kusikia kwenye mdomo
wako wakati unaomba kwa sababu sio wewe unayeishi ila yeye anaishi ndani yako.
Kwa maana mawazo yanayokuja ndani yako ya ni yake, Lakini kama mawazo
mengo yanayokuja ndani yako ni ya Shetani unahitaji kusoma Biblia vizuri ili
ujue kwanini mawazo mengi yanayokujia ni mabaya!.
Kama umeokoka wazo linalokuja ndani yako
jifunze kulipa nafasi ya kwanza na kama bado unapambana huko ndani hakikisha
una Neno la kutosha kwa sababu Neno linakusaidia kukarabati nafsi yako
ubadilishe namna kufikiri ili uweze kufikiri jinsi Mungu alivyokuuumba
anatengeneza utu mpya na utu wa kale unaondolewa.
Neno la Mungu linakusaidia kukukarabati na
kuweka ndani yako mtazamo mpya na fikra mpya. Ukiona mawazo yanakusumbua
tatitizo sio kwamba hujaokoka ila huna Neno ndani na kama lipo basi hujalipa
heshima linalostahili kwenye maisha yako. Kwa sababu kama umekufa ndani ya
kristo wazo la kwanza halitakuwa la kwako litakuwa la Yesu na kama Yesu yupo
ndani yako shetani hawezi kuanza kabla ya Yesu.
Ndio maana anasema kabla hujanena alisikia na
kujibu alisikia lini na wapi? Alisikia moyoni mwako! Kwa sababu anajua nini
unachohitaji kabla hujaomba lakini kwanini anataka uombe ni kwa sababu ya shida
iliyotokea kwenye bustani ya Edeni!
Mwandamu alimkataa Mungu na hapo ndipo haja ya
maombi ilipokuja kabla dhambi haijaingia maombi hayakuwepo. Kulikuwa na
fellowship (ushirika) hatukuhitaji barua ya appointment kumsikia Mungu
hatukuhitaji itifaki ya kwenda mbinguni kuzungumza na Mungu, tulikuwa watoto
wake, ndio maana watoto wako hawana haja ya itifaki kuja kukuona. Kuna namna
watakuja kwa kuwa wanajua huyu ni baba na huyu ni mama si kwamba hawata
kuheshimu hapana bali wanajua huyu ni mzazi wetu. Ni tofauti sana na mtoto
ambaye alikukosea anapokuja kwa sababu kwanza hana uhakika kama utamkubalia kwa
hiyo inabidi ataengeneze itifaki ya namna ya kuja ili apate msaada kutoka
kwako.
Tangu tulipomkataa Mungu mwanadamu akitaka
msaada wa Mungu lazima apeleke ombi kwamba Mungu nahitaji msaada ndipo apewe
msaada. Hapo ndipo maombi yalikotoka yakaja yakasambaa kwa style tofauti
tofauti. Maana yake Mungu anasema mlinikataa kama mnanihitaji mtaniita na
akaweka itifaki kwenye Biblia ya kukubalia na kuja kufanya kazi pamoja na wewe
kwa maombi kwanza.
Ukisoma kitabu cha Mwanzo humuoni Adamu
akimuita Mungu kuja kwenye bustani lakini sasa tunamuita Mungu kuja kwenye
ibada, ofisini, kwenye semina, ndoa, kazi nk. Baada ya kumkataa Mungu adamu
alifukizwa kwenye bustani na Malaika wakawekwa kulinda. Tangu wakati huo
kama unamtaka Mungu ni lazima ufuate utaratibu, lazima upeleke request,
ndio maana maombi yanampa Mungu nafasi ya kuwa mtenda kazi pamoja na wewe.
Ukishaokoka kuna watu wengi wanaacha baadhi ya
maombi kwa sababu wanafikiri wana kila kitu na ni kwa sababu hawajui ngazi
tofauti tofauti za maombi yana. Kwa sababu kuna maombi ya kusema nataka
Mungu uende namni katika hili au hili lakini kadri unavyoendelea kukua huwezi
kuomba kama unavyotaka. Maana utakuwa unaomba namna ya kuombea mapenzi ya
Mungu kwanza katika maisha au mwaka ulionao. Hii ni kwa sababu unatafuta kwanza
mapenzi yake na si ya kwako.
Pamoja na kwamba Mungu amesema omba
lolote nami nitakupa kuna ngazi huwezi kuomba lolote
kwa sababu utakuwa mwangalifu sana unapoomba. Si kila kitu unachoomba ni
mapenzi yake akupe mengine amekupa kwa sababu umeng’ang’ania tu, uking’ang’ana
unapewa lakini si kila kitu unachoomba ni mapenzi ya Mungu. Wana wa Israel
waling’ang’ana wapewe nyama lakini akawakondesha mioyo yao.
Kwa hiyo kuna ngazi tofauti za maombi kadri
unavyokua kiroho maombi yanabadilika. Hata watoto wako kadri wanavyo kua na
wanaendelea kukufahamu kitu wanachokuja kuzungumza na wewe kina badilika ndipo
inakuja ile
Waefeso 3:20
Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya
ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo
kazi ndani yetu;
Kwa hiyo kuna maombi ambavyo siyo kwa ajili ya
kuzungumza na Mungu lakini ni maombi ya kuhakikisha nguvu zilizoko ndani yako
zinaingia kazini zinaenda kwenye eneo lile unaloliombea na kutengeneza hicho
kitu ambacho unakiombea na kukusaidia.
Mungu hajibu kwa kadri ya nguvu inayotoka
mbinguni anajibu kwa kadri ya nguvu inayotenda kazi ndani yako.
Kwa hiyo kama una upako 100% na unaotenda kazi
ni 10% majibu ya maombi yako yatatokana na 10% haijalishi 90% uliyonayo ndani
yako.
Mfano Tanesco wanaku charge kwa umeme unaotumia
sio umeme unaoingia ndani yako na kukaa tu na umeme usio tumia hauna faida kwa
Tanesco na hauna faida kwako maana hautumiki.
Upako usioutumia hauna faida kwako na
kwa Mungu. Njia mojawapo ya kufanya upako ufanye kazi ndani yako ni
maombi. Kama unataka kumuona Mungu katika kila jambo unalofanya unahitaji
kufanya maombi kulingana na nguvu itendayo kazi ndani yako
Ukisoma kama ninavyosoma utaanza kuona heshima
ya Mungu kila eneo. Haijalishi niwe nahubiri au niwe nimesimama kwenye vikao
vya umoja wa mataifa ninazungumza habari za uchumi maombi ninayoomba hapa ni
sawa sawa na maombi ninayoomba minaposimama na wataalam wa uchumi kule.
Wakinitazama wakati naongea wanajua ninajua
kila kitu lakini kumbe ninae Mungu aliye hai ambaye ananipa kitu cha kusema
.Nikimaliza kuongea waandishi wa habari wananizunguka wanaanza kuuliza umetokea
wapi! sasa tukuitaje doctor! Wanatafuta kila cheo kinachoendana na kitu
nilichosema halafu wanashangaa nakataa kila cheo na wanasema haiwezekani. Kwa
sababu ninacho zungumza wakati huo ni cha ngazi ya juu sana.
USHUHUDA
Niliandika siku moja andiko la kuweka
changamoto juu ya watalaamu wa uchumi ulimwenguni waliobuni mbinu mbali
mbali za kukuza uchumi wa nchi tofauti tofauti na likasambaa kwenye
vyombo vya uchumi huko Duniani.
Baada ya muda nikapigiwa simu kuwa natakiwa
niende Washington DC Marekani kwa ajili ya kwenda “kupresent” kila
nilichoandika kwenye lile andiko maana kutakuwa na mkutano wa wataalaam wa
uchumi duniani.
Wakanitumia makaratasi ya watu watakao
hudhuria kikao hicho. Nilishangaa sana maana kulikuwa na watu ambao ndio watu
walioandika Vitabu vya uchumi na ndio waliobuni uchumi wa Marekani na World
bank na Nchi tofauti tofauti duniani hata nchi zetu zinazoendelea. Na mimi
nilikuwa miongoni mwa wazungumzaji wa siku hiyo.
Sasa hapo niliomba kuliko
kufikiri. Japo nilikuwa nasoma maana Biblia inasema fanya bidii kusoma
kwa sababu Roho Mtakatifu hakocopy na kupaste. Lakini unaweza ukasoma na
usielewe na ukaelewa na ukashindwa kujieleza. Hapo ndipo unahitaji msaada wa
Mungu.
Kwa hiyo niliomba sana kumkaribisha Mungu
anisaidie katika kueleza maswali niliyouliza na kwanini nimepinga hili kwanini
haliwezi kufanikiwa labda liende kwa style nyingine.
Nilipoenda kwenye mkutano niliomba Mungu na
niliweza kuongea kitu ambacho Mungu alinipa kuongea na nilijibu Maswali yao
yote. Nilipokuwa nimesima pale alikuwa Yesu ndani yangu anaongea na kilitoka
kiingereza safi kabisa hata mimi nilishangaa. Wale watalaam walinitazama sana
na walishangaa sana.
Nilipomaliza mtu mmoja akaniuliza unafanya
kazi serikalini? nikamjibu hapana. Wakauliza tena sasa unapofuatalia sana
masuala ya uchumi wakati wewe hufanyi kazi serikalini sasa umetumwa na nani?.
Huwa nawajibu kuwa mimi ni mtumishi wa Mungu na kazi mojawapo ambayo Mungu
kanipa ni kufuatilia masuala ya uchumi.
Mtu ambaye ni Dereva na akajifunza kumuomba
Mungu aingie kazini anapokuwa anaendesha gari. Huwa hachoki akiwa kazini
anachoka wakati kamaliza kuendesha maana kuna kitu kinamshikilia maana nguvu za
Mungu zinatenda kazi ndani yake.
Yesu anapokuwa ndani yako, ukajifunza kuomba
aachilie nguvu ndani yako katika kile unachofanya utaona msaada mkubwa saba.
SABABU
YA TATU.
3. MAOMBI NI ISHARA KWA MUNGU KUWA UNAHITAJI REHEMA
ZAKE KILA SIKU
Maombolezo 3:22
Ni huruma za Bwana kwambahatuangamii, Kwa kuwa
rehema zake hazikomi.Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu.Bwana
ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye.
Rehema sio neema. Biblia inasema katika
Waebrania 11:6
Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza;
kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa
thawabu wale wamtafutao.
Mtu yeyote aliye na Mungu anajua umuhimu wa imani katika kutembea na Mungu na katika kupokea majibu ya maombi yake. Imani ina sehemu kubwa.
Mtu yeyote aliye na Mungu anajua umuhimu wa imani katika kutembea na Mungu na katika kupokea majibu ya maombi yake. Imani ina sehemu kubwa.
Sasa inapokuja kuwa imani imepotea, imani
imetindika na umekata tamaa kabisa au umepita mahali pagumu na pamenyang’anya
imani yako kabisa Lakini Biblia inasema Pasipo Imani haiwezekani kumpendeza
Mungu.
Kama una mstari mmoja kwenye Biblia inatosha
kukukatisha usiombe tena. Kuna kitu kinaitwa rehema. Rehema ni
huruma na uaminifu wa Mungu kwa agano lake.
Kuna wakati unapita mahali pagumu ambapo
pananyang’anya kabisa imani yako na unakata tamaa huoni kama Mungu anakusikia.
Au kuna jambo unaomba na huoni kama Mungu hakusikii lakini huwezi kuishi
bila Mungu.
Biblia inasema rehema zake ni mpya kila siku
maana yake ni rehema ni za kila siku. Sasa si kila wakati zinakuja maana ni
lazima awepo mtu anayeomba. Akiomba kuwa Mungu naomba umrehemu huyu akisha sema
namna hiyo maana yake anamwambia Mungu tazama uaminifu wako uliomwachia mwanao
pale msalabani Damu yake ikamwagika, ulimfia hajakujua, ulimsamehe na hajaomba
msahama ulikuwa tayari kumpokea wakati yeye bado hajakukubali. Ee Mungu naomba
kumbuka rehema zako naomba umrehemu.
Mungu ukishamweleza namna hiyo
maana ana fadhili zake , rehema zake siku kwa siku. Ukishamweleza namna hiyo
Mungu anatazama rehema zake za siku hiyo na anatuma Malaika kusema teremka
nenda kamsaidie yule. Wewe ndani yako unasaidiwa hadi unatikisa kichwa.
“Mtu mwingine anasema Mungu yani simuelewi
maana imani yangu ilikuwa imeisha kabisa”. Katika hali ya namna hiyo huwezi
kuhesabia kuwa imani yako imekusaidia maana ni rehema za Mungu zimeingia
kazini.
Ndio maana kama imani yako imetindika na
unaona kabisa kama Mungu hakusikii usiache kupiga kelele kuwa ee mwana wa Daudi
unirehemu. Kama umeishiwa kuomba usiku wewe sema tu ee Mwana wa Daudi unirehemu
na funga macho yako. Na ukiamka asubuhi sema tena ee mwana wa Daudi unirehemu
atakusaidia siku hiyo maana ana wingi wa Rehema zakw siku kwa siku.
SABABU
YA NNE.
4. UNAWEZA KUTUMIA MAOMBI KUISAIDIA NCHI NA
WATU WENGINE
Ezekieli 22:30-31
30 Nami nikatafuta mtu miongoni mwao,
atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili
ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu. 31 Kwa sababu hiyo nimemwaga
ghadhabu yangu juu yao; nimewateketeza kwa moto wa hasira yangu; nami nimeileta
njia yao wenyewe juu ya vichwa vyao, asema Bwana MUNGU.
Mungu anasema Nami nikatafuta mtu hasemi watu
bali anatafuta mtu ambaye atambebesha mzigo kwa ajili ya nchi isije ikaangamia.
Ni upendo wa ajabu sana kuwa unamkorofisha
Mungu hataki kukuangamiza na anatafuta mtu wa kukuombea wewe kabla
haujaangamia. Inawezekana kakutafuta wewe mwenyewe uombe na hujaomba sasa
anatafuta mtu mwingine akuombee
Huu ni moyo wa tofauti sana na huwa nauona kwa
wayahudi peke yake kwenye jeshi lao. Ni jeshi pekee duniani ambalo
likitaka kupiga nyumbani ya mtu mahali huwa wanatoa taarifa dakika kumi kabla
kuwa wataangamiza nyumba fulani kwa hiyo walipo pale
wajisalimishe.Wakijisalimisja wanapona na wasipofanya hivyo baada ya dakika
kumi nyumba zao zinapigwa mabomu.
Wakitaka kuangamiza mji wanapitisha ndege
dakika kumi kabla ili kurusha makaratasi ya taarifa kuwa wanakuja
kuangamiza mji huo. kwa hiyo watu wajisalimishe baada ya hapo wanakuja kweli
kuangamiza. sasa huwa nawaza kuwa wakitoa taarifa ni kuwa wanatala
kuja kugombana na watu au na majumba?
Lakini ni roho ya ajabu sana wanayo maana
wakipiga watu kwa mabomu na watu wakajeruhiwa huwa wanawapeleka hospitali
kuwatibu.
Biblia inasema Mungu anatafuta mtu ambaye kama
kuna shida nyumbani kwenu au kazini au kwenye nchi ambaye yuko tayari kukaa
kuomba toba kwa ajili ya nchi au mahali anapotaka ukae kuomba.
Mungu anamuweka kila mtu kwa maksudi kwa
sababu Mungu hakumpamga kila mtu aliyeokoka atoke kesho aende kuhubiri. Biblia
inasema kila alie na mwana anao ushuhuda kushuhudia sio kuhubiri maana
maisha yetu ni ushuhuda. Kushuhudia ni kwa kila aliye na mwana na kuhubiri ni
kwa kila aliyepangiwa kuhubiri kwa hiyo kama ndani yako unapangiwa
kushuhudia haina maana uende kuhubiri. Ushuhudie kile ambacho Yesu alikutendea
maana ni ushuhuda kwako na kinatosha kuwavuta watu kuja kwa Yesu. Kwa sababu
kazi ya kuwaleta watu kwa Yesu sio kazi ya wahubiri tu na mikutano bali ni kazi
ya kila mmoja wetu.
Kwa hiyo maneno yetu yanatakiwa yawavute watu
kwa Yesu. Haitoshi tu kuwaleta watu kwenye mikutano na kanisani ili waongozwe
sala ya toba bali tunatakiwa tuwaongoze sala ya toba. Maana kama hujui
kumwongoza mtu sala ya toba andika kwenye karatasi na kila ukimpata mtu msomee
au unamwambia soma hapa.
Hayo ndio mazoezi yenyewe maana si wote
waliokutana na watu na kuwaongoza sala ya toba kwani walikuwa wanajua? Maana
mara nyingine walikuwa hata hawajui hata kuongoza sala ya toba. Lakini walianza
kidogo kidogo na wakaweza.
Sasa katika malengo ya mwaka huu unakuta hata
hujaweka lengo na kutaka Mungu akusaidie kuwaleta watu kwa Yesu. Utakuwa
umeweka malengo ya kuomba hela lakini hili hujaweka. Hakikisha mwaka huu lengo
mojawapo la kwako ni kuwaleta watu kwa Yesu.
Inapofika kwenye maombi Mungu anatafuta watu
waliotayari kuomba maana yake atakuwa anateremsha mzigo wa maombi ndani yao kama
wako tayari kubeba. Unakuta mtu anapata mzigo wa kuomba na haombi muda
huo anaanza kuwaza kuwa hili ntalipeleka kwenye kikundi cha maombi.
Ikifika asubuhi ule mzigo wa maombi hana tena na anaanza kusema jana nilikuwa
na mzigo wa kuomba ila sasa umetoweka. Mungu hatafuti kikundi bali anatafuta
mtu maana ulihitaji kusema ee Bwana niko hapa nisaidie niombe.
Sasa unapoanza kuomba Mungu atakusaidia maana
hata kama utashirikisha wengine lakini ndani yako unakuja tayari
umejiweka sawa kuomba maana wanaweza kuja wenzio na agenda za kwao za
kuombea na usipojua namna ya kusimamia agenda ambayo Mungu kakupa unajikuta
umehama kwenye kusudi.
Mungu anataka kukuambia kuwa kwa maombi yako
Sekta, Nchi itapona. Ukiona sekta inaangamia na wewe uko pale ujue hujawa
chumvi inayotakiwa.
Suala la maombi ni mfumo wa maisha maana ni
mawasiliano yako na Mungu kila wakati. Kuna saa unaacha kila kitu unaomba. Ile
kwamba umemaliza kuomba haina maana hutaomba tena maana maombi ni mfumo
wa maisha.
0 Comments